Barua ya Pili kwa Timotheo 2:1-26

  • Wakabidhi ujumbe wanaume wanaostahili (1-7)

  • Kuvumilia mateso kwa ajili ya habari njema (8-13)

  • Litumie sawasawa neno la Mungu (14-19)

  • Zikimbie tamaa za ujana (20-22)

  • Jinsi ya kushughulika na wapinzani (23-26)

2  Kwa hiyo, wewe mwanangu,+ endelea kujipatia nguvu katika fadhili zisizostahiliwa zilizo katika Kristo Yesu;  na mambo uliyoyasikia kutoka kwangu yaliyothibitishwa na mashahidi wengi,+ mambo hayo uwakabidhi wanaume waaminifu, ambao watastahili vya kutosha kuwafundisha wengine.  Ukiwa mwanajeshi mwema+ wa Kristo Yesu, shiriki katika kuvumilia dhiki.+  Mtu anayetumikia akiwa mwanajeshi hajihusishi* katika shughuli za kibiashara* za maisha, ili apate kibali cha yule aliyemwandikisha kuwa mwanajeshi.  Hata katika michezo, yeyote anayeshindana havikwi taji asiposhindana kulingana na sheria.+  Mkulima anayefanya kazi kwa bidii lazima awe wa kwanza kula matunda.  Fikiria daima mambo ninayosema; Bwana atakupatia uelewaji* katika mambo yote.  Kumbuka kwamba Yesu Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu+ na alikuwa uzao wa Daudi,*+ kulingana na habari njema ninayohubiri,+  ambayo kwa ajili yake ninavumilia na kufungwa gerezani kama mhalifu.+ Hata hivyo, neno la Mungu halifungwi.+ 10  Kwa sababu hiyo ninaendelea kuvumilia mambo yote kwa ajili ya wale waliochaguliwa,+ ili wao pia wapate wokovu ambao ni kupitia Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. 11  Maneno haya yanategemeka: Hakika ikiwa tulikufa pamoja, tutaishi pamoja pia;+ 12  tukiendelea kuvumilia, tutatawala pamoja pia tukiwa wafalme;+ tukimkana, naye pia atatukana sisi;+ 13  tukikosa kuwa waaminifu, yeye anabaki kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe. 14  Endelea kuwakumbusha mambo haya, ukiwaagiza* mbele za Mungu wasipigane kuhusu maneno, jambo hilo halina faida kabisa kwa sababu linawadhuru* wale wanaosikiliza. 15  Fanya yote unayoweza ili ujitoe kwa Mungu ukiwa mtu aliyekubaliwa, mfanyakazi asiye na lolote la kuonea aibu, ukilitumia sawasawa neno la kweli.+ 16  Lakini kataa maneno matupu ambayo huchafua mambo matakatifu,+ kwa maana yataongoza kwenye kutomwogopa Mungu zaidi na zaidi, 17  na neno lao litaenea kama kidonda kinachooza. Himenayo na Fileto ni kati yao.+ 18  Watu hao wamegeuka kutoka kwenye kweli, wakisema kwamba tayari ufufuo umetukia,+ nao wanapindua imani ya wengine. 19  Ingawa hivyo, msingi imara wa Mungu unakaa ukiwa umesimama, ukiwa na muhuri huu: “Yehova* anawajua walio wake,”+ na “Kila mtu anayeliitia jina la Yehova*+ na aukatae ukosefu wa uadilifu.” 20  Basi ndani ya nyumba kubwa kuna vyombo vya dhahabu na fedha, na pia kuna vyombo vya miti na vya udongo, na vingine ni vya matumizi yanayoheshimika lakini vingine ni vya matumizi yasiyoheshimika. 21  Kwa hiyo, yeyote akijiepusha na hivyo vya mwisho, atakuwa kifaa* cha matumizi yanayoheshimika, kilichotakaswa, chenye faida kwa bwana wake, kilichotayarishwa kwa ajili ya kila kazi njema. 22  Basi zikimbie tamaa za ujana, lakini fuatilia uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na wale wanaomwitia Bwana kwa moyo safi. 23  Isitoshe, kataa mabishano ya kipumbavu na ya kijinga,+ ukijua kwamba hayo hutokeza mapigano. 24  Kwa maana mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali anahitaji kuwa mpole* kwa wote,+ mwenye uwezo wa kufundisha, anayejizuia anapokosewa,+ 25  akiwafundisha kwa upole wale wasio na mwelekeo unaofaa.+ Huenda Mungu akawasaidia kutubu* na kupata ujuzi sahihi wa kweli,+ 26  nao warudiwe na fahamu na kutoka kwenye mtego wa Ibilisi, kwa kuwa amewanasa wakiwa hai ili wafanye mapenzi yake.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “hajifungi.”
Au labda, “shughuli za kila siku.”
Au “utambuzi.”
Tnn., “wa mbegu ya Daudi.”
Tnn., “ukiwatolea ushahidi kamili.”
Au “linawaharibu; linawavuruga.”
Au “chombo.”
Au “mwenye busara.”
Au “kubadili mawazo.”