Ayubu 21:1-34

  • Ayubu ajibu (1-34)

    • ‘Kwa nini waovu wanafanikiwa?’ (7-13)

    • Afichua hila za “wafariji” wake (27-34)

21  Ayubu akajibu:   “Sikilizeni kwa makini ninayosema;Na hii iwe faraja mnayonipa.   Nivumilieni ninapozungumza;Nikimaliza kuzungumza, mnaweza kunidhihaki.+   Je, ninamlalamikia mwanadamu? Ikiwa ndivyo, je, nisingekosa* subira?   Niangalieni na kunikodolea macho kwa mshangao;Funikeni kinywa chenu kwa mkono wenu.   Ninapofikiria jambo hilo, nashikwa na wasiwasi,Na mwili wangu wote unatetemeka.   Kwa nini waovu wanaendelea kuishi,+Wanazeeka, na kutajirika?*+   Huwaona watoto wao sikuzote,Nao huendelea kuishi na kuwaona wazao wao.   Nyumba zao zina usalama, hawana hofu yoyote,+Na Mungu hawaadhibu kwa fimbo yake. 10  Ng’ombe dume wao hawashindwi kuzalisha;Ng’ombe wao huzaa na mimba haziharibiki. 11  Wavulana wao hukimbia nje kama kondoo,Na watoto wao hurukaruka huku na huku. 12  Wao huimba kwa tari na kinubiNa kushangilia wanaposikia sauti ya zumari.*+ 13  Huishi siku zao wakiwa wameridhikaNao hushuka kwa amani* Kaburini.* 14  Lakini wanamwambia Mungu wa kweli, ‘Tuache! Hatutamani kuzijua njia zako.+ 15  Mweza-Yote ni nani ili tumtumikie?+ Tutapata faida gani tukimfahamu?’+ 16  Lakini ninajua kwamba hawaudhibiti ufanisi wao wenyewe.+ Mawazo ya waovu yako mbali nami.*+ 17  Ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa?+ Ni mara ngapi wanapopatwa na msiba? Ni mara ngapi Mungu huwaangamiza kwa hasira yake? 18  Je, kuna wakati wowote wanapopeperushwa na upepo kama majani makavuNa kama makapi yanayopeperushwa mbali na upepo wa dhoruba? 19  Mungu atawawekea watoto wa mtu mwovu adhabu ya mtu huyo. Lakini Mungu na amlipe ili apate kujua hilo.+ 20  Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake,Na anywe mwenyewe ghadhabu ya Mweza-Yote.+ 21  Kwa maana, kwa nini ahangaikie kitakachoipata nyumba yake baada ya kifo chakeIkiwa idadi ya miezi yake imepunguzwa?*+ 22  Je, kuna yeyote anayeweza kumfundisha Mungu ujuzi,*+Wakati Yeye ndiye anayewahukumu hata walio juu zaidi?+ 23  Kuna mtu anayekufa akiwa na nguvu zake zote+Akiwa amestarehe kabisa na bila mahangaiko,+ 24  Wakati mapaja yake yamenenepa kwa mafutaNa mifupa yake ikiwa na nguvu.* 25  Lakini mtu mwingine hufa akiwa ametaabika sana,*Akiwa hajaonja kamwe vitu vyema. 26  Wote watalala mavumbini,+Na mabuu yatawafunika wote wawili.+ 27  Tazama! Ninajua vizuri mambo mnayofikiriaNa njama mnazopanga ili kunidhuru.*+ 28  Kwa maana mnasema, ‘Iko wapi nyumba ya yule mtu maarufu,Na liko wapi hema alimoishi yule mtu mwovu?’+ 29  Je, hamjawauliza wasafiri? Je, hamchunguzi kwa makini mambo waliyoona,* 30  Kwamba mtu mwovu huokolewa katika siku ya msibaNa kuokolewa katika siku ya ghadhabu? 31  Ni nani atakayemuuliza kuhusu njia yake,Na ni nani atakayemlipa kwa sababu ya mambo aliyotenda? 32  Anapopelekwa kaburini,Kaburi lake litalindwa. 33  Mabonge ya udongo wa bondeni* yatakuwa matamu kwake,+Na wanadamu wote humfuata*+Kama idadi isiyohesabika ya waliomtangulia. 34  Basi kwa nini mnipe faraja isiyo na maana?+ Majibu yenu hayana lolote isipokuwa udanganyifu!”

Maelezo ya Chini

Tnn., “roho yangu isingekosa.”
Au “kuwa na nguvu.”
Au “filimbi.”
Au “haraka,” yaani, wanakufa upesi bila maumivu.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Mashauri; Njama za waovu ziko mbali nami.”
Au “imegawanywa mara mbili.”
Au “kumfundisha Mungu jambo lolote.”
Tnn., “umajimaji ulio mifupani haujakauka.”
Au “akiwa na uchungu nafsini.”
Au labda, “ili kunitendea kikatili.”
Tnn., “ishara zao.”
Au “korongoni.”
Tnn., “Naye atawakokota wanadamu wote wamfuate.”