Barua ya Pili kwa Wathesalonike 2:1-17

  • Yule mtu wa uasi-sheria (1-12)

  • Wahimizwa kubaki imara (13-17)

2  Hata hivyo, akina ndugu, kuhusu kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo+ na kukusanywa kwetu pamoja kwake,+ tunawaomba  msitikiswe upesi kutoka kwenye kufikiri kwenu wala msitishwe na maneno yaliyoongozwa na roho*+ au ujumbe uliosemwa au barua inayodhaniwa kutoka kwetu, kwamba siku ya Yehova*+ imefika.  Msiruhusu mtu yeyote awapotoshe* kwa njia yoyote, kwa sababu siku hiyo haitafika kabla uasi imani+ haujatokea kwanza na yule mtu wa uasi sheria+ kufunuliwa, mwana wa maangamizi.+  Yeye ni mpinzani na hujiinua juu ya wale wanaoitwa mungu au vitu vinavyoabudiwa,* na hivyo huketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha waziwazi kuwa mungu.  Je, hamkumbuki kwamba nilikuwa nikiwaambia mambo hayo nilipokuwa pamoja nanyi?  Sasa mnajua kinachomzuia, ili afunuliwe wakati wake unaofaa.  Kwa kweli, fumbo la uasi sheria huu tayari linafanya kazi,+ lakini ni mpaka tu yule anayeuzuia sasa atakapoondolewa.  Ndipo, kwa kweli, yule mwasi sheria atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamwangamiza kwa roho ya kinywa chake+ na kumharibu kupitia ufunuo+ wa kuwapo kwake.  Lakini kuwapo kwa huyo mwasi sheria ni kupitia kazi ya Shetani+ pamoja na kila tendo lenye nguvu na ishara za uwongo na mambo ya ajabu*+ 10  na kila namna ya udanganyifu usio wa uadilifu+ kwa wale wanaoangamia, kama malipo kwa sababu hawakukubali kuipenda kweli ili waokolewe. 11  Ndiyo sababu Mungu anaacha wapotoshwe kupitia udanganyifu, na hivyo waamini uwongo,+ 12  ili wote wahukumiwe kwa sababu hawakuiamini kweli, bali walipenda ukosefu wa uadilifu. 13  Hata hivyo, tuna wajibu wa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu akina ndugu mnaopendwa na Yehova,* kwa sababu tangu mwanzo Mungu aliwachagua+ ili mwokolewe kwa kuwatakasa+ kupitia roho yake na imani yenu katika kweli. 14  Aliwaita kupitia habari njema tunayotangaza, ili mpate utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.+ 15  Basi, akina ndugu, simameni imara+ na mwendelee kufuata desturi mlizofundishwa,+ iwe ni kupitia ujumbe wa maneno au barua kutoka kwetu. 16  Zaidi ya hayo, Bwana wetu Yesu Kristo, na Mungu Baba yetu aliyetupenda+ na kutupatia faraja ya milele na tumaini jema+ kupitia fadhili zisizostahiliwa, 17  na aifariji mioyo yenu na kuwaimarisha* katika kila tendo na neno jema.

Maelezo ya Chini

Au “kupitia kwa roho.” Angalia Kamusi, “Roho.”
Au “awashawishi.”
Au “vinavyoheshimiwa.”
Au “miujiza.”
Au “kuwatia nguvu.”