Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 9:1-31

  • Malkia wa Sheba amtembelea Sulemani (1-12)

  • Utajiri wa Sulemani (13-28)

  • Kifo cha Sulemani (29-31)

9  Basi malkia wa Sheba+ alisikia habari za Sulemani, kwa hiyo akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu.* Alikuja na msafara wenye kuvutia sana, pamoja na ngamia waliobeba mafuta ya zeri na dhahabu nyingi sana+ na mawe yenye thamani. Akafika mbele ya Sulemani na kumwambia mambo yote yaliyokuwa moyoni mwake.+  Kisha Sulemani akajibu maswali yake yote. Hakuna jambo lolote lililokuwa gumu sana* kwa Sulemani asiweze kumweleza.  Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Sulemani,+ nyumba aliyojenga,+  chakula kilichokuwa mezani pake,+ jinsi watumishi wake walivyoketi, jinsi watumishi wake walivyohudumu mezani na pia mavazi yao, na wale waliompa vinywaji na jinsi walivyovalia, na dhabihu zake za kuteketezwa alizotoa kwa ukawaida katika nyumba ya Yehova,+ alipigwa na bumbuazi.*  Basi akamwambia mfalme: “Habari nilizosikia katika nchi yangu kuhusu mafanikio* yako na kuhusu hekima yako zilikuwa za kweli.  Lakini sikuamini habari hizo mpaka nilipokuja na kujionea kwa macho yangu mwenyewe.+ Na kwa kweli sikuwa nimeambiwa hata nusu ya hekima yako nyingi.+ Umezidi kwa mbali habari nilizosikia.+  Wenye furaha ni watu wako, na wenye furaha ni watumishi wako wanaosimama mbele yako daima, wakiisikiliza hekima yako!  Na asifiwe Yehova Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka kwenye kiti chake cha ufalme ukiwa mfalme kwa niaba ya Yehova Mungu wako. Kwa sababu Mungu wako anawapenda Waisraeli,+ na ili kuwafanya wadumu milele, alikuweka kuwa mfalme juu yao ili utekeleze haki na uadilifu.”  Kisha akampa mfalme talanta 120* za dhahabu+ na kiasi kikubwa sana cha mafuta ya zeri na mawe yenye thamani. Mfalme Sulemani hakuwahi tena kuletewa kiasi kikubwa hivyo cha mafuta ya zeri kama alicholetewa na malkia wa Sheba.+ 10  Isitoshe, watumishi wa Hiramu na watumishi wa Sulemani ambao walileta dhahabu kutoka Ofiri,+ walileta pia mbao za misandali na mawe yenye thamani.+ 11  Mfalme alitumia mbao hizo za misandali kutengeneza ngazi za nyumba ya Yehova+ na nyumba ya* mfalme,+ na pia vinubi na vinanda vya waimbaji.+ Mbao kama hizo hazikuwa zimewahi kuonekana katika nchi ya Yuda. 12  Mfalme Sulemani alimpa pia malkia wa Sheba kitu chochote alichotamani na kuomba, zaidi ya* vitu alivyomletea mfalme. Kisha akaondoka na kurudi katika nchi yake, pamoja na watumishi wake.+ 13  Na dhahabu iliyoletwa kwa Sulemani katika mwaka mmoja ilikuwa na uzito wa talanta 666 za dhahabu,+ 14  mbali na dhahabu iliyoletwa na wafanyabiashara wasafiri na wauzaji wa bidhaa na wafalme wote wa Uarabuni na magavana wa nchi waliokuwa wakimletea Sulemani dhahabu na fedha.+ 15  Mfalme Sulemani alitengeneza ngao kubwa 200 za dhahabu iliyochanganywa na madini mengine+ (kwa kila ngao alitumia shekeli 600* za dhahabu hiyo)+ 16  na ngao ndogo* 300 za dhahabu iliyochanganywa na madini mengine (kwa kila ngao ndogo alitumia mina tatu* za dhahabu). Kisha mfalme akaziweka katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni.+ 17  Mfalme pia alitengeneza kiti kikubwa cha ufalme cha pembe za tembo na kukifunika kwa dhahabu safi.+ 18  Kiti hicho cha ufalme kilikuwa na ngazi sita, nacho kiliunganishwa na kiti cha miguu cha dhahabu, na kilikuwa pia na mikono pande zote mbili, na simba wawili+ walisimama kando ya mikono hiyo. 19  Na kulikuwa na simba 12+ waliosimama kwenye ngazi hizo sita, wawili kwenye kila ngazi, mmoja upande huu na mwingine upande wa pili. Hakuna ufalme mwingine wowote uliokuwa umetengeneza kiti kama hicho. 20  Vyombo vyote vya kunywea vya Mfalme Sulemani vilikuwa vya dhahabu, na vyombo vyote vya Nyumba ya Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu chochote kilichotengenezwa kwa fedha, kwa maana fedha ilionwa kuwa si kitu katika siku za Sulemani.+ 21  Kwa maana meli za mfalme zilikuwa zikienda Tarshishi+ na watumishi wa Hiramu.+ Mara moja baada ya kila miaka mitatu, meli za Tarshishi zilikuja zikiwa zimejazwa dhahabu na fedha, pembe za tembo,+ sokwe, na tausi. 22  Kwa hiyo Mfalme Sulemani alikuwa na utajiri mwingi zaidi na hekima kuliko wafalme wengine wote duniani.+ 23  Na wafalme wote duniani walitaka kukutana na* Sulemani ili wasikie hekima yake ambayo Mungu wa kweli alikuwa ameweka moyoni mwake.+ 24  Kila mmoja wao alileta zawadi—vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, mavazi,+ silaha, mafuta ya zeri, farasi, na nyumbu—na walifanya hivyo mwaka baada ya mwaka. 25  Na Sulemani alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi wake na magari yake ya vita na pia alikuwa na farasi* 12,000,+ naye aliwaweka katika majiji ya magari ya vita karibu naye huko Yerusalemu.+ 26  Naye aliwatawala wafalme wote kuanzia Mto Efrati mpaka nchi ya Wafilisti hadi kwenye mpaka wa Misri.+ 27  Mfalme alifanya fedha huko Yerusalemu iwe nyingi kama mawe, na mbao za mierezi ziwe nyingi kama mikuyu katika Shefela.+ 28  Nao walikuwa wakimletea Sulemani farasi kutoka Misri+ na kutoka katika nchi nyingine zote. 29  Na mambo mengine katika historia ya Sulemani,+ kuanzia mwanzo mpaka mwisho, je, hayajaandikwa katika maandishi ya nabii Nathani,+ katika unabii wa Ahiya+ Mshilo, na katika kumbukumbu ya maono ya mwonaji Ido+ kumhusu Yeroboamu+ mwana wa Nebati? 30  Sulemani alitawala nchi yote ya Israeli kwa miaka 40 akiwa Yerusalemu. 31  Kisha Sulemani akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake. Basi wakamzika katika Jiji la Daudi baba yake;+ na Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.+

Maelezo ya Chini

Au “mafumbo.”
Tnn., “lililofichwa.”
Tnn., “hakubaki na roho yoyote ndani yake.”
Au “maneno.”
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Au “jumba la.”
Au labda, “pamoja na zawadi zilizolingana na thamani ya.”
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Katika Maandiko ya Kiebrania mina moja inalingana na gramu 570. Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “waliutafuta uso wa.”
Au “wapanda farasi.”