Ayubu 29:1-25

  • Ayubu akumbuka maisha mazuri aliyokuwa nayo kabla ya mateso (1-25)

    • Aliheshimiwa kwenye lango la jiji (7-10)

    • Jinsi alivyokuwa akitenda haki awali (11-17)

    • Kila mtu alisikiliza ushauri wake (21-23)

29  Ayubu akaendelea kuzungumza:*   “Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa miezi ya zamani,Siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,   Alipoifanya taa yake iniangazie kichwani,Nilipotembea gizani kwa nuru yake,+   Nilipokuwa katika kilele cha mafanikio,Urafiki pamoja na Mungu ulipohisiwa katika hema langu,+   Mweza-Yote alipokuwa bado pamoja nami,Watoto* wangu wote waliponizunguka,   Nyayo zangu zilipoloweshwa katika siagi,Na miamba iliponimwagia vijito vya mafuta.+   Nilipokuwa nikienda kwenye lango la jiji+Na kuketi mahali pangu kwenye uwanja wa jiji,+   Vijana waliponiona walinipisha,*Na hata wazee waliinuka na kuendelea kusimama.+   Wakuu waliacha kuzungumza;Walifunika kinywa chao kwa mkono wao. 10  Sauti za watu maarufu zilinyamazishwa;Ulimi wao ulishikamana na kaakaa lao. 11  Yeyote aliyenisikia alinisifu,Na wale walioniona walinitetea. 12  Kwa maana nilimwokoa maskini aliyelilia msaada,+Pamoja na yatima na yeyote ambaye hakuwa na msaidizi.+ 13  Mtu aliyekaribia kuangamia alinibariki,+Nami niliufanya moyo wa mjane ushangilie.+ 14  Nilivaa uadilifu kama mavazi yangu;Haki yangu ilikuwa kama joho* na kilemba. 15  Nilikuwa macho kwa vipofuNa miguu kwa walemavu. 16  Nilikuwa baba ya maskini;+Nilichunguza kesi ya watu nisiowajua.+ 17  Nilivunja mataya ya mwovu+Na kuvuta mawindo kutoka katika meno yake. 18  Nilikuwa nikisema, ‘Nitafia nyumbani kwangu,*+Na siku zangu zitakuwa nyingi kama chembe za mchanga. 19  Mizizi yangu itaenea ndani ya maji,Na umande utakaa usiku kucha kwenye matawi yangu. 20  Utukufu wangu hufanywa kuwa mpya daima,Na upinde ulio mkononi mwangu utaendelea kupiga mishale.’ 21  Watu walisikiliza kwa hamu,Walingojea kimyakimya ushauri wangu.+ 22  Nilipomaliza kuongea, hawakuwa na la kuongezea;Maneno yangu yalipenya taratibu* masikioni mwao. 23  Waliningojea kama wanavyongojea mvua;Walifumbua vinywa vyao wazi kana kwamba wanangojea mvua ya masika.+ 24  Nilipotabasamu, hawakuamini;Nuru ya uso wangu iliwapa ujasiri.* 25  Niliwapa mwelekezo nikiwa kiongozi wao,Nami niliishi kama mfalme anayezungukwa na majeshi yake,+Kama mtu anayewafariji waombolezaji.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kutoa methali.”
Au “Watumishi.”
Tnn., “walijificha.”
Yaani, joho lisilo na mikono.
Tnn., “kwenye kiota changu.”
Tnn., “yalitonatona.”
Au labda, “Hawakuitia giza nuru ya uso wangu.”