Kitabu cha Pili cha Samweli 21:1-22

  • Nyumba ya Sauli yalipizwa kisasi kwa ajili ya Wagibeoni (1-14)

  • Vita dhidi ya Wafilisti (15-22)

21  Basi katika siku za Daudi kulikuwa na njaa kali+ kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akamwomba Yehova ushauri, kisha Yehova akasema: “Sauli na nyumba yake wana hatia ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”+  Basi mfalme akawaita Wagibeoni+ na kuongea nao. (Sasa, Wagibeoni hawakuwa Waisraeli bali walikuwa Waamori+ waliokuwa wamebaki, na Waisraeli walikuwa wameapa kwamba hawatawaua,+ lakini Sauli akichochewa na bidii yake kwa ajili ya watu wa Israeli na Yuda alitaka kuwaangamiza.)  Daudi akawauliza Wagibeoni: “Niwafanyie nini, nami nitawalipaje kwa ajili ya mliyotendewa, ili muubariki urithi wa Yehova?”  Wagibeoni wakamwambia: “Jambo ambalo Sauli na nyumba yake walitutendea si suala la fedha wala dhahabu;+ wala hatuwezi kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akasema: “Nitawafanyia jambo lolote mtakalosema.”  Wakamwambia mfalme: “Mtu aliyetuua na kupanga njama ya kutuangamiza ili tusiishi katika eneo lolote la Israeli+  tupatieni wanawe saba. Tutatundika maiti zao*+ mbele za Yehova katika jiji la Gibea+ la Sauli, aliyechaguliwa na Yehova.”+ Ndipo mfalme akasema: “Nitawapa.”  Hata hivyo, mfalme akamhurumia Mefiboshethi,+ mwana wa Yonathani mwana wa Sauli, kwa sababu ya kiapo ambacho Daudi na Yonathani mwana wa Sauli walikuwa wameapiana mbele za Yehova.+  Basi mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili ambao Rispa+ binti ya Aya alimzalia Sauli, na wana watano ambao Mikali*+ binti ya Sauli alimzalia Adrieli+ mwana wa Barzilai, Mmeholathi.  Daudi akawapa Wagibeoni wana hao, nao wakatundika maiti zao mlimani mbele za Yehova.+ Wana wote saba walikufa pamoja; waliuawa siku za kwanza za mavuno, mwanzoni mwa mavuno ya shayiri. 10  Kisha Rispa+ binti ya Aya akachukua gunia na kulitandika mwambani tangu mwanzo wa mavuno mpaka mvua kutoka mbinguni iliponyeshea maiti hizo; hakuruhusu ndege wa angani watue juu ya maiti hizo wakati wa mchana wala wanyama wa mwituni wazikaribie wakati wa usiku. 11  Daudi akaambiwa mambo ambayo Rispa binti ya Aya suria wa Sauli alikuwa amefanya. 12  Kwa hiyo Daudi akaenda na kuchukua mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwana wake kutoka kwa viongozi* wa Yabesh-gileadi,+ waliokuwa wameiba mifupa hiyo katika uwanja wa jiji la Beth-shani, ambako Wafilisti walikuwa wamewatundika siku ambayo walimuua Sauli juu ya Gilboa.+ 13  Akachukua mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwana wake kutoka mlimani, pia wakaikusanya mifupa ya wanaume waliokuwa wameuawa.*+ 14  Kisha wakaizika mifupa ya Sauli na Yonathani mwana wake katika nchi ya Benjamini kule Sela+ katika kaburi la Kishi+ baba yake. Baada ya kufanya kila jambo ambalo mfalme alikuwa ameamuru, Mungu akasikiliza maombi yao ya kumsihi kuhusu nchi.+ 15  Vita vikatokea tena kati ya Wafilisti na Waisraeli.+ Kwa hiyo, Daudi na watumishi wake wakashuka kwenda kupigana na Wafilisti, lakini Daudi akachoka. 16  Mzao wa Warefaimu+ aliyeitwa Ishbi-benobu, aliyekuwa na mkuki wa shaba wenye uzito wa shekeli 300*+ na aliyejihami kwa upanga mpya, alikusudia kumuua Daudi. 17  Mara moja Abishai+ mwana wa Seruya akaja kumsaidia,+ akampiga Mfilisti huyo na kumuua. Wakati huo wanaume wa Daudi wakamwapia hivi: “Usiende tena vitani pamoja nasi!+ Usiizime taa ya Israeli!”+ 18  Baada ya hayo, wakapigana tena na Wafilisti+ kule Gobu. Wakati huo Sibekai+ Mhusha alimuua Safu, aliyekuwa mzao wa Warefaimu.+ 19  Wakapigana tena na Wafilisti+ huko Gobu, na Elhanani mwana wa Yaare-oregimu Mbethlehemu akamuua Goliathi Mgathi, aliyekuwa na mkuki wenye mpini kama mti wa wafumaji wa nguo.+ 20  Vita vikatokea tena huko Gathi, ambako kulikuwa na mwanamume mkubwa isivyo kawaida, mwenye vidole 6 katika kila mkono na vidole 6 katika kila mguu, jumla ya vidole 24; naye pia alikuwa mzao wa Warefaimu.+ 21  Aliendelea kuwadhihaki Waisraeli.+ Basi Yonathani mwana wa Shimei,+ ndugu ya Daudi, akamuua. 22  Watu hao wanne walikuwa wazao wa Warefaimu huko Gathi, na Daudi na watumishi wake ndio waliowaua.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “tutawaanika,” yaani, mikono na miguu yao ikiwa imevunjwa.
Au labda, “Merabu.”
Au labda, “wamiliki wa mashamba.”
Tnn., “wameanikwa.”
Karibu kilogramu 3.42. Angalia Nyongeza B14.