Barua ya Tatu ya Yohana 1:1-14

  • Salamu na sala (1-4)

  • Gayo apongezwa (5-8)

  • Diotrefe aliyependa makuu (9, 10)

  • Demetrio ashuhudiwa vema (11, 12)

  • Mipango ya kutembelea na salamu (13, 14)

 Mwanamume mzee,* kwa Gayo mpendwa, ninayempenda kweli.  Mpendwa, ninasali kwamba katika mambo yote uendelee kusitawi na kuwa na afya njema, kama unavyositawi* sasa.  Kwa maana nilishangilia sana akina ndugu walipokuja na kutoa ushahidi kuhusu kweli unayoshika, unapoendelea kutembea katika kweli.+  Sina shangwe kubwa* kuliko hii: kwamba nisikie watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.+  Mpendwa, unaonyesha uaminifu kwa yale unayofanya kwa ajili ya akina ndugu, hata kama ni wageni.+  Wametoa ushahidi kuhusu upendo wako mbele ya kutaniko. Tafadhali shughulikia safari yao kwa njia inayomfaa Mungu.+  Kwa maana walisafiri kwa ajili ya jina lake, bila kuchukua kitu chochote+ kutoka kwa watu wa mataifa.  Kwa hiyo, tuna wajibu wa kuwakaribisha watu kama hao,+ ili tuwe wafanyakazi wenzi katika kweli.+  Niliandikia kutaniko jambo fulani, lakini Diotrefe, anayependa kuwa wa kwanza kati yao,+ hakubali kwa heshima jambo lolote kutoka kwetu.+ 10  Hiyo ndiyo sababu nikija, nitayashughulikia matendo anayofanya kwa kueneza maneno mabaya kutuhusu.*+ Hatosheki na hayo, bali pia anakataa kuwakaribisha kwa heshima akina ndugu;+ na wale wanaotaka kuwakaribisha, anajaribu kuwazuia na kuwatupa nje ya kutaniko. 11  Mpendwa, usiige yaliyo mabaya, bali iga yaliyo mema.+ Mtu anayetenda mema anatokana na Mungu.+ Mtu anayetenda mabaya hajamwona Mungu.+ 12  Demetrio ameshuhudiwa vema nao wote na ile kweli yenyewe. Kwa kweli, sisi pia tunatoa ushahidi kumhusu, nanyi mnajua ushahidi tunaotoa ni wa kweli. 13  Nilikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sitaki kuendelea kukuandikia kwa kalamu na wino. 14  Hata hivyo, ninatumaini kukuona hivi karibuni, nasi tutazungumza uso kwa uso. Na uwe na amani. Rafiki wanakutumia salamu zao. Wape rafiki salamu zangu kwa jina.

Maelezo ya Chini

Au “Mzee.”
Au “nafsi yako inavyositawi.”
Au labda, “sababu ya kushukuru.”
Tnn., “akipiga porojo kutuhusu kwa maneno maovu.”