Ayubu 35:1-16

  • Elihu ataja mawazo yasiyofaa ya Ayubu (1-16)

    • Ayubu asema yeye ni mwadilifu kuliko Mungu (2)

    • Mungu yuko juu sana, haathiriwi na dhambi (5, 6)

    • Ayubu anapaswa kumngojea Mungu (14)

35  Elihu akaendelea kusema:   “Je, unasadiki kabisa kwamba uko sahihi hivi kwamba unasema,‘Mimi ni mwadilifu kuliko Mungu’?+   Kwa maana unasema, ‘Hilo linakuhusuje?* Je, hali yangu ni bora kuliko kama ningetenda dhambi?’+   Nitakujibu weweNa rafiki zako+ walio pamoja nawe.   Tazama mbinguni uone,Yaangalie mawingu,+ ambayo yako mbali sana juu yako.   Ukitenda dhambi, unamuumizaje?+ Dhambi zako zikiongezeka, unamwathirije?+   Ukiwa mwadilifu, unampa nini;Anapokea nini kutoka kwako?+   Uovu wako unamwathiri tu mwanadamu kama wewe,Na uadilifu wako, binadamu.   Watu hulia kwa sauti wanapokandamizwa sana;Wanalia wapate kitulizo kutoka chini ya mamlaka ya* wenye nguvu.+ 10  Lakini hakuna anayeuliza, ‘Yuko wapi Mungu, Muumba wangu Mkuu,+Yule anayesababisha nyimbo ziimbwe usiku?’+ 11  Hutufundisha+ kuliko wanyama mwitu wa dunia,+Naye hutufanya tuwe na hekima kuliko ndege wa angani. 12  Watu hulia kwa sauti, lakini Yeye hajibu,+Kwa sababu ya kiburi cha waovu.+ 13  Kwa kweli Mungu hasikilizi kilio kisicho na maana;*+Mweza-Yote hakisikilizi. 14  Sembuse wewe unapolalamika kwamba humwoni!+ Kesi yako iko mbele zake, kwa hiyo unapaswa kumngojea kwa hamu.+ 15  Kwa maana hajakuadhibu kwa hasira;Wala hajakazia fikira maneno unayosema haraka-haraka bila kufikiri.+ 16  Ayubu hufumbua kinywa chake wazi kwa ubatili;Huongea maneno mengi bila ujuzi.”+

Maelezo ya Chini

Inaelekea anamwambia Mungu.
Tnn., “kutoka mkononi mwa.”
Au “hasikilizi uwongo.”