Barua ya Pili kwa Wakorintho 7:1-16

  • Tujisafishe unajisi (1)

  • Shangwe ya Paulo kuhusu Wakorintho (2-4)

  • Tito aleta habari nzuri (5-7)

  • Huzuni ya kimungu na toba (8-16)

7  Kwa hiyo, wapendwa, kwa kuwa tuna ahadi hizi,+ acheni tujisafishe kila unajisi wa mwili na roho,+ tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.  Tupatieni nafasi mioyoni mwenu.+ Hatujamkosea yeyote, hatujamharibu yeyote, hatujamdanganya yeyote ili tupate faida.+  Sisemi jambo hili ili niwahukumu. Kwa maana tayari nimesema kwamba ninyi mko ndani ya mioyo yetu ili kufa pamoja na kuishi pamoja.  Nina uhuru mwingi wa kusema kuwaelekea ninyi. Ninajisifu sana kuhusiana nanyi. Nimejawa na faraja; ninafurika shangwe katika taabu yetu yote.+  Kwa kweli, tulipofika Makedonia,+ miili yetu haikupata kitulizo, bali tuliendelea kutaabishwa katika kila njia—nje kulikuwa na mapigano na ndani woga.  Lakini Mungu, ambaye huwafariji wale waliovunjika moyo,+ alitufariji kwa kuwapo kwa Tito;  na si kwa kuwapo kwake tu bali pia kwa faraja ambayo alipokea kwa sababu yenu, kwa kuwa alirudi na kutujulisha kuhusu tamaa yenu ya kuniona, huzuni yenu nyingi, na jinsi mlivyonihangaikia sana;* hivyo nikashangilia hata zaidi.  Kwa maana hata kama niliwahuzunisha kwa barua yangu,+ sijuti kuhusu jambo hilo. Ingawa mwanzoni nilijuta (nilipoona kwamba barua hiyo iliwahuzunisha, ingawa ni kwa muda mfupi tu),  sasa ninashangilia, si kwa sababu mlihuzunishwa tu, bali kwa sababu mlihuzunishwa hivi kwamba mkatubu. Kwa maana mlihuzunishwa kwa njia ya kimungu, kwa hiyo hamkupata madhara kwa sababu yetu. 10  Kwa kuwa huzuni kwa njia ya kimungu hutokeza toba inayoongoza kwenye wokovu, bila kuleta majuto;+ lakini huzuni ya ulimwengu hutokeza kifo. 11  Kwa maana, ona jinsi kuhuzunishwa kwenu kwa njia ya kimungu kulivyotokeza bidii nyingi ndani yenu, ndiyo, mlijiondolea hatia, ndiyo, ghadhabu, ndiyo, woga, ndiyo, kutamani sana,* ndiyo, bidii, ndiyo, kurekebisha kosa!+ Katika kila njia mlijionyesha kuwa safi* kuhusu jambo hili. 12  Ingawa niliwaandikia, sikufanya hivyo kwa ajili ya yule aliyefanya kosa,+ wala kwa ajili ya yule aliyekosewa, bali ili bidii yenu kwa ajili yetu ithibitishwe miongoni mwenu machoni pa Mungu. 13  Ndiyo sababu tumefarijiwa. Lakini kwa kuongezea faraja yetu, tulishangilia hata zaidi kuhusu shangwe ya Tito, kwa sababu ninyi nyote mliiburudisha roho yake. 14  Kwa maana ikiwa nimejisifu kwake juu yenu, sijapata aibu; lakini kama vile mambo tuliyowaambia yalivyokuwa ya kweli, ndivyo pia kujisifu kwetu kwa Tito kumekuwa kweli. 15  Pia, upendo wake mwororo kwenu ni mwingi anapokumbuka utii wenu nyote,+ jinsi mlivyompokea kwa kuogopa na kutetemeka. 16  Ninashangilia kwamba katika kila njia nitakuwa na uhakika kuwahusu ninyi.*

Maelezo ya Chini

Tnn., “bidii yenu kwa ajili yangu.”
Au “kutamani sana kutubu.”
Au “safi kiadili; bila hatia.”
Au labda, “nitakuwa na ujasiri mwingi kwa sababu yenu.”