Ayubu 10:1-22

  • Ayubu aendelea kujibu (1-22)

    • ‘Kwa nini Mungu anapambana nami?’ (2)

    • Mungu si kama Ayubu anayeweza kufa (4-12)

    • ‘Naomba nipate kitulizo kidogo’ (20)

10  “Nayachukia sana* maisha yangu.+ Nitamwaga malalamiko yangu. Nitasema waziwazi katika mateso yangu makali!*   Nitamwambia Mungu: ‘Usinitangaze kuwa mwenye hatia. Niambie kwa nini unapambana nami.   Je, unafaidika unaponikandamiza,Unapodharau kazi ya mikono yako+Huku ukipendelea ushauri wa waovu?   Je, una macho ya kimwili,Au je, unaona kama mwanadamu anayeweza kufa anavyoona?   Je, siku zako ni kama siku za wanadamu wanaoweza kufa,Au je, miaka yako ni kama ya mwanadamu,+   Hivi kwamba utafute kosa languNa kuendelea kutafuta dhambi yangu?+   Unajua kwamba sina hatia;+Na hakuna yeyote anayeweza kuniokoa kutoka mkononi mwako.+   Mikono yako mwenyewe ilinifinyanga na kuniumba,+Lakini sasa unataka kuniangamiza kabisa.   Tafadhali, kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo,+Lakini sasa unanirudisha mavumbini.+ 10  Je, hukunimwaga kama maziwaNa kunigandisha kama jibini? 11  Ulinivisha ngozi na nyama,Na kunifuma kwa mifupa na misuli.+ 12  Umenipa uhai na kunipenda kwa ushikamanifu;Umeilinda na kuitunza roho yangu.*+ 13  Lakini ulikusudia kwa siri kufanya mambo haya.* Najua kwamba mambo haya yametoka kwako. 14  Ikiwa ningetenda dhambi, ungenitazama,+Nawe hungenisamehe kosa langu. 15  Kama nina hatia, ole wangu! Na hata kama sina hatia, siwezi kuinua kichwa changu,+Kwa sababu nimejaa aibu na mateso.+ 16  Nikiinua kichwa changu juu, unaniwinda kama simba+Na kuonyesha tena nguvu zako dhidi yangu. 17  Unaleta mashahidi wapya dhidi yanguNa kuzidisha hasira yako dhidi yangu,Huku shida baada ya shida ikinikabili. 18  Basi kwa nini ulinitoa katika tumbo la mama yangu?+ Laiti ningekufa kabla ya jicho lolote kuniona. 19  Ingekuwa kana kwamba sikuwahi kuwepo;Ningetolewa moja kwa moja tumboni na kupelekwa kaburini.’ 20  Je, siku zangu si chache?+ Naomba aniache;Na ayageuze macho yake mbali nami, ili nipate kitulizo kidogo*+ 21  Kabla sijaenda zangu—nami sitarudi+Katika nchi yenye giza zito kabisa,*+ 22  Kwenye nchi yenye giza totoro,Nchi ya kivuli kizito na vurugu,Ambako hata nuru ni kama giza.”

Maelezo ya Chini

Au “Nafsi yangu inachukia sana.”
Au “kwa uchungu mwingi sana wa nafsi yangu!”
Au “pumzi yangu; uhai wangu.”
Tnn., “Na mambo haya umeyaficha moyoni mwako.”
Au “nichangamke kidogo.”
Au “yenye giza na kivuli cha kifo.”