Ayubu 17:1-16

  • Ayubu aendelea kujibu (1-16)

    • “Wadhihaki wananizunguka” (2)

    • “Amenifanya niwe kitu cha kudharauliwa” (6)

    • “Kaburi litakuwa makao yangu” (13)

17  “Roho yangu imevunjwa, siku zangu zimezimwa;Makaburi yananingojea.+   Wadhihaki wananizunguka,+Na macho yangu yanalazimika kutazama* uasi wao.   Tafadhali ikubali dhamana yangu, na ukae nayo. Ni nani mwingine atakayenipa mkono wake na kutoa dhamana kwa niaba yangu?+   Kwa sababu umeficha utambuzi mbali na moyo wao;+Ndiyo maana huwakwezi.   Huenda akajitolea kushiriki vitu vyake na rafiki zake,Huku macho ya watoto wake yakidhoofika.   Amenifanya niwe kitu cha kudharauliwa* miongoni mwa mataifa,+Hivi kwamba nikawa mtu wanayemtemea mate usoni.+   Macho yangu yanafifia kwa sababu ya maumivu makali,+Na viungo vyangu vyote ni kivuli tu.   Watu wanyoofu wananitazama kwa mshangao,Na asiye na hatia anasumbuka kwa sababu ya mtu anayemkataa Mungu.*   Mwadilifu anaendelea kushikamana na njia yake,+Na mwenye mikono safi anazidi kuwa na nguvu.+ 10  Hata hivyo, nyote mnaweza kuja na kuendelea kunishambulia kwa hoja zenu,Kwa maana sijamwona yeyote mwenye hekima miongoni mwenu.+ 11  Siku zangu zimekwisha;+Mipango yangu, tamaa za moyo wangu, zimevunjwavunjwa.+ 12  Wanaendelea kufanya usiku uwe mchana,Wakisema, ‘Bila shaka mwangaza unakaribia kwa sababu kuna giza.’ 13  Nikisubiri, Kaburi* litakuwa makao yangu;+Nitakitandaza kitanda changu gizani.+ 14  Nitaliambia shimo*+ kwa sauti, ‘Wewe ni baba yangu!’ Na mabuu, ‘Ninyi ni mama yangu na dada yangu!’ 15  Basi, tumaini langu liko wapi?+ Ni nani anayeweza kuona tumaini hilo? 16  Litashuka* kwenye malango ya Kaburi* yenye makomeoTutakaposhuka sote pamoja mavumbini.”+

Maelezo ya Chini

Au “kuendelea kuangalia.”
Tnn., “methali; msemo.”
Au “mwasi imani.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kaburi.”
Yaani, tumaini langu.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.