Ayubu 23:1-17

  • Ayubu ajibu (1-17)

    • Ataka kupeleka kesi yake mbele za Mungu (1-7)

    • Asema kwamba hampati Mungu (8, 9)

    • “Nimefuata njia yake bila kukengeuka” (11)

23  Ayubu akajibu:   “Hata leo nitalalamika kwa ukaidi;*+Nimeishiwa na nguvu kwa sababu ya kulia kwa uchungu.   Laiti ningejua mahali ninapoweza kumpata Mungu!+ Ningeenda mahali anapoishi.+   Ningepeleka kesi yangu mbele zakeNa kujaza hoja za kujitetea kinywani mwangu;   Ningefahamu jinsi ambavyo angenijibuNa kutilia maanani anayoniambia.   Je, angepambana nami kwa nguvu zake nyingi? Hapana, bila shaka angenisikiliza.+   Huko mtu mnyoofu angenyoosha mambo pamoja naye,Na Mwamuzi wangu angefutilia mbali mashtaka yangu milele.   Lakini nikienda mashariki, hayuko huko;Na nikirudi, simpati.   Anapofanya kazi upande wa kushoto, siwezi kumwona;Kisha anageuka upande wa kulia, lakini bado simwoni. 10  Lakini anajua kijia ninachofuata.+ Baada ya kunijaribu, nitatoka nikiwa kama dhahabu safi.+ 11  Miguu yangu imefuata nyayo zake kwa ukaribu;Nimefuata njia yake bila kukengeuka.+ 12  Sijaacha amri ya midomo yake. Nimeyathamini maneno yake+ kama hazina hata kuliko nilivyoamriwa.* 13  Anapokusudia, ni nani anayeweza kumpinga?+ Anapotaka kufanya jambo, yeye hulifanya.+ 14  Kwa maana atatenda kwa ukamili aliyokusudia* kwa ajili yangu,Naye ana mambo mengi kama hayo akibani. 15  Ndiyo sababu nina wasiwasi kwa sababu yake;Ninapomfikiria, hofu yangu inaongezeka. 16  Mungu amenifanya nihofu,Na Mweza-Yote amenitia woga. 17  Lakini bado sijanyamazishwa na gizaWala utusitusi uliofunika uso wangu.

Maelezo ya Chini

Au “lalamiko langu ni uasi.”
Au “nilivyoagizwa.”
Au “aliyoagiza.”