Ayubu 32:1-22

  • Kijana Elihu ajiunga na mazungumzo (1-22)

    • Amkasirikia Ayubu na rafiki zake (2, 3)

    • Alisubiri kwa heshima kabla ya kuzungumza (6, 7)

    • Umri peke yake haumfanyi mtu awe na hekima (9)

    • Elihu atamani kuongea (18-20)

32  Basi wanaume hao watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alisadiki kwamba yeye ni mwadilifu.*+  Lakini Elihu mwana wa Barakeli, kutoka Buzi,+ wa ukoo wa Ramu, akakasirika sana. Hasira yake iliwaka dhidi ya Ayubu kwa sababu alijaribu kujithibitisha mwenyewe kuwa mwadilifu badala ya Mungu.+  Pia, aliwakasirikia vikali marafiki watatu wa Ayubu kwa sababu walishindwa kujibu lakini walikuwa wamemtangaza Mungu kuwa mwovu.+  Elihu alikuwa amesubiri kumjibu Ayubu, kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kuliko yeye.+  Elihu alipoona kwamba wanaume hao watatu hawakuwa na jambo la kusema, aliwaka hasira.  Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli, kutoka Buzi, akaanza kuzungumza, akasema: “Mimi ni kijana*Lakini ninyi ni wazee.+ Kwa hiyo kwa heshima nilijizuia,+Nami sikuthubutu kuwaambia ninayojua.   Niliwaza, ‘Acha umri uzungumze,*Na acha wingi wa miaka utangaze hekima.’   Lakini ni roho iliyo ndani ya watu,Pumzi ya Mweza-Yote, inayowapa uelewaji.+   Umri peke yake haumfanyi* mtu awe na hekima,Wala si wazee peke yao wanaoelewa yaliyo sawa.+ 10  Kwa hiyo ninasema, ‘Nisikilizeni,Nami pia nitawaambia ninayojua.’ 11  Tazameni! Nimesubiri maneno yenu;Niliendelea kusikiliza hoja zenu+Mlipokuwa mkitafuta mambo ya kusema.+ 12  Niliwasikiliza kwa makini,Lakini hakuna yeyote miongoni mwenu aliyeweza kuthibitisha kwamba Ayubu amekosea*Wala kujibu hoja zake. 13  Kwa hiyo msiseme, ‘Tumepata hekima;Mungu ndiye anayempinga, si mwanadamu.’ 14  Ayubu hakuelekeza maneno yake kwangu,Kwa hiyo sitamjibu kwa kutumia hoja zenu. 15  Wamefadhaika, hawana mambo zaidi ya kusema;Wameishiwa na maneno. 16  Nimesubiri, lakini hawaendelei kuzungumza;Wamesimama pale tu, hawana majibu zaidi. 17  Basi, mimi pia nitajibu;Mimi pia nitasema ninayojua, 18  Kwa maana nina mengi ya kusema;Roho iliyo ndani yangu inanishurutisha. 19  Matumbo yangu ni kama divai isiyo na mahali pa kutokea,Kama viriba vipya vya divai vinavyokaribia kupasuka.+ 20  Acha nizungumze ili nipate kitulizo! Nitafungua midomo yangu na kujibu. 21  Sitampendelea yeyote;+Wala kumsifusifu* mwanadamu yeyote, 22  Kwa maana sijui kusifusifu;Nikifanya hivyo, Muumba wangu ataniangamiza.

Maelezo ya Chini

Au “alijiona kuwa mwadilifu.”
Tnn., “Mimi ni mdogo wa siku.”
Tnn., “siku ziseme.”
Au “Siku nyingi peke yake hazimfanyi.”
Au “aliyeweza kumkaripia Ayubu.”
Au “kumpa jina la cheo.”