Kitabu cha Pili cha Samweli 22:1-51

  • Daudi amsifu Mungu kwa sababu ya matendo yake ya wokovu (1-51)

    • “Yehova ni jabali langu” (2)

    • Yehova ni mshikamanifu kwa walio washikamanifu (26)

22  Daudi akamwimbia Yehova maneno ya wimbo huu+ siku ambayo Yehova alimwokoa kutoka mikononi mwa maadui wake wote+ na kutoka mikononi mwa Sauli.+  Akasema: “Yehova ni jabali langu na ngome yangu+ na Mwokozi wangu.+   Mungu wangu ni mwamba wangu,+ ninayemkimbilia,Ngao yangu+ na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama*+Na mahali pangu pa kukimbilia,+ mwokozi wangu;+ wewe unayeniokoa kutoka katika ukatili.   Ninamlilia Yehova, anayestahili kusifiwa,Nami nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.   Mawimbi ya kifo yalinizunguka pande zote;+Mafuriko ya ghafla ya wanaume wasiofaa kitu yaliniogopesha.+   Kamba za Kaburi* zilinizunguka;+Mitego ya kifo ilinikabili.+   Katika taabu yangu nilimwita Yehova,+Niliendelea kumlilia Mungu wangu. Kisha akiwa katika hekalu lake akaisikia sauti yangu,Na kilio changu cha kuomba msaada kilifika masikioni mwake.+   Dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika huku na huku;+Misingi ya mbingu ikasukasuka+Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+   Moshi ulipanda kutoka katika mianzi ya pua yake,Na moto unaoteketeza kabisa ukatoka kinywani mwake;+Makaa ya mawe yanayowaka moto mkali yakatoka kwake. 10  Alizifanya mbingu zijikunje alipokuwa akishuka,+Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.+ 11  Alipanda juu ya kerubi,+ akaja akiruka. Alionekana juu ya mabawa ya kiumbe wa roho.*+ 12  Kisha akaweka giza kumzunguka kama kibanda,+Katika maji yenye giza na mawingu mazito. 13  Kutoka katika mwangaza ulio mbele zake makaa ya mawe yenye moto mkali yaliwaka. 14  Kisha Yehova akaanza kunguruma kutoka mbinguni;+Aliye Juu Zaidi aliifanya sauti yake isikike.+ 15  Alipiga mishale yake+ akawatawanya;Radi, akawavuruga.+ 16  Sakafu ya bahari ikaonekana;+Misingi ya nchi ikafunuliwa kwa kemeo la Yehova,Kwa mlipuko wa pumzi kutoka katika mianzi ya pua yake.+ 17  Aliunyoosha mkono wake kutoka juu;Akanishika na kunivuta kutoka katika maji yenye kina.+ 18  Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+Kutoka kwa wale wanaonichukia, waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi. 19  Walinikabili katika siku ya msiba wangu,+Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu. 20  Alinitoa nje na kunileta mahali penye usalama;*+Aliniokoa kwa sababu alipendezwa nami.+ 21  Yehova hunithawabisha kulingana na uadilifu wangu;+Hunilipa kulingana na usafi wa* mikono yangu.+ 22  Kwa maana nimezishika njia za Yehova,Nami sijamwacha kwa uovu Mungu wangu. 23  Hukumu zake zote+ ziko mbele yangu;Sitageuka kando kutoka kwenye sheria zake.+ 24  Nitabaki bila lawama+ mbele zake,Nami nitajiepusha na uovu.+ 25  Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+Kulingana na usafi wangu* mbele zake.+ 26  Kwa mtu mshikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+Kwa mtu asiye na lawama, mtu hodari, unatenda bila lawama;+ 27  Kwa walio safi unajidhihirisha mwenyewe kuwa safi,+Lakini kwa waliopotoka unajidhihirisha mwenyewe kuwa mwenye busara.*+ 28  Kwa maana wewe huwaokoa walio wanyenyekevu,+Lakini macho yako hayapendezwi na wenye kiburi, nawe huwashusha.+ 29  Kwa maana wewe ni taa yangu, Ee Yehova;+Yehova ndiye anayefanya giza langu liangaze.+ 30  Kwa msaada wako ninaweza kukabiliana na kundi la wavamizi;Kwa nguvu za Mungu ninaweza kuupanda ukuta.+ 31  Njia ya Mungu wa kweli ni kamilifu;+Neno la Yehova ni safi.+ Yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia.+ 32  Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+ Na ni nani aliye mwamba isipokuwa Mungu wetu?+ 33  Mungu wa kweli ni ngome yangu imara,+Naye ataifanya njia yangu iwe kamilifu.+ 34  Huifanya miguu yangu iwe kama ya paa;Hunifanya nisimame mahali palipo juu.+ 35  Huizoeza mikono yangu kupigana vita;Mikono yangu inaweza kuukunja upinde wa shaba. 36  Wewe hunipa ngao yako ya wokovu,Na unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu.+ 37  Unapanua njia kwa ajili ya hatua zangu;Miguu yangu haitateleza.*+ 38  Nitawafuatia maadui wangu na kuwaangamiza;Sitarudi mpaka watakapoangamizwa kabisa. 39  Nami nitawaangamiza kabisa na kuwaponda, hivi kwamba hawatainuka;+Wataanguka chini ya miguu yangu. 40  Utanipa nguvu kwa ajili ya vita;+Utawafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+ 41  Utawafanya maadui wangu wanikimbie;*+Nitawakomesha* wale wanaonichukia.+ 42  Wanalilia msaada, lakinihakuna mtu wa kuwaokoa;Hata wanamlilia Yehova, lakini yeye hawajibu.+ 43  Nitawaponda wawe laini kama mavumbi ya dunia;Nitawapondaponda na kuwakanyaga-kanyaga kama matope barabarani. 44  Utaniokoa kutoka kwa watu wangu ambao hutafuta makosa.+ Utanilinda niwe kiongozi wa mataifa;+Watu ambao siwajui watanitumikia.+ 45  Wageni watakuja wakijikunyata mbele zangu;+Watanitii kwa sababu ya mambo watakayosikia kunihusu.* 46  Wageni watakosa ujasiri;*Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao. 47  Yehova yuko hai! Mwamba wangu na asifiwe!+ Mungu wa mwamba wa wokovu wangu na akwezwe.+ 48  Mungu wa kweli hunilipizia kisasi;+Huyatiisha mataifa chini yangu;+ 49  Yeye huniokoa kutoka kwa maadui wangu. Unaniinua juu+ ya wale wanaonishambulia;Unaniokoa kutoka kwa mtu mkatili.+ 50  Ndiyo sababu nitakushukuru wewe, Ee Yehova, miongoni mwa mataifa,+Nami nitaliimbia sifa* jina lako:+ 51  Yeye hutenda matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake;*+Humtendea mtiwa-mafuta wake kwa upendo mshikamanifu,Kwa Daudi na kwa uzao wake* milele.”+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “mwokozi wangu mwenye nguvu.”
Au “kilele changu salama.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “ya upepo.”
Au “mahali penye nafasi kubwa.”
Au “ukosefu wa hatia wa.”
Au “ukosefu wangu wa hatia.”
Au labda, “unatenda kama mpumbavu.”
Au “Vifundo vya miguu yangu havitateleza.”
Au “Utanionyesha migongo ya maadui wangu.”
Au “Nitawanyamazisha.”
Tnn., “Mara tu sikio lao linaposikia, watanitii.”
Au “watafifia.”
Au “nitalipigia muziki.”
Au “humpa ushindi mkubwa mfalme wake.”
Tnn., “mbegu yake.”