Ayubu 22:1-30

  • Elifazi azungumza kwa mara ya tatu (1-30)

    • ‘Mwanadamu ana faida gani kwa Mungu?’ (2, 3)

    • Adai kwamba Ayubu ni mwenye pupa na hatendi haki (9)

    • ‘Mrudie Mungu, utarudishiwa hali njema’ (23)

22  Elifazi+ Mtemani akajibu:   “Je, mwanadamu anaweza kuwa na faida kwa Mungu? Je, mtu yeyote mwenye ufahamu anaweza kuwa na faida kwake?+   Je, Mweza-Yote anajali* kwamba wewe ni mwadilifu,Au je, anapata faida yoyote kwa sababu unafuata njia ya utimilifu?+   Je, atakuadhibuNa kukushtaki kwa sababu unamheshimu?   Je, si kwa sababu uovu wako mwenyewe ni mkubwa sanaNa makosa yako hayana mwisho?+   Kwa maana unachukua dhamana kutoka kwa ndugu zako bila sababu,Nawe unawavua watu mavazi yao na kuwaacha uchi.*+   Humpi aliyechoka maji ya kunywa,Nawe unamnyima chakula mwenye njaa.+   Nchi ni ya mtu mwenye nguvu,+Na anayependelewa huishi ndani yake.   Lakini uliwafukuza wajane mikono mitupu,Nawe uliiponda mikono ya mayatima. 10  Ndiyo sababu umezungukwa na mitego,*+Na vitisho vya ghafla vinakuogopesha; 11  Ndiyo sababu kuna giza sana hivi kwamba huwezi kuona,Na mafuriko ya maji yamekufunika. 12  Je, Mungu hayuko katika vilele vya mbinguni? Na tazama jinsi nyota zote zilivyo juu sana. 13  Lakini umesema: ‘Kwa kweli Mungu anajua nini? Je, anaweza kuhukumu katika giza zito? 14  Mawingu humfunika hivi kwamba haoniAnapotembea huku na kule kwenye duara ya mbingu.’ 15  Je, utafuata kijia cha kaleAmbacho watu waovu wamefuata, 16  Watu ambao waliangamizwa* kabla ya wakati wao,Ambao msingi wao ulifagiliwa na mafuriko?*+ 17  Walikuwa wakimwambia Mungu wa kweli: ‘Achana nasi!’ Na ‘Mweza-Yote anaweza kutufanya nini?’ 18  Lakini, Yeye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vizuri. (Sina mawazo maovu kama hayo.) 19  Waadilifu wataona hilo na kushangilia,Na wasio na hatia watawadhihaki na kusema: 20  ‘Wapinzani wetu wameangamizwa,Na moto utateketeza mabaki yao.’ 21  Mjue Yeye, nawe utakuwa na amani;Kisha mambo mema yatakujia. 22  Kubali sheria inayotoka katika kinywa chake,Na uyaweke maneno yake moyoni mwako.+ 23  Ukimrudia Mweza-Yote, utarudishiwa hali njema;+Ukiondoa uovu katika hema lako, 24  Ukitupa dhahabu yako* mavumbiniNa dhahabu ya Ofiri+ kwenye miamba ya mabondeni,* 25  Ndipo Mweza-Yote atakapokuwa dhahabu yako,*Naye atakuwa fedha yako iliyo bora kabisa. 26  Kwa maana ndipo utakapopendezwa na Mweza-Yote,Nawe utauinua uso wako kumwelekea Mungu. 27  Utamsihi, naye atakusikiliza;Nawe utatimiza nadhiri zako. 28  Jambo lolote utakaloamua kufanya litafanikiwa,Na nuru itaangaza kwenye kijia chako. 29  Kwa maana utaaibishwa ukiongea kwa kiburi,Lakini atawaokoa wanyenyekevu.* 30  Atawaokoa watu wasio na hatia;Kwa hiyo ikiwa mikono yako ni safi, hakika utaokolewa.”

Maelezo ya Chini

Au “anafurahi.”
Tnn., “unawavua walio uchi mavazi yao.”
Tnn., “mitego ya ndege.”
Au “ambao maisha yao yalifupishwa.”
Tnn., “mto.”
Au “Ukivitupa vipande vyako vya dhahabu.”
Au “makorongoni.”
Au “vipande vyako vya dhahabu.”
Au “walio na macho yanayotazama chini.”