Barua ya Pili kwa Wathesalonike 3:1-18

  • Endeleeni kusali (1-5)

  • Onyo dhidi ya kutofuata utaratibu (6-15)

  • Salamu za mwisho (16-18)

3  Mwishowe, akina ndugu, endeleeni kusali kwa ajili yetu,+ ili neno la Yehova* lizidi kuenea upesi+ na kutukuzwa, kama ilivyo kwenu,  na kwamba tukombolewe kutoka kwa watu hatari na waovu,+ kwa maana imani si mali ya watu wote.+  Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha na kuwalinda dhidi ya yule mwovu.  Zaidi ya hayo, tuna uhakika katika Bwana kuwahusu ninyi, kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya mambo tunayowaagiza.  Bwana na aendelee kuongoza mioyo yenu ili mfanikiwe kumpenda Mungu+ na kuvumilia+ kwa ajili ya Kristo.  Sasa akina ndugu, tunawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, mjiepushe na kila ndugu asiyefuata utaratibu+ na desturi* mlizopokea* kutoka kwetu.+  Kwa maana ninyi wenyewe mnajua jinsi mnavyopaswa kutuiga,+ kwa sababu hatukukosa kufuata utaratibu tulipokuwa nanyi,  wala hatukula chakula cha yeyote bure.*+ Badala yake, tulifanya kazi ngumu na yenye kutaabisha usiku na mchana ili tusimpe yeyote kati yenu mzigo wenye gharama.+  Si kwamba hatuna mamlaka,+ bali tulitaka kuwawekea mfano ili mtuige.+ 10  Kwa kweli, tulipokuwa nanyi tulikuwa tukiwaagiza hivi: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, asile chakula.”+ 11  Kwa maana tunasikia watu fulani miongoni mwenu hawafuati utaratibu,+ hawafanyi kazi yoyote, bali wanajiingiza katika mambo yasiyowahusu.+ 12  Tunawaagiza watu hao na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo wafanye kazi kwa utulivu na kula chakula ambacho wao wenyewe wamekifanyia kazi.+ 13  Nanyi akina ndugu, msichoke kutenda mema. 14  Lakini ikiwa yeyote hatii maneno yetu kupitia barua hii, mtieni alama na mwache kushirikiana naye,+ ili aone aibu. 15  Lakini msimwone mtu huyo kama adui, bali endeleeni kumwonya+ kama ndugu. 16  Basi, Bwana wa amani na aendelee kuwapa amani kwa kila njia.+ Bwana awe nanyi nyote. 17  Hii ni salamu yangu, mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe,+ ambayo ni ishara katika kila barua; hivi ndivyo ninavyoandika. 18  Fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu Kristo na ziwe pamoja nanyi nyote.

Maelezo ya Chini

Au “maagizo.”
Au labda, “walizopokea.”
Au “bila kulipa.”