Amosi 9:1-15
9 Nilimwona Yehova+ akiwa juu ya madhabahu, naye akasema: “Piga kichwa cha nguzo, na vizingiti vitatikisika. Kata vichwa vya nguzo, nami nitamuua wa mwisho kwa upanga. Hakuna yeyote anayekimbia atakayeponyoka, na hakuna yeyote anayejaribu kutoroka atakayefanikiwa.+
2 Wakichimba chini kuingia Kaburini,*Mkono wangu utawatoa humo;Na wakipanda juu mbinguni,Nitawashusha chini kutoka huko.
3 Nao wakijificha kwenye kilele cha Karmeli,Nitawasaka na kuwatoa huko.+
Wakijificha chini ya bahari ili macho yangu yasiwaone,Huko nitamwamuru nyoka awaume.
4 Wakipelekwa utekwani na maadui wao,Huko nitauamuru upanga, nao utawaua;+Nitawakazia macho kwa mabaya, wala si kwa mema.+
5 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, Ndiye anayeigusa nchi,*Hivi kwamba inayeyuka,+ na wakaaji wake wote wataomboleza;+Na nchi yote itapanda kama Mto Nile,Na kushuka chini kama Mto Nile wa Misri.+
6 ‘Yule anayejenga ngazi zake mbinguniNa kujenga jengo* lake juu ya dunia;Yule anayeyaita maji ya bahari,Ili ayamwage duniani+—Yehova ndilo jina lake.’+
7 ‘Je, ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu, enyi watu wa Israeli?’ asema Yehova.
‘Je, sikuwapandisha Waisraeli kutoka nchini Misri,+Na Wafilisti kutoka Krete,+ na Wasiria kutoka Kiri?’+
8 ‘Tazameni! Macho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova yanautazama ufalme huu wenye dhambi,Naye atauangamiza kabisa kutoka nchini.+
Lakini sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,’+ asema Yehova.
9 ‘Kwa maana tazameni! Ninatoa amri,Nami nitaichekecha nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote,+Kama mtu anavyochekecha nafaka kwa chujio,Na hakuna kijiwe hata kimoja kinachoanguka chini.
10 Watu wangu wote wanaotenda dhambi watauawa kwa upanga,Wale wanaosema: “Msiba hautatukaribia wala kutufikia.”’
11 ‘Siku hiyo nitakiinua kibanda cha Daudi+ kilichoanguka,*Nitarekebisha sehemu* zilizoharibika,Na kujenga upya magofu yake;Nitakijenga upya kama kilivyokuwa siku za kale,+
12 Ili wamiliki sehemu zilizobaki za Edomu,+Na mataifa yote yanayoitwa kwa jina langu,’ asema Yehova, anayefanya hayo.
13 ‘Tazameni! Siku zinakuja,’ asema Yehova,‘Wakati ambapo mtu anayelima kwa plau atampita anayevuna,Na anayekanyaga zabibu atampita anayepanda mbegu;+Na milima itadondosha divai tamu,+Na vilima vyote vitatiririka divai.*+
14 Nitawakusanya na kuwarudisha watu wangu Waisraeli walio utekwani,+Nao watajenga upya majiji yaliyoachwa ukiwa na kuishi humo;+Watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake,+Nao watalima bustani za matunda na kula matunda yake.’+
15 ‘Nitawapanda katika nchi yao,Nao hawatang’olewa tena kamweKutoka katika nchi yao ambayo nimewapa,’+ asema Yehova Mungu wenu.”