Ayubu 24:1-25

  • Ayubu aendelea kujibu (1-25)

    • ‘Kwa nini Mungu haweki wakati wa hukumu?’ (1)

    • Asema kwamba Mungu ameruhusu uovu (12)

    • Watenda dhambi wanapenda giza (13-17)

24  “Kwa nini Mweza-Yote haweki wakati wa hukumu?+ Kwa nini wale wanaomjua hawaioni siku yake?*   Watu husogeza alama za mipaka;+Wanaiba mifugo kwa ajili ya malisho yao.   Huwachukua punda wa mayatimaNa kumchukua ng’ombe dume wa mjane kuwa dhamana ya mkopo.*+   Huwasukuma maskini waondoke barabarani;Watu wasio na uwezo duniani hulazimika kujificha kwa sababu yao.+   Maskini hutafuta chakula kama punda mwitu+ nyikani;Huwatafutia watoto wao chakula jangwani.   Wanalazimika kuvuna shamba la mtu mwingine*Na kuokota masalio katika shamba la mizabibu la mwovu.   Wanalala uchi usiku, bila nguo;+Hawana cha kujifunika ili wasipigwe na baridi.   Wanaloweshwa na mvua za milimani;Wanashikilia miamba kwa nguvu kwa sababu hawana mahali pa kujificha.   Mtoto asiye na baba hunyakuliwa kutoka kwenye matiti ya mama yake;+Na mavazi ya maskini huchukuliwa kuwa dhamana ya mkopo,+ 10  Na kuwalazimisha kutembea uchi, bila nguo,Wakiwa na njaa, huku wakibeba masuke ya nafaka. 11  Hufanya kazi ngumu kwenye matuta yaliyo milimani katika joto la mchana;*Hukanyaga mashinikizo ya divai, lakini wanaona kiu.+ 12  Wanaokufa wanaendelea kulia kwa uchungu jijini;Waliojeruhiwa vibaya sana hulilia msaada,+Lakini Mungu haoni jambo hilo kuwa baya.* 13  Kuna wale wanaoasi nuru;+Hawatambui njia zake,Nao hawafuati vijia vyake. 14  Muuaji huamka wakati wa mapambazuko;Huwaua wasio na uwezo na maskini,+Naye huiba wakati wa usiku. 15  Macho ya mzinzi husubiri giza linapoingia,+Akisema, ‘Hakuna atakayeniona!’+ Naye huufunika uso wake. 16  Wakati wa giza wanavunja nyumba;Wakati wa mchana wanajifungia ndani. Wanaepuka nuru.+ 17  Kwa maana kwao, asubuhi ni kama giza zito;Wamezoea vitisho vya giza zito. 18  Lakini wanabebwa upesi na maji.* Fungu lao la ardhi litalaaniwa.+ Hawatarudi kwenye mashamba yao ya mizabibu. 19  Kama theluji iliyoyeyuka inavyokaushwa na ukame na joto,Ndivyo Kaburi* linavyowachukua waliotenda dhambi!+ 20  Mama yake atamsahau;* naye ataliwa na mabuu. Hatakumbukwa tena.+ Na uovu utakatwa kama mti. 21  Humwinda mwanamke tasa,Na kumtesa mjane. 22  Mungu atatumia nguvu zake kuwaangamiza wenye nguvu;Hata wakiinuka, hawana uhakika wa kuishi. 23  Mungu anawaacha wawe na uhakika na wajihisi salama,+Lakini macho yake yanatazama kila jambo wanalotenda.*+ 24  Wanakwezwa kwa muda mfupi, kisha wanatoweka.+ Wanashushwa chini+ na kukusanywa kama watu wengine wote;Wanakatwa kama masuke ya nafaka. 25  Sasa ni nani anayeweza kuthibitisha kwamba mimi ni mwongoAu kupinga neno langu?”

Maelezo ya Chini

Yaani, siku yake ya hukumu.
Au “rehani.”
Au labda, “kuvuna chakula cha mifugo shambani.”
Au labda, “Hukamua mafuta katikati ya kuta za matuta.”
Au labda, “Mungu hamhukumu yeyote kwa kutenda mabaya.”
Tnn., “Yeye ni mwepesi juu ya maji.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “Tumbo la uzazi litamsahau.”
Tnn., “njia zao.”