Kitabu cha Pili cha Samweli 7:1-29

  • Daudi hatajenga hekalu (1-7)

  • Agano pamoja na Daudi kwa ajili ya ufalme (8-17)

  • Sala ya Daudi ya shukrani (18-29)

7  Mfalme alipoanza kuishi katika nyumba yake mwenyewe*+ na baada ya Yehova kumpumzisha kutokana na maadui wake wote waliomzunguka,  mfalme alimwambia hivi nabii Nathani:+ “Mimi hapa ninaishi katika nyumba ya mierezi+ huku Sanduku la Mungu wa kweli likikaa katikati ya vitambaa vya mahema.”+  Nathani akamwambia mfalme: “Nenda ufanye jambo lolote lililo moyoni mwako, kwa sababu Yehova yuko pamoja nawe.”+  Usiku huohuo, neno hili la Yehova likamjia Nathani:  “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Je, utanijengea nyumba nikae ndani yake?+  Kwa maana sijakaa ndani ya nyumba tangu siku nilipowatoa watu wa Israeli huko Misri mpaka leo,+ bali nimekuwa nikihama* huku na kule katika hema na katika hema la ibada.+  Wakati wote nilipotembea na Waisraeli wote,* je, niliwahi wakati wowote kumuuliza kiongozi yeyote wa kabila la Israeli niliyemweka awachunge watu wangu Waisraeli, ‘Kwa nini hukunijengea nyumba ya mierezi?’”’  Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo,+ uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+  Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapoenda,+ nami nitawaangamiza maadui wako wote kutoka mbele yako;+ nami nitafanya jina lako liwe maarufu+ kama jina la watu maarufu duniani. 10  Nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Waisraeli na kuwaweka humo, nao wataishi humo na hawatasumbuliwa tena; na watu waovu hawatawakandamiza tena kama walivyofanya zamani,+ 11  tangu siku nilipowaweka waamuzi+ juu ya watu wangu Waisraeli. Nami nitakupumzisha kutokana na maadui wako wote.+ “‘“Pia, Yehova amekuambia kwamba Yehova atakujengea nyumba.*+ 12  Siku zako zitakapokwisha+ nawe ufe na kuzikwa pamoja na mababu zako, ndipo nitakapomwinua mzao wako* baada yako, mwana wako mwenyewe,* nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+ 13  Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ nami nitakiimarisha kabisa kiti cha ufalme wake milele.+ 14  Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu.+ Atakapokosea, nitamkaripia kwa fimbo ya wanadamu na kwa viboko vya wana wa binadamu.*+ 15  Upendo wangu mshikamanifu hautaondolewa kwake kama nilivyouondoa kwa Sauli,+ niliyemwondoa kutoka mbele yako. 16  Nyumba yako na ufalme wako utakuwa salama milele mbele yako; kiti chako cha ufalme kitaimarishwa kabisa milele.”’”+ 17  Nathani akamwambia Daudi maneno hayo yote na maono hayo yote.+ 18  Ndipo Mfalme Daudi akaingia na kuketi mbele za Yehova na kusema: “Mimi ni nani, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova? Na nyumba yangu ni nini hivi kwamba umenileta mpaka hapa nilipofika?+ 19  Na kana kwamba hilo halitoshi, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, unasema pia kwamba nyumba yangu mimi mtumishi wako itadumu kwa muda mrefu; na haya ni maagizo* kwa wanadamu wote, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 20  Mimi mtumishi wako Daudi nitakwambia nini zaidi wakati unanijua vizuri sana,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova? 21  Kwa ajili ya neno lako na kupatana na moyo wako* umetenda mambo haya yote makuu na kunifunulia mimi mtumishi wako.+ 22  Ndiyo sababu wewe kwa kweli ni mkuu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. Hakuna aliye kama wewe,+ na hakuna Mungu ila wewe;+ mambo yote tuliyosikia kwa masikio yetu yanathibitisha jambo hilo. 23  Na kuna taifa gani lingine duniani lililo kama watu wako Waisraeli?+ Wewe Mungu ulienda na kuwakomboa wakiwa watu wako,+ ukajijengea jina+ kwa kufanya mambo makuu na yenye kuogopesha kwa ajili yao.+ Uliyafukuza mataifa na miungu yao kwa ajili ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri kwa ajili yako mwenyewe. 24  Uliwaimarisha watu wako Waisraeli ili wawe watu wako milele;+ na wewe, Ee Yehova, umekuwa Mungu wao.+ 25  “Sasa, Ee Yehova Mungu, timiza ahadi uliyotoa kunihusu mimi mtumishi wako na nyumba yangu milele, na ufanye kama ulivyoahidi.+ 26  Jina lako na likwezwe milele,+ ili watu waseme, ‘Yehova wa majeshi ni Mungu wa Israeli,’ na nyumba yangu mimi mtumishi wako Daudi na iimarishwe kabisa mbele zako.+ 27  Kwa maana wewe, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, umenifunulia mimi mtumishi wako ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’*+ Ndiyo sababu mimi mtumishi wako nina ujasiri wa* kutoa sala hii kwako. 28  Na sasa, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, wewe ndiye Mungu wa kweli, na maneno yako ni kweli,+ nawe umeniahidi mimi mtumishi wako mambo hayo mema. 29  Basi na ufurahie kuibariki nyumba yangu mimi mtumishi wako, na idumu milele mbele zako;+ kwa sababu wewe, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, umeahidi, na kwa baraka yako, nyumba yangu mimi mtumishi wako na ibarikiwe milele.”+

Maelezo ya Chini

Au “jumba lake mwenyewe la mfalme.”
Tnn., “nikitembea.”
Tnn., “wana wote wa Israeli.”
Au “ukoo wa kifalme.”
Tnn., “mbegu yako.”
Tnn., “yule atakayetoka katika viungo vyako vya ndani.”
Au labda, “Adamu.”
Au “na hii ni sheria.”
Au “kulingana na mapenzi yako.”
Au “ukoo wa kifalme.”
Tnn., “nimepata moyo wa.”