Ayubu 25:1-6

  • Bildadi azungumza kwa mara ya tatu (1-6)

    • ‘Mwanadamu anawezaje kuwa bila hatia mbele za Mungu?’ (4)

    • Adai kwamba utimilifu wa mwanadamu ni wa bure (5, 6)

25  Bildadi+ Mshua akajibu:   “Utawala na uwezo wenye kutisha ni wake;Yeye huimarisha amani mbinguni.*   Je, majeshi yake yanaweza kuhesabiwa? Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?   Basi mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu,+Au mtu aliyezaliwa na mwanamke anawezaje kuwa bila hatia?*+   Hata mwezi si mwangavuNa nyota si safi machoni pake,   Sembuse mwanadamu anayeweza kufa ambaye ni buu,Na binadamu ambaye ni mnyoo!”

Maelezo ya Chini

Tnn., “katika vilele vyake.”
Au “safi.”