Ayubu 31:1-40

  • Ayubu atetea utimilifu wake (1-40)

    • “Agano na macho yangu” (1)

    • Aomba Mungu ampime (6)

    • Hakuwa mzinzi (9-12)

    • Hakupenda pesa (24, 25)

    • Hakuabudu sanamu (26-28)

31  “Nimefanya agano na macho yangu.+ Basi ninawezaje kumtazama bikira kwa njia isiyofaa?+   Basi, nitapata fungu gani kutoka kwa Mungu aliye juu,Urithi gani kutoka kwa Mweza-Yote aliye juu?   Je, msiba haumngojei mkosajiNa maafa wale wanaofanya mambo yanayodhuru?+   Je, yeye haoni njia zangu+Na kuhesabu hatua zangu zote?   Je, nimewahi kutembea katika njia isiyo ya kweli?* Je, mguu wangu umekimbilia udanganyifu?+   Mungu na anipime kwa mizani sahihi;+Ndipo atakapotambua utimilifu wangu.+   Hatua zangu zikikengeuka kutoka kwenye njia+Au ikiwa moyo wangu umefuata macho yangu+Au ikiwa mikono yangu imechafuliwa,   Basi acha nipande mbegu na mtu mwingine ale,+Na acha mimea ninayopanda ing’olewe.*   Ikiwa moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke+Nami nimenyemelea+ katika mlango wa jirani yangu, 10  Basi acha mke wangu amsagie nafaka mwanamume mwingine,Na acha wanaume wengine wafanye ngono naye.*+ 11  Kwa maana hilo lingekuwa tendo la aibu,Kosa linalostahili adhabu kutoka kwa waamuzi.+ 12  Ungekuwa moto unaoteketeza na kuangamiza,*+Unaoteketeza hata mizizi ya* mazao yangu yote. 13  Ikiwa niliwanyima haki watumishi wangu wa kiume na wa kikeWalipokuwa na malalamiko* dhidi yangu, 14  Nitafanya nini Mungu akinikabili?* Nitamjibu nini akinifanya niwajibike?+ 15  Je, Yule aliyeniumba tumboni mwa mama yangu hakuwaumba wao pia?+ Je, si Ndiye aliyetuumba sisi kabla hatujazaliwa?*+ 16  Ikiwa nilikataa kuwapa maskini walichotamani+Au ikiwa niliyahuzunisha macho ya mjane;*+ 17  Ikiwa nilikula chakula changu peke yanguBila kuwagawia mayatima;+ 18  (Kwa maana tangu nilipokuwa kijana, nimemlea yatima kana kwamba mimi ni baba yake,Nami nimekuwa kiongozi wa mjane tangu utotoni.*) 19  Ikiwa nilimwona yeyote akiangamia kwa kukosa mavaziAu maskini asiye na chochote cha kujifunika;+ 20  Ikiwa hakunibariki*+Alipokuwa akijipasha joto kwa manyoya ya kondoo wangu; 21  Ikiwa nilitikisa ngumi yangu na kumtisha yatima+Alipohitaji msaada wangu kwenye lango la jiji;*+ 22  Basi acha mkono* wangu ung’oke kutoka begani mwangu,Na acha mkono wangu uvunjwe kwenye kiwiko* chake. 23  Kwa maana niliogopa sana msiba kutoka kwa Mungu,Nami sikuweza kustahimili adhama yake. 24  Ikiwa nilifanya dhahabu kuwa tumaini languAu kuiambia dhahabu bora, ‘Wewe ni mlinzi wangu!’+ 25  Ikiwa shangwe yangu ilikuwa utajiri wangu mwingi+Kwa sababu ya mali nyingi nilizokusanya;+ 26  Ikiwa niliona jua liking’aa*Au mwezi ukizunguka kwa fahari yake;+ 27  Na moyo wangu ukashawishiwa kwa siri,Na kinywa changu kikabusu mkono wangu nikiviabudu;+ 28  Basi hilo ni kosa linalostahili adhabu kutoka kwa waamuzi,Kwa maana nitakuwa nimemkana Mungu wa kweli aliye juu. 29  Je, nimewahi kushangilia kuangamizwa kwa adui yangu+Au kumcheka kwa sababu amepatwa na uovu? 30  Sikuruhusu kamwe kinywa changu kitende dhambiKwa kuapa kwamba afe.+ 31  Je, watu wa hema langu hawajauliza,‘Ni nani anayeweza kumpata mtu ambaye hajashibishwa na chakula chake?’*+ 32  Hakuna mgeni* aliyelazimika kulala nje usiku;+Nilimfungulia milango msafiri. 33  Je, nimewahi kujaribu kufunika dhambi zangu, kama watu wengine,+Kwa kuficha uovu wangu katika mfuko wa vazi langu? 34  Je, nimewahi kuogopa umati utakavyotenda,Au kutishwa na dharau za familia nyingine,Na hivyo kukaa kimya na kuogopa kutoka nje? 35  Laiti mtu fulani angenisikiliza!+ Ningeweka sahihi ya jina langu kwenye mambo niliyosema!* Mweza-Yote na anijibu!+ Laiti mshtaki wangu angeandika mashtaka yangu kwenye hati! 36  Ningeibebea begani mwangu,Nami ningeifunga kama taji kuzunguka kichwa changu. 37  Ningempa habari kuhusu kila hatua niliyopiga;Ningemfikia kwa ujasiri, kama kiongozi. 38  Ikiwa ardhi yangu mwenyewe ingetoa kilio dhidi yanguNa mitaro yake ingelia pamoja; 39  Ikiwa nimekula mazao yake bila kulipa,+Au ikiwa nimewakatisha tamaa wamiliki wake;+ 40  Basi miiba ichipuke kwa ajili yangu badala ya nganoNa magugu yenye harufu mbaya badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yanaishia hapa.

Maelezo ya Chini

Au labda, “na watu wasiopenda kweli?”
Au “acha wazao wangu wang’olewe.”
Tnn., “acha wanaume wengine wapige magoti juu yake.”
Tnn., “unaokula (unaonyafua) na kuangamiza.”
Au “Unaong’oa.”
Au “kesi.”
Tnn., “akiinuka?”
Tnn., “katika tumbo la uzazi.”
Tnn., “niliyadhoofisha macho ya mjane.”
Tnn., “tangu tumboni mwa mama yangu.”
Tnn., “Ikiwa kiuno chake hakikunibariki.”
Au labda, “Nilipoona kwamba nina watu wanaonisaidia katika lango la jiji.”
Au “mtulinga.”
Au “kwenye kiungio chake; kutoka kwenye mfupa wake wa juu.”
Tnn., “nuru iking’aa.”
Tnn., “nyama yake.”
Au “mkaaji mgeni.”
Au “Hii ndiyo sahihi yangu.”