Barua ya Pili kwa Wakorintho 10:1-18

  • Paulo aitetea huduma yake (1-18)

    • Silaha zetu si za kimwili (4, 5)

10  Basi mimi mwenyewe, Paulo, ninawasihi kwa upole na fadhili za Kristo,+ ingawa mimi ni wa hali ya chini ninapokuwa kati yenu uso kwa uso,+ lakini jasiri kuwaelekea ninyi nisipokuwapo.+  Ninaomba kwamba nitakapokuwapo, nisilazimike kuwa jasiri na kuchukua hatua kali ambazo ninakusudia dhidi ya wale wanaotuona kana kwamba tulitembea kwa njia ya kimwili.  Kwa maana ingawa tunatembea katika mwili, hatupigani vita kulingana na vile tulivyo katika mwili.  Kwa maana silaha za vita vyetu si za kimwili,+ bali ni zenye nguvu kupitia Mungu+ kwa ajili ya kuzipindua ngome zenye nguvu.  Kwa maana tunapindua mawazo na kila jambo lililo juu sana ambalo limeinuliwa kinyume cha ujuzi wa Mungu,+ nasi tunaiteka kila fikira ili kuifanya imtii Kristo;  nasi tuko tayari kutoa adhabu kwa ajili ya kila tendo la kutotii,+ mara tu utii wenu utakapokamilika.  Mnayatazama mambo kulingana na thamani yake ya nje. Mtu yeyote akijiamini kwamba yeye ni wa Kristo, acheni afikirie tena jambo hili: Kama vile yeye alivyo wa Kristo, ndivyo na sisi pia.  Kwa maana hata nikijisifu sana kuhusu mamlaka ambayo Bwana alitupatia ili tuwajenge wala si kuwabomoa ninyi,+ mimi sitaaibishwa.  Kwa maana sitaki ionekane kama ninajaribu kuwatisha kwa barua zangu. 10  Kwa maana wanasema: “Barua zake ni nzito na zenye nguvu, lakini akiwapo yeye mwenyewe, ni dhaifu na maneno yake ni yenye kudharaulika.” 11  Mtu kama huyo ajue kwamba mambo tunayosema* kupitia barua tusipokuwapo, tutayafanya pia* tutakapokuwapo.+ 12  Kwa maana sisi hatuthubutu kujiweka katika kikundi au kujilinganisha na watu fulani wanaojipendekeza wenyewe.+ Lakini wanapojipima wenyewe kwa wenyewe na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, hawana uelewaji.+ 13  Hata hivyo, hatutajisifu nje ya mipaka tuliyogawiwa, bali katika mpaka wa eneo ambalo Mungu alitupimia,* na kuufanya ufike hadi kwenu.+ 14  Kwa kweli, sisi hatuvuki mpaka wetu kana kwamba hatukuwafikia ninyi, kwa maana tulikuwa wa kwanza kufika hadi kwenu tukiwa na habari njema kuhusu Kristo.+ 15  Hapana, hatujisifu kuhusu kazi za mtu mwingine nje ya mipaka tuliyogawiwa, bali tunatumaini kwamba imani yenu inapozidi kuongezeka, mambo tuliyofanya yatazidi kuongezeka katika eneo letu. Ndipo tutazidi hata zaidi, 16  ili tutangaze habari njema katika nchi zilizo ng’ambo yenu, na hivyo tusijisifu kuhusu mambo ambayo tayari yamefanywa katika eneo la mtu mwingine. 17  “Lakini yule anayejisifu, na ajisifu katika Yehova.”*+ 18  Kwa maana si yule anayejipendekeza ambaye hukubaliwa,+ bali ni yule ambaye Yehova* humpendekeza.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “tutakuwa hivyo pia katika matendo.”
Tnn., “jinsi tulivyo katika maneno.”
Au “alitugawia kwa kipimo.”