Amosi 6:1-14

  • Ole wao wasiojali! (1-14)

    • Vitanda vya pembe za tembo; mabakuli ya divai (4, 6)

6  “Ole wao wanaojitumaini* huko Sayuni,Wale wanaojiona wakiwa salama katika mlima wa Samaria,+Wanaume maarufu wa taifa kuu zaidi kati ya mataifa,Wale ambao nyumba ya Israeli huwaendea!   Vukeni mwende Kalne mkaone. Tokeni huko mwende katika Jiji Kubwa la Hamathi,+Na mteremke mpaka jiji la Gathi la Wafilisti. Je, majiji hayo ni bora kuliko falme hizi,*Au je, eneo lao ni kubwa kuliko lenu?   Je, mnaiondoa akilini mwenu ile siku ya msiba+Na kuukaribisha utawala wa* ukatili?+   Wanalalia vitanda vya pembe za tembo+ na kujinyoosha kwenye makochi,+Wakila kondoo dume wa kundi na ndama* waliononeshwa;+   Wanatunga nyimbo papo hapo kupatana na sauti ya kinubi,*+Na kama Daudi, wanabuni ala za muziki;+   Wanakunywa divai iliyojazwa kwenye mabakuli+Na kujitia wenyewe mafuta yaliyo bora. Lakini hawajali* msiba wa Yosefu.+   Basi watakuwa mstari wa mbele kupelekwa uhamishoni,+Na karamu zenye shamrashamra za wanaojinyoosha kwa starehe zitakoma.   ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameapa kwa nafsi yake mwenyewe,’+ asema Yehova Mungu wa majeshi,‘“Nakichukia sana kiburi cha Yakobo,+Naichukia minara yake yenye ngome,+Nami nitawapa wengine jiji lao na vyote vilivyomo.+  “‘“Na watu kumi wakibaki katika nyumba moja, wao pia watakufa. 10  Mtu wa ukoo* atakuja na kuwatoa nje na kuwachoma mmoja baada ya mwingine. Ataitoa mifupa yao ndani ya nyumba hiyo; kisha atamuuliza yeyote aliye katika vyumba vya ndani vya nyumba hiyo, ‘Je, kuna wengine pamoja nawe?’ Naye atajibu, ‘Hakuna yeyote!’ Kisha atasema, ‘Nyamaza kimya! Kwa maana huu si wakati wa kutaja kwa vyovyote vile jina la Yehova.’” 11  Kwa maana ni Yehova anayetoa amri hiyo,+Naye ataibomoa ile nyumba kubwa ibaki rundo la mawe,Na nyumba ndogo ibaki kifusi.+ 12  Je, farasi hukimbia kwenye mwamba,Au je, mtu anaweza kulima kwa ng’ombe kwenye mwamba? Kwa maana mmebadili haki kuwa mmea wenye sumu,Na tunda la uadilifu kuwa pakanga.*+ 13  Mnashangilia jambo lisilo na manufaa yoyote,Nanyi mnasema, “Je, hatujapata nguvu* kwa uwezo wetu wenyewe?”+ 14  Kwa hiyo, Ee nyumba ya Israeli, nitaleta taifa dhidi yenu,’+ asema Yehova Mungu wa majeshi,‘Nao litawakandamiza kuanzia Lebo-hamathi*+ mpaka kwenye Korongo* la Araba.’”

Maelezo ya Chini

Au “wasiojali.”
Inaonekana falme hizo ni Yuda na Israeli.
Tnn., “kukikaribisha kiti cha.”
Au “ng’ombe dume wachanga.”
Au “kinanda.”
Tnn., “hawakuwa wagonjwa kwa sababu ya.”
Tnn., “Ndugu ya baba yake.”
Au “uchungu.”
Tnn., “hatukujitwalia pembe.”
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Angalia Kamusi.