Amosi 9:1-15

  • Hukumu za Mungu haziepukiki (1-10)

  • Kibanda cha Daudi kitainuliwa (11-15)

9  Nilimwona Yehova+ akiwa juu ya madhabahu, naye akasema: “Piga kichwa cha nguzo, na vizingiti vitatikisika. Kata vichwa vya nguzo, nami nitamuua wa mwisho kwa upanga. Hakuna yeyote anayekimbia atakayeponyoka, na hakuna yeyote anayejaribu kutoroka atakayefanikiwa.+   Wakichimba chini kuingia Kaburini,*Mkono wangu utawatoa humo;Na wakipanda juu mbinguni,Nitawashusha chini kutoka huko.   Nao wakijificha kwenye kilele cha Karmeli,Nitawasaka na kuwatoa huko.+ Wakijificha chini ya bahari ili macho yangu yasiwaone,Huko nitamwamuru nyoka awaume.   Wakipelekwa utekwani na maadui wao,Huko nitauamuru upanga, nao utawaua;+Nitawakazia macho kwa mabaya, wala si kwa mema.+   Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, Ndiye anayeigusa nchi,*Hivi kwamba inayeyuka,+ na wakaaji wake wote wataomboleza;+Na nchi yote itapanda kama Mto Nile,Na kushuka chini kama Mto Nile wa Misri.+   ‘Yule anayejenga ngazi zake mbinguniNa kujenga jengo* lake juu ya dunia;Yule anayeyaita maji ya bahari,Ili ayamwage duniani+—Yehova ndilo jina lake.’+   ‘Je, ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu, enyi watu wa Israeli?’ asema Yehova. ‘Je, sikuwapandisha Waisraeli kutoka nchini Misri,+Na Wafilisti kutoka Krete,+ na Wasiria kutoka Kiri?’+   ‘Tazameni! Macho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova yanautazama ufalme huu wenye dhambi,Naye atauangamiza kabisa kutoka nchini.+ Lakini sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,’+ asema Yehova.   ‘Kwa maana tazameni! Ninatoa amri,Nami nitaichekecha nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote,+Kama mtu anavyochekecha nafaka kwa chujio,Na hakuna kijiwe hata kimoja kinachoanguka chini. 10  Watu wangu wote wanaotenda dhambi watauawa kwa upanga,Wale wanaosema: “Msiba hautatukaribia wala kutufikia.”’ 11  ‘Siku hiyo nitakiinua kibanda cha Daudi+ kilichoanguka,*Nitarekebisha sehemu* zilizoharibika,Na kujenga upya magofu yake;Nitakijenga upya kama kilivyokuwa siku za kale,+ 12  Ili wamiliki sehemu zilizobaki za Edomu,+Na mataifa yote yanayoitwa kwa jina langu,’ asema Yehova, anayefanya hayo. 13  ‘Tazameni! Siku zinakuja,’ asema Yehova,‘Wakati ambapo mtu anayelima kwa plau atampita anayevuna,Na anayekanyaga zabibu atampita anayepanda mbegu;+Na milima itadondosha divai tamu,+Na vilima vyote vitatiririka divai.*+ 14  Nitawakusanya na kuwarudisha watu wangu Waisraeli walio utekwani,+Nao watajenga upya majiji yaliyoachwa ukiwa na kuishi humo;+Watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake,+Nao watalima bustani za matunda na kula matunda yake.’+ 15  ‘Nitawapanda katika nchi yao,Nao hawatang’olewa tena kamweKutoka katika nchi yao ambayo nimewapa,’+ asema Yehova Mungu wenu.”

Maelezo ya Chini

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “dunia.”
Au “kuba.”
Au “hema la Daudi lililoanguka.”
Au “sehemu zao.”
Tnn., “vitayeyuka.”