Amosi 2:1-16

  • Wahukumiwa kwa sababu ya kuasi tena na tena (1-16)

2  “Yehova anasema hivi: ‘“Kwa sababu ya maasi matatu* ya Moabu,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,Kwa sababu aliiteketeza mifupa ya mfalme wa Edomu kwa ajili ya chokaa.   Kwa hiyo nitaishushia moto Moabu, Nao utateketeza kabisa minara ya Keriothi yenye ngome;+Moabu itakufa katika ghasia,Kwa kelele za vita, kwa mlio wa pembe.+   Nitamwondoa mtawala* miongoni mwakeNa kuwaua wakuu wake wote pamoja naye,”+ asema Yehova.’   Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Yuda,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,Kwa sababu walikataa sheria* ya Yehova,Na kwa sababu hawakufuata masharti yake;+Lakini uwongo uleule ambao mababu zao walifuata umewapotosha.+   Kwa hiyo nitaishushia moto Yuda,Nao utateketeza kabisa minara ya Yerusalemu yenye ngome.’+   Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Israeli,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,Kwa sababu wanamuuza mwadilifu ili wapate fedha,Na maskini kwa jozi ya viatu.+   Wanavikanyaga-kanyaga vichwa vya watu wa hali ya chini katika mavumbi ya dunia,+Nao wanaziba njia ya wapole.+ Mtu na baba yake wanalala na msichana yuleyule,Na hivyo kulichafua jina langu takatifu.   Wanajinyoosha kando ya kila madhabahu+ juu ya nguo walizochukua kwa nguvu kutoka kwa maskini kama dhamana ya mkopo;*+Na divai wanayokunywa katika nyumba ya* miungu yao waliipata kutoka kwa wale waliowatoza faini.’   ‘Lakini ni mimi niliyemwangamiza Mwamori mbele yao,+Aliyekuwa mrefu kama mierezi na mwenye nguvu kama mialoni;Niliyaharibu matunda yake juu na mizizi yake chini.+ 10  Nilikupandisha kutoka nchini Misri,+Nami nikakufanya utembee kupitia nyikani kwa miaka 40,+Ili umiliki nchi ya Mwamori. 11  Niliwainua baadhi ya wana wako kuwa manabii+Na baadhi ya vijana wako wa kiume kuwa Wanadhiri.+ Je, sivyo ilivyo, enyi watu wa Israeli?’ asema Yehova. 12  ‘Lakini uliendelea kuwapa Wanadhiri divai wanywe,+Nawe ukawaamuru hivi manabii: “Hampaswi kutoa unabii.”+ 13  Basi nitakupondaponda mahali pako,Kama vile ambavyo gari la kukokotwa lililojazwa miganda ya nafaka iliyotoka kuvunwa linavyopondaponda kilicho njiani. 14  Mwenye mbio hatakuwa na mahali pa kukimbilia,+Mwenye nguvu hatabaki na nguvu zake,Na hakuna shujaa atakayeokoa uhai wake.* 15  Mwanamume anayeshika upinde hatasimama,Mtu anayekimbia kwa kasi* hataponyoka,Na mpanda farasi hataokoa uhai wake.* 16  Hata mashujaa wenye ujasiri* zaidiWatakimbia uchi siku hiyo,’+ asema Yehova.”

Maelezo ya Chini

Au “matendo matatu ya uhalifu.”
Tnn., “mwamuzi.”
Au “mafundisho.”
Au “hekalu la.”
Au “rehani.”
Au “nafsi yake.”
Tnn., “mwenye miguu myepesi.”
Au “nafsi yake.”
Au “wenye moyo mkuu.”