Ayubu 12:1-25

  • Jibu la Ayubu (1-25)

    • “Mimi si duni kwenu” (3)

    • “Nimekuwa kichekesho” (4)

    • ‘Mungu ana hekima’ (13)

    • Mungu ni mkuu kuliko waamuzi na wafalme (17, 18)

12  Kisha Ayubu akajibu:   “Kwa kweli ninyi ndio mnaojua,*Na hekima itakufa pamoja nanyi!   Lakini mimi pia nina uelewaji.* Mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya?   Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu,+Mtu anayemlilia Mungu ili amjibu.+ Mtu mwadilifu na asiye na lawama ni kichekesho.   Mtu asiye na mahangaiko hudharau msiba,Akifikiri kwamba msiba huwajia tu wale ambao miguu yao inayumbayumba.*   Mahema ya wezi yana amani,+Na wale wanaomkasirisha Mungu wako salama,+Wale wanaobeba mungu wao mikononi mwao.   Lakini, tafadhali, waulize wanyama, nao watakufundisha;Pia ndege wa angani, nao watakwambia.   Au ichunguze* dunia, nayo itakufundisha;Na samaki wa baharini watakutangazia.   Ni nani kati ya hao wote asiyejuaKwamba mkono wa Yehova umefanya haya? 10  Uhai wa kila kiumbe umo* mikononi mwakeNa roho* ya kila mwanadamu.+ 11  Je, sikio halipimi manenoKama ulimi unavyoonja* chakula?+ 12  Je, hekima haipatikani miongoni mwa waliozeeka,+Na je, uelewaji hauji kwa sababu ya kuishi muda mrefu? 13  Yeye ana hekima na nguvu;+Ana mashauri na uelewaji.+ 14  Anapobomoa kitu, hakiwezi kujengwa tena;+Alichofunga, hakuna mwanadamu anayeweza kukifungua. 15  Anapoyazuia maji, kila kitu hukauka;+Anapoyaachilia, yanailemea dunia.+ 16  Ana nguvu na hekima inayotumika;+Anayepotosha na anayepotoshwa wote ni wake; 17  Huwafanya washauri watembee bila viatu,*Naye huwafanya waamuzi waonekane wapumbavu.+ 18  Hulegeza pingu zilizofungwa na wafalme,+Naye huwafunga mshipi kiunoni. 19  Huwafanya makuhani watembee bila viatu,+Naye huwapindua walio imara kabisa katika mamlaka;+ 20  Huwanyamazisha washauri wanaotegemekaNa kuwapokonya wanaume wazee* busara; 21  Huwamwagia wakuu dharau,+Naye huwafanya wenye nguvu wawe dhaifu;* 22  Hufunua mambo yenye kina kutoka gizani,+Naye huleta giza zito kwenye nuru; 23  Huyafanya mataifa yawe na nguvu ili ayaangamize;Huyafanya mataifa yawe makubwa ili ayapeleke uhamishoni. 24  Huwapokonya viongozi wa watu uelewaji* waoNa kuwafanya watangetange jangwani kusiko na njia.+ 25  Wao hupapasa-papasa gizani,+ ambamo hamna nuru;Huwafanya wapepesuke kama walevi.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ninyi ndio watu.”
Tnn., “moyo.”
Au “inateleza.”
Au labda, “zungumza na.”
Au “Nafsi ya kila mtu aliye hai imo.”
Au “pumzi.”
Tnn., “kaakaa linavyoonja.”
Au “bila chochote.”
Au “wazee.”
Tnn., “hulegeza mshipi wa wenye nguvu.”
Tnn., “moyo.”