Amosi 8:1-14

  • Maono ya kikapu kilichojaa matunda ya wakati wa kiangazi (1-3)

  • Wakandamizaji washutumiwa (4-14)

    • Njaa ya kiroho (11)

8  Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova alinionyesha mambo haya: Tazama! Kulikuwa na kikapu chenye matunda ya wakati wa kiangazi.  Kisha akaniuliza, “Unaona nini, Amosi?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda ya wakati wa kiangazi.” Kisha Yehova akaniambia: “Mwisho wa watu wangu Waisraeli umefika. Sitawasamehe tena.+  ‘Siku hiyo nyimbo za hekalu zitabadilika kuwa kilio kikubwa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Kutakuwa na mizoga mingi iliyotupwa kila mahali+—kimya cha ajabu!’   Sikieni hili, ninyi mnaowakandamiza maskiniNa kuwaangamiza wapole nchini,+   Mnaosema, ‘Sherehe ya mwezi mpya itakwisha lini,+ ili tuuze nafaka yetu,Na Sabato+ itakwisha lini, tukauze nafaka? Ili tupunguze kipimo cha efa*Na kuongeza uzito wa shekeli,*Kuipotosha mizani yetu ya udanganyifu;+   Ili tuwanunue wenye uhitaji kwa fedhaNa maskini kwa jozi ya viatu,+Na kuuza makapi ya nafaka.’   Yehova ameapa kwa Fahari ya Yakobo,+‘Sitasahau kamwe matendo yao yote.+   Kwa sababu hiyo nchi* itatetemeka,Na kila mkaaji nchini ataomboleza.+ Je, nchi yote haitapanda kama Mto Nile,Na kuinuka na kushuka chini kama Mto Nile wa Misri?’+   ‘Siku hiyo,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,‘Nitalifanya jua litue wakati wa adhuhuri,Nami nitaitia nchi giza siku nyangavu.+ 10  Nitabadili sherehe zenu ziwe maombolezo+Na nyimbo zenu zote ziwe nyimbo za huzuni.* Nitavisha nyonga zote nguo za magunia na kukitia kila kichwa upara;Nitafanya wakati huo uwe kama wakati wa kumwombolezea mwana wa pekee,Na mwisho wake kama siku yenye uchungu.’ 11  ‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,‘Nitakapoleta njaa kali nchini,Si njaa kali ya chakula* au kiu ya maji,Bali ya kusikia maneno ya Yehova.+ 12  Watapepesuka kutoka bahari mpaka bahariNa kutoka kaskazini mpaka mashariki.* Watatangatanga wakitafuta neno la Yehova, lakini hawatalipata. 13  Siku hiyo mabikira warembo watazimia,Na pia vijana wa kiume, kwa sababu ya kiu; 14  Wale wanaoapa kwa hatia ya Samaria+ na kusema,“Kwa hakika kama mungu wako anavyoishi, Ee Dani!”+ Na, “Kwa hakika kama inavyoishi njia ya Beer-sheba!”+ Wataanguka, na hawatainuka tena.’”+

Maelezo ya Chini

Au “dunia.”
Au “maombolezo.”
Tnn., “mkate.”
Au “mawio ya jua.”