Amosi 3:1-15

  • Kutangaza hukumu ya Yehova (1-8)

    • Mungu afunua siri yake (7)

  • Ujumbe dhidi ya Samaria (9-15)

3  “Sikieni neno hili ambalo Yehova amesema kuwahusu ninyi, enyi watu wa Israeli, kuhusu familia nzima niliyoipandisha kutoka nchini Misri:   ‘Ni ninyi peke yenu niliowajua kati ya familia zote duniani.+ Ndiyo sababu nitawafanya muwajibike* kwa sababu ya makosa yenu yote.+   Je, watu wawili watatembea pamoja ikiwa hawajakubaliana kukutana?*   Je, simba atanguruma mwituni ikiwa hana mawindo? Je, mwanasimba* atanguruma pangoni mwake ikiwa hajakamata chochote?   Je, ndege ataanguka kwenye mtego ardhini ikiwa hakuna mtego wa kumnasa?* Je, mtego hufyatuka ardhini ikiwa haujanasa chochote?   Pembe ikipigwa jijini, je, watu hawatetemeki? Msiba ukitokea jijini, je, si Yehova aliyetenda?   Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hatafanya jambo loloteKabla hajawafunulia watumishi wake manabii siri yake.+   Simba amenguruma!+ Ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema! Ni nani ambaye hatatoa unabii?’+   ‘Tangazeni jambo hilo kwenye minara ya Ashdodi yenye ngomeNa kwenye minara yenye ngome katika nchi ya Misri. Semeni: “Kusanyikeni pamoja dhidi ya milima ya Samaria;+Tazameni machafuko yaliyo ndani yakeNa ulaghai ulio ndani yake.+ 10  Kwa maana hawajui kufanya yaliyo sawa,” asema Yehova,“Wale wanaojikusanyia ukatili na maangamizi katika minara yao yenye ngome.”’ 11  Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Adui ataizingira nchi,+Atakuvua nguvu zako,Na minara yako yenye ngome itaporwa.’+ 12  Yehova anasema hivi: ‘Kama mchungaji anavyompokonya simba miguu miwili au kipande cha sikio kutoka kinywani mwake,Hivyo ndivyo watu wa Israeli watakavyookolewa,Wale ambao sasa wanaketi kwenye vitanda vya kifahari na kwenye makochi bora* kule Samaria.’+ 13  ‘Sikieni na kuionya* nyumba ya Yakobo,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mungu wa majeshi. 14  ‘Kwa maana siku nitakapowafanya Waisraeli wawajibike* kwa sababu ya maasi yao yote,*+Pia nitawafanya wawajibike kwa sababu ya madhabahu za Betheli;+Pembe za madhabahu zitakatwa na kuanguka ardhini.+ 15  Nitaibomoa nyumba ya majira ya baridi kali pamoja na nyumba ya majira ya kiangazi.’ ‘Nyumba za pembe za tembo zitatoweka,+Na majumba makubwa hayatasalia,’*+ asema Yehova.”

Maelezo ya Chini

Au “nitawaadhibu.”
Au “hawajakutana kama walivyokubaliana.”
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Au labda, “ikiwa hauna chambo?”
Au “makochi ya Damasko.”
Au “kutoa ushahidi dhidi ya.”
Au “nitakapowaadhibu Waisraeli.”
Au “matendo yao yote ya uhalifu.”
Au labda, “nyumba nyingi hazitasalia.”