Amosi 4:1-13
4 “Sikieni neno hili, enyi ng’ombe wa Bashani,Mlio kwenye mlima wa Samaria,+Ninyi wanawake mnaowalaghai watu wa hali ya chini+ na kuwakandamiza maskini,Mnaowaambia waume zenu,* ‘Tuleteeni kinywaji!’
2 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameapa kwa utakatifu wake,‘“Tazameni! Siku zinakuja wakati ambapo atawainua juu kwa kulabu za mchinjaji wa wanyamaNa wale watakaobaki kati yenu kwa ndoano za samaki.
3 Kila mmoja wenu atatoka nje moja kwa moja kupitia sehemu zilizobomolewa ukutani;Nanyi mtatupwa kule Harmoni,” asema Yehova.’
4 ‘Njooni Betheli mtende dhambi,*+Njooni Gilgali mzidi kutenda dhambi!+
Leteni dhabihu zenu+ asubuhi,Na sehemu zenu za kumi+ katika siku ya tatu.
5 Teketezeni dhabihu ya shukrani ya mikate iliyotiwa chachu;+Tangazeni kwa sauti matoleo yenu ya hiari!
Kwa maana hivyo ndivyo mnavyopenda kufanya, enyi watu wa Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
6 ‘Lakini mimi niliyafanya meno yenu yawe safi bila chakula* katika majiji yenu yoteNikasababisha mkose mikate katika nyumba zenu zote;+Lakini hamkunirudia,’+ asema Yehova.
7 ‘Pia niliwanyima mvua miezi mitatu kabla ya mavuno;+Nilileta mvua katika jiji moja lakini sikuileta katika jiji lingine.
Shamba moja lilipata mvua,Lakini shamba lingine lilikauka kwa sababu halikupata mvua.
8 Watu wa majiji mawili au matatu walipepesuka kwenda kwenye jiji moja kunywa maji,+Nao hawakutosheka;Lakini hamkunirudia,’+ asema Yehova.
9 ‘Niliwapiga kwa joto linalounguza na kuvu.+
Mlizidisha bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu,Lakini nzige walitafuna mitini yenu na mizeituni yenu;+Na bado hamkunirudia,’+ asema Yehova.
10 ‘Niliwaletea ugonjwa hatari kama ule wa* Misri.+
Niliwaua vijana wenu wa kiume+ kwa upanga na kuwateka farasi wenu.+
Nilifanya uvundo wa kambi zenu upande katika mianzi ya pua zenu;+Lakini hamkunirudia,’ asema Yehova.
11 ‘NiliwaangamizaKama Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora.+
Nanyi mlikuwa kama gogo lililochomolewa haraka motoni;Lakini hamkunirudia,’+ asema Yehova.
12 Basi hivyo ndivyo nitakavyokutendea, Ee Israeli.
Kwa kuwa nitakutendea hivyo,Jitayarishe kukutana na Mungu wako, Ee Israeli.
13 Kwa maana tazama! yeye Ndiye aliyeumba milima+ na kuumba upepo;+Humwambia mwanadamu mawazo Yake,Hubadili mapambazuko kuwa giza,+Naye hukanyaga vilele vya dunia;+Yehova Mungu wa majeshi ndilo jina lake.”