Barua ya Pili ya Yohana 1:1-13

  • Salamu (1-3)

  • Endeleeni kutembea katika kweli (4-6)

  • Jihadharini na wadanganyifu (7-11)

  • Mipango ya kuwatembelea na salamu (12, 13)

 Mwanamume mzee,* kwa bibi aliyechaguliwa na kwa watoto wake, ambao ninawapenda kweli, na si mimi tu, bali pia wale wote ambao wameijua kweli,  kwa sababu ya kweli inayokaa ndani yetu na itakayokuwa pamoja nasi milele.  Tutakuwa na fadhili zisizostahiliwa, rehema, na amani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, pamoja na kweli na upendo.  Ninashangilia sana kwa sababu nimekuta baadhi ya watoto wako wakitembea katika kweli,+ kama tulivyopokea amri kutoka kwa Baba.  Bibi, sasa ninakuomba kwamba tupendane. (Siwaandikii amri mpya, bali amri tuliyokuwa nayo tangu mwanzo.)+  Na upendo unamaanisha hivi, kwamba tuendelee kutembea kulingana na amri zake.+ Hii ndiyo amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mnapaswa kuendelea kutembea ndani yake.  Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea ulimwenguni,+ wale wasiokiri kwamba Yesu Kristo alikuja katika mwili.+ Huyu ndiye yule mdanganyifu na mpinga-Kristo.+  Jihadharini, msije mkapoteza mambo ambayo tumefanya kazi ili kuyatokeza, bali mpate thawabu kamili.+  Kila mtu anayevuka mipaka na ambaye hakai katika fundisho la Kristo hana Mungu.+ Mtu anayekaa katika fundisho hili ndiye aliye na Baba na Mwana pia.+ 10  Mtu yeyote akija kwenu naye haleti fundisho hili, msimpokee nyumbani mwenu+ wala kumsalimu. 11  Kwa maana mtu anayemsalimu anashiriki matendo yake maovu. 12  Ingawa nina mambo mengi ya kuwaandikia, sitaki kufanya hivyo kwa karatasi na wino, bali ninatumaini kuja kwenu na kuzungumza nanyi uso kwa uso, ili shangwe yenu iwe kamili. 13  Watoto wa dada yako, yule aliyechaguliwa, wanakutumia salamu zao.

Maelezo ya Chini

Au “Mzee.”