Kitabu cha Pili cha Samweli 23:1-39

  • Maneno ya mwisho ya Daudi (1-7)

  • Mambo yaliyotendwa na mashujaa hodari wa Daudi (8-39)

23  Haya ndiyo maneno ya mwisho ya Daudi:+ “Neno la Daudi mwana wa Yese,+Na neno la mwanamume aliyeinuliwa juu,+Mtiwa-mafuta+ wa Mungu wa Yakobo,Mwimbaji anayependeza* wa nyimbo+ za Israeli.   Roho ya Yehova ilisema kupitia mimi;+Neno lake lilikuwa kwenye ulimi wangu.+   Mungu wa Israeli alisema;Mwamba wa Israeli+ aliniambia: ‘Yule anayetawala wanadamu anapokuwa mwadilifu,+Anapotawala kwa kumwogopa Mungu,+   Ni kama mwangaza wa asubuhi jua linapoangaza,+Asubuhi isiyo na mawingu. Ni kama mwangaza baada ya mvua kunyesha,Ambao unaotesha majani duniani.’+   Je, sivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Kwa maana amefanya pamoja nami agano la milele,+Lililopangwa kwa utaratibu katika kila jambo na kuhakikishwa. Kwa sababu linamaanisha wokovu wangu wote na furaha yangu yote,Je, yeye halifanyi lisitawi kwa sababu hiyo?+   Lakini watu wasiofaa kitu hutupwa+ wote kama vichaka vya miiba,Kwa maana hawawezi kuchukuliwa kwa mkono.   Mtu anapowagusa,Anapaswa kujihami kikamili kwa chuma na mpini wa mkuki,Nao wanapaswa kuteketezwa kabisa kwa moto mahali walipo.”  Haya ndiyo majina ya mashujaa hodari wa Daudi:+ Yosheb-bashebethi Mtakemoni, kiongozi wa wale watatu.+ Wakati mmoja, alitumia mkuki wake kuwaua watu 800.  Aliyemfuata ni Eleazari+ mwana wa Dodo+ mwana wa Ahohi, naye alikuwa miongoni mwa mashujaa hao watatu hodari waliokuwa na Daudi walipowadhihaki Wafilisti. Walikuwa wamekusanyika huko kwa ajili ya vita, na wanaume wa Israeli walipokimbia, 10  alisimama imara na kuendelea kuwaua Wafilisti mpaka mkono wake ulipochoka na kuganda kwa sababu ya kuushika upanga.+ Basi Yehova akawapa ushindi* mkubwa siku hiyo;+ na watu wakamfuata Eleazari ili kuchukua nyara za watu waliouawa. 11  Aliyemfuata ni Shamma mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walikusanyika kule Lehi, mahali ambapo palikuwa na shamba lililojaa dengu; na watu wakakimbia kwa sababu ya Wafilisti. 12  Lakini alisimama katikati ya shamba hilo na kuwazuia Wafilisti wasiingie humo, naye aliendelea kuwaua Wafilisti, hivi kwamba Yehova akawapa ushindi* mkubwa.+ 13  Viongozi watatu kati ya wale viongozi 30 walishuka wakati wa mavuno kwenda kwa Daudi katika pango la Adulamu,+ na kikosi* cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la* Refaimu.+ 14  Wakati huo Daudi alikuwa ndani ya ngome,+ na kituo cha ulinzi cha Wafilisti kilikuwa Bethlehemu. 15  Kisha Daudi akasema alichotamani: “Laiti ningekunywa maji kutoka katika tangi lililo karibu na lango la Bethlehemu!” 16  Ndipo wale mashujaa watatu hodari wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti, wakateka maji kutoka katika tangi hilo lililo karibu na lango la Bethlehemu na kumletea Daudi; lakini akakataa kuyanywa, akayamwaga mbele za Yehova.+ 17  Akasema: “Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia, Ee Yehova, kufanya hivyo! Je, ninywe damu+ ya wanaume walioenda kuhatarisha uhai wao?”* Basi akakataa kuyanywa. Hayo ndiyo mambo waliyotenda mashujaa wake watatu hodari. 18  Abishai+ ndugu ya Yoabu mwana wa Seruya+ alikuwa kiongozi wa wengine watatu; alitumia mkuki wake kuwaua watu 300, naye alikuwa maarufu kama wale watatu.+ 19  Ingawa alikuwa mashuhuri zaidi kuliko wale wengine watatu na alikuwa kiongozi wao, hakuwa shujaa kama wale watatu wa kwanza. 20  Benaya+ mwana wa Yehoyada alikuwa mwanamume jasiri* aliyefanya mambo mengi ya kishujaa kule Kabzeeli.+ Aliwaua wana wawili wa Arieli wa Moabu, naye aliingia ndani ya shimo la maji siku ya theluji na kumuua simba.+ 21  Alimuua pia mwanamume Mmisri aliyekuwa mkubwa isivyo kawaida. Ingawa Mmisri huyo alikuwa na mkuki mkononi, Benaya alikabiliana naye akiwa na fimbo, akamnyang’anya Mmisri huyo mkuki kutoka mkononi mwake na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe. 22  Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, naye alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu hodari. 23  Ingawa alikuwa mashuhuri hata kuliko wale 30, hakuwa shujaa kama wale watatu. Lakini Daudi alimweka kuwa kiongozi wa walinzi wake binafsi. 24  Asaheli+ ndugu ya Yoabu alikuwa miongoni mwa wale 30: Elhanani mwana wa Dodo wa Bethlehemu,+ 25  Shamma Mharodi, Elika Mharodi, 26  Helezi+ Mpeleti, Ira+ mwana wa Ikeshi Mtekoa, 27  Abiezeri+ Mwanathothi,+ Mebunai Mhusha, 28  Salmoni Mwahohi, Maharai+ Mnetofa, 29  Helebu mwana wa Baana Mnetofa, Itai mwana wa Ribai wa jiji la Gibea la Wabenjamini, 30  Benaya+ Mpirathoni, Hidai kutoka katika makorongo* ya Gaashi,+ 31  Abi-alboni Mwarbathi, Azmavethi Mbarhumu, 32  Eliaba Mshaalboni, wana wa Yasheni, Yonathani,⁠ 33  Shamma Mharari, Ahiamu, mwana wa Sharari Mharari, 34  Elifeleti mwana wa Ahasbai mwana wa yule Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli+ Mgiloni, 35  Hezro Mkarmeli, Paarai Mwarabi, 36  Igali mwana wa Nathani wa Soba, Bani Mgadi, 37  Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, aliyembebea silaha Yoabu mwana wa Seruya, 38  Ira Mwithri, Garebu Mwithri,+ 39  na Uria+ Mhiti—wote walikuwa 37.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Yule anayependeza.”
Au “wokovu.”
Au “wokovu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Au “kijiji cha mahema.”
Au “nafsi zao.”
Tnn., “mwana wa mwanamume jasiri.”
Angalia Kamusi.