Barua ya Pili kwa Wakorintho 3:1-18

  • Barua za mapendekezo (1-3)

  • Wahudumu wa agano jipya (4-6)

  • Utukufu ulio bora wa agano jipya (7-18)

3  Je, tunaanza tena kujipendekeza wenyewe? Au kama watu fulani, je, tunahitaji barua za pendekezo kuja au kutoka kwenu?  Ninyi wenyewe ndio barua yetu,+ iliyoandikwa juu ya mioyo yetu na kujulikana na kusomwa na wanadamu wote.  Kwa maana ni wazi kwamba ninyi ni barua ya Kristo ambayo tuliandika tukiwa wahudumu,+ iliyoandikwa si kwa wino bali kwa roho ya Mungu aliye hai, si juu ya mabamba ya mawe,+ bali juu ya mabamba ya nyama, juu ya mioyo.+  Tuna uhakika wa namna hii kwa Mungu kupitia Kristo.  Si kwamba sisi wenyewe tunastahili vya kutosha kufikiri kuwa jambo lolote linatoka kwetu, bali kustahili kwetu vya kutosha hutoka kwa Mungu,+  ambaye kwa kweli ametustahilisha vya kutosha kuwa wahudumu wa agano jipya,+ si wa sheria zilizoandikwa,+ bali wa roho; kwa maana sheria zilizoandikwa huleta hukumu ya kifo,+ bali roho hufanya kuwa hai.+  Basi ikiwa sheria zinazotoa kifo ambazo zilichongwa kwa herufi kwenye mawe+ zilikuja kwa utukufu kama huo hivi kwamba wana wa Israeli hawakuweza kuutazama uso wa Musa kwa sababu ya utukufu wa uso wake,+ utukufu ambao ungekuja kuondolewa,  kwa nini kutolewa kwa roho+ kusiwe kwenye utukufu zaidi?+  Kwa maana ikiwa sheria zilizotoa hukumu ya hatia+ zilikuwa zenye utukufu,+ kutolewa kwa uadilifu kungekuwa na utukufu mwingi kadiri gani!+ 10  Kwa kweli, hata kile ambacho wakati fulani kilifanywa kiwe na utukufu kimevuliwa utukufu, kwa sababu ya utukufu unaokizidi.+ 11  Kwa maana ikiwa kile ambacho kingeondolewa kiliingizwa kwa utukufu,+ basi utukufu wa kinachobaki ungekuwa mwingi kadiri gani!+ 12  Kwa kuwa tuna tumaini hilo,+ tunazungumza kwa uhuru mwingi, 13  nasi hatufanyi kama Musa alivyofanya alipofunika uso wake kwa kitambaa+ ili wana wa Israeli wasitazame mwisho wa kile ambacho kingeondolewa. 14  Lakini akili zao zilitiwa uzito.+ Kwa maana mpaka leo kitambaa kilekile kinadumu bila kuondolewa agano la zamani linaposomwa,+ kwa sababu kinaondolewa tu kupitia Kristo.+ 15  Kwa kweli, mpaka leo kila mara maandishi ya Musa yanaposomwa,+ kitambaa hukaa juu ya mioyo yao.+ 16  Lakini mtu anapomgeukia Yehova,* kitambaa huondolewa.+ 17  Basi Yehova* ni Roho,+ na mahali palipo na roho ya Yehova,* pana uhuru.+ 18  Na sisi sote, tunapotoa kama vioo mrudisho wa utukufu wa Yehova* tukiwa na nyuso zisizo na kitambaa, tunageuzwa kuwa katika mfano uleule kutoka kiwango kimoja cha utukufu mpaka kingine,* sawa na anavyofanya Yehova* ambaye ni Roho.*+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kutoka utukufu mpaka utukufu.”
Au labda, “kupitia roho ya Yehova.”