Ayubu 16:1-22

  • Jibu la Ayubu (1-22)

    • ‘Ninyi ni wafariji wasumbufu!’ (2)

    • Adai kwamba Mungu anamfanya kuwa shabaha yake (12)

16  Ayubu akajibu:  “Nimeshasikia mambo mengi kama hayo. Ninyi nyote ni wafariji wasumbufu!+   Je, maneno yasiyo na maana* yana mwisho? Ni nini kinachowachochea kujibu hivi?   Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi. Ikiwa mngekuwa katika hali yangu,*Ningetoa hoja zenye kusadikisha dhidi yenuNa kuwatikisia kichwa changu.+   Hata hivyo, badala yake, ningewaimarisha kwa maneno ya kinywa changu,Na faraja ya midomo yangu ingewatuliza.+   Nikiongea, maumivu yangu mwenyewe hayatulii,+Nami nikiacha kuongea, maumivu yangu yanapungua kwa kadiri gani?   Lakini sasa amenichosha;+Ameiangamiza nyumba yangu yote.*   Pia unanikamata, na wengine wameshuhudia jambo hilo,Hivi kwamba kukonda kwangu kumezidi na kunatoa ushahidi mbele yangu.   Hasira yake imenirarua vipandevipande, naye ana chuki kunielekea.+ Hunisagia meno yake. Adui yangu hunitoboa kwa macho yake.+ 10  Wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yangu,+Nao wameyapiga mashavu yangu kwa dharau;Wanakusanyika kwa wingi dhidi yangu.+ 11  Mungu hunitia mikononi mwa wavulana,Naye hunitupa kwa nguvu mikononi mwa waovu.+ 12  Nilikuwa na amani, lakini akanivunjavunja;+Alinikamata nyuma shingoni na kunipondaponda;Kisha akanifanya shabaha yake. 13  Wapiga mishale wake wananizunguka;+Huzichoma figo+ zangu bila huruma;Humwaga nyongo yangu ardhini. 14  Hunitoboa tena na tena kama ukuta;Hunishambulia kama shujaa. 15  Nimeshona nguo ya magunia ili kufunika ngozi yangu,+Nami nimezika heshima yangu* mavumbini.+ 16  Uso wangu ni mwekundu kwa sababu ya kulia,+Na kuna kivuli kizito* juu ya kope zangu, 17  Ingawa mikono yangu haijatenda ukatili wowote Na sala yangu ni safi. 18  Ee dunia, usiifunike damu yangu!+ Acha kilio changu kisiwe na mahali pa kupumzikia! 19  Hata sasa, shahidi wangu yuko mbinguni;Yule anayeweza kunitetea yuko juu. 20  Rafiki zangu wananidhihaki+Huku macho yangu yakimwaga machozi* nikimlilia Mungu.+ 21  Acha mtu fulani awe mwamuzi kati ya mwanadamu na Mungu,Kama anavyoweza kuwa mwamuzi kati ya mtu mmoja na mwenzake.+ 22  Kwa maana miaka iliyobaki ni michache,Nami nitafuata njia ambayo wale wanaoifuata hawarudi.+

Maelezo ya Chini

Au “ya ubatili.”
Au “Ikiwa nafsi zenu zingechukua nafasi ya nafsi yangu.”
Au “Amewaangamiza wale wanaokusanyika nami.”
Au “nguvu zangu.” Tnn., “pembe yangu.”
Au “kivuli cha kifo.”
Au labda, “yakikosa usingizi.”