Ayubu 34:1-37

  • Elihu atetea haki ya Mungu na njia zake (1-37)

    • Ayubu asema kwamba Mungu alimnyima haki (5)

    • Mungu wa kweli hawezi kamwe kutenda uovu (10)

    • Ayubu hana ujuzi (35)

34  Kwa hiyo, Elihu akaendelea kusema:   “Sikilizeni maneno yangu, ninyi mlio na hekima;Nisikilizeni, ninyi mnaojua mambo mengi sana.   Kwa maana sikio hupima manenoKama ulimi unavyoonja* chakula.   Acheni tuchanganue wenyewe yaliyo sawa;Acheni tuamue miongoni mwetu yaliyo mema.   Kwa maana Ayubu amesema, ‘Sijakosea,+Lakini Mungu ameninyima haki.+   Je, ninaweza kusema uwongo kuhusu hukumu ninayostahili? Kidonda changu hakiponi, ingawa sina kosa.’+   Ni nani aliye kama Ayubu,Anayekunywa dharau kama maji?   Yeye ni rafiki ya watenda dhambiNaye hushirikiana na waovu.+   Kwa maana amesema, ‘Mwanadamu hafaidikiKwa kujitahidi kumpendeza Mungu.’+ 10  Kwa hiyo nisikilizeni, ninyi watu wenye uelewaji:* Mungu wa kweli hawezi kamwe kuwazia kutenda uovu,+Na Mweza-Yote hawezi kamwe kutenda kosa!+ 11  Kwa maana atamlipa mwanadamu kulingana na matendo yake+Na kumletea matokeo ya njia zake. 12  Kwa hakika, Mungu hatendi uovu;+Mweza-Yote hapotoshi haki.+ 13  Ni nani aliyempa mamlaka ya kusimamia dunia,Na ni nani aliyemweka asimamie ulimwengu mzima?* 14  Akiwakazia fikira,*Akijikusanyia roho yao na pumzi yao,+ 15  Wanadamu wote wataangamia* pamoja,Nao watarudi mavumbini.+ 16  Basi ikiwa mna uelewaji, sikilizeni mambo haya;Sikilizeni kwa makini ninayosema. 17  Je, mtu anayechukia haki anapaswa kuongoza,Au je, mtamhukumu mwenye nguvu ambaye ni mwadilifu? 18  Je, mtamwambia mfalme, ‘Wewe hufai kitu,’Au viongozi, ‘Ninyi ni waovu’?+ 19  Kuna Yule asiyewapendelea wakuuNa ambaye hawapendelei matajiri na kuwapuuza maskini,*+Kwa maana wote ni kazi ya mikono yake.+ 20  Wanaweza kufa ghafla,+ katikati ya usiku;+Wanatikisika kwa nguvu na kufa;Hata wenye nguvu huondolewa, lakini si kwa mikono ya wanadamu.+ 21  Kwa maana macho ya Mungu hutazama njia za mwanadamu,+Naye huziona hatua zake zote. 22  Hakuna giza wala kivuli kizitoAmbamo watenda maovu wanaweza kujificha.+ 23  Kwa maana Mungu hajaweka wakati hususa wa mwanadamu yeyoteKufika mbele zake ili ahukumiwe. 24  Huwapondaponda wenye nguvu bila kuhitaji kufanya uchunguziNa kuwaweka wengine mahali pao.+ 25  Kwa maana anajua wanayofanya;+Huwapindua wakati wa usiku, nao huangamizwa.+ 26  Huwapiga kwa sababu ya uovu wao,Mahali ambapo watu wote wanaweza kuona,+ 27  Kwa sababu wameacha kumfuata+Nao hawaheshimu yoyote kati ya njia zake;+ 28  Wanasababisha maskini wamlilie,Hivi kwamba anasikia kilio cha wasio na uwezo.+ 29  Mungu akikaa kimya, ni nani anayeweza kumshutumu? Akiuficha uso wake, ni nani anayeweza kumwona? Iwe ni kwa taifa au mtu mmoja, matokeo ni yaleyale, 30  Ili mtu anayemkataa Mungu* asitawale+Au kuwawekea wengine mitego. 31  Je, kuna yeyote anayeweza kumwambia Mungu,‘Nimeadhibiwa, ingawa sijafanya kosa lolote;+ 32  Nifundishe jambo ambalo nimeshindwa kuona;Ikiwa nimetenda kosa lolote, sitalirudia tena’? 33  Je, akuthawabishe kwa masharti yako wakati unakataa hukumu yake? Amua mwenyewe, si mimi. Basi niambie mambo unayojua vema. 34  Watu wenye uelewaji* wataniambia—Mtu yeyote mwenye hekima anayenisikiliza— 35  ‘Ayubu anazungumza bila ujuzi,+Na maneno yake hayana ufahamu.’ 36  Acha Ayubu ajaribiwe* kikamiliKwa sababu majibu yake ni kama ya watu waovu! 37  Anaongeza uasi kwenye dhambi yake;+Anapiga makofi kwa dharau mbele yetuNa kusema maneno mengi dhidi ya Mungu wa kweli!”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kaakaa linavyoonja.”
Tnn., “moyo.”
Au “dunia inayokaliwa.”
Tnn., “moyo wake.”
Tnn., “Miili yote itaangamia.”
Au “watu maarufu na kuwapuuza watu wa hali ya chini.”
Au “mwasi imani.”
Tnn., “moyo.”
Au labda, “Baba yangu, acha Ayubu ajaribiwe.”