Amosi 3:1-15
3 “Sikieni neno hili ambalo Yehova amesema kuwahusu ninyi, enyi watu wa Israeli, kuhusu familia nzima niliyoipandisha kutoka nchini Misri:
2 ‘Ni ninyi peke yenu niliowajua kati ya familia zote duniani.+
Ndiyo sababu nitawafanya muwajibike* kwa sababu ya makosa yenu yote.+
3 Je, watu wawili watatembea pamoja ikiwa hawajakubaliana kukutana?*
4 Je, simba atanguruma mwituni ikiwa hana mawindo?
Je, mwanasimba* atanguruma pangoni mwake ikiwa hajakamata chochote?
5 Je, ndege ataanguka kwenye mtego ardhini ikiwa hakuna mtego wa kumnasa?*
Je, mtego hufyatuka ardhini ikiwa haujanasa chochote?
6 Pembe ikipigwa jijini, je, watu hawatetemeki?
Msiba ukitokea jijini, je, si Yehova aliyetenda?
7 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hatafanya jambo loloteKabla hajawafunulia watumishi wake manabii siri yake.+
8 Simba amenguruma!+ Ni nani ambaye hataogopa?
Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema! Ni nani ambaye hatatoa unabii?’+
9 ‘Tangazeni jambo hilo kwenye minara ya Ashdodi yenye ngomeNa kwenye minara yenye ngome katika nchi ya Misri.
Semeni: “Kusanyikeni pamoja dhidi ya milima ya Samaria;+Tazameni machafuko yaliyo ndani yakeNa ulaghai ulio ndani yake.+
10 Kwa maana hawajui kufanya yaliyo sawa,” asema Yehova,“Wale wanaojikusanyia ukatili na maangamizi katika minara yao yenye ngome.”’
11 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
‘Adui ataizingira nchi,+Atakuvua nguvu zako,Na minara yako yenye ngome itaporwa.’+
12 Yehova anasema hivi:
‘Kama mchungaji anavyompokonya simba miguu miwili au kipande cha sikio kutoka kinywani mwake,Hivyo ndivyo watu wa Israeli watakavyookolewa,Wale ambao sasa wanaketi kwenye vitanda vya kifahari na kwenye makochi bora* kule Samaria.’+
13 ‘Sikieni na kuionya* nyumba ya Yakobo,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mungu wa majeshi.
14 ‘Kwa maana siku nitakapowafanya Waisraeli wawajibike* kwa sababu ya maasi yao yote,*+Pia nitawafanya wawajibike kwa sababu ya madhabahu za Betheli;+Pembe za madhabahu zitakatwa na kuanguka ardhini.+
15 Nitaibomoa nyumba ya majira ya baridi kali pamoja na nyumba ya majira ya kiangazi.’
‘Nyumba za pembe za tembo zitatoweka,+Na majumba makubwa hayatasalia,’*+ asema Yehova.”
Maelezo ya Chini
^ Au “nitawaadhibu.”
^ Au “hawajakutana kama walivyokubaliana.”
^ Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
^ Au labda, “ikiwa hauna chambo?”
^ Au “makochi ya Damasko.”
^ Au “kutoa ushahidi dhidi ya.”
^ Au “nitakapowaadhibu Waisraeli.”
^ Au “matendo yao yote ya uhalifu.”
^ Au labda, “nyumba nyingi hazitasalia.”