Ayubu 37:1-24

  • Nguvu za asili zinafunua ukuu wa Mungu (1-24)

    • Mungu anaweza kusimamisha shughuli za wanadamu (7)

    • ‘Tafakari kazi za Mungu zinazostaajabisha’ (14)

    • Wanadamu hawawezi kumwelewa Mungu (23)

    • Hakuna mwanadamu anayepaswa kufikiri kwamba ana hekima (24)

37  “Kwa sababu hiyo moyo wangu hupigapigaNa kuruka kutoka mahali pake.   Sikiliza kwa makini mrindimo wa sauti yakeNa mngurumo unaotoka kinywani mwake.   Huuachilia kwa ghafla chini ya mbingu zoteNa kuituma radi yake+ mpaka kwenye miisho ya dunia.   Kisha sauti ya mngurumo husikika;Hunguruma kwa sauti yenye fahari,+Naye haizuii radi sauti yake inaposikiwa.   Mungu hunguruma kwa sauti yake+ kwa njia inayostaajabisha;Hufanya mambo makuu ambayo hatuwezi kuelewa.+   Kwa maana huiambia theluji, ‘Anguka duniani,’+Na mvua kubwa, ‘Nyesha kwa nguvu.’+   Mungu husimamisha shughuli zote za wanadamu*Ili kila mwanadamu anayeweza kufa ajue kazi Yake.   Wanyama wa mwituni huingia katika mapango yaoNa kubaki katika makao yao.   Upepo wa dhoruba huvuma kutoka katika chumba chake,+Na baridi huletwa na pepo za kaskazini.+ 10  Kwa pumzi ya Mungu, barafu hutokea,+Na maji mengi huganda kabisa.+ 11  Naam, huyalemea mawingu kwa mvuke;Hutawanya radi yake+ mawinguni; 12  Huzunguka-zunguka anakoyaelekeza;Hutekeleza chochote anachoamuru+ juu ya dunia inayokaliwa.* 13  Iwe ni adhabu*+ au kwa ajili ya nchiAu kwa ajili ya upendo mshikamanifu, yeye husababisha yatendeke.+ 14  Sikiliza hili, Ayubu;Tulia na utafakari kwa makini kazi za Mungu zinazostaajabisha.+ 15  Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza* mawinguNa jinsi anavyosababisha radi imweke kutoka katika mawingu yake? 16  Je, unajua jinsi mawingu yanavyoelea?+ Hizi ni kazi zinazostaajabisha za Yule ambaye ni mkamilifu katika ujuzi.+ 17  Kwa nini mavazi yako yanapata jotoWakati dunia imetulia kwa sababu ya upepo wa kusini?+ 18  Je, waweza, pamoja naye, kuzitandaza* anga+Zilizo ngumu kama kioo cha chuma? 19  Tuambie tunalopaswa kumwambia;Hatuwezi kumjibu kwa sababu tuko gizani. 20  Je, anapaswa kuambiwa kwamba ninataka kuzungumza? Au kuna yeyote ambaye amesema jambo ambalo lazima ajulishwe?+ 21  Hata hawawezi kuona nuru,*Ingawa inang’aa angani,Mpaka upepo unapopita na kuondoa kabisa mawingu. 22  Fahari inayong’aa kama dhahabu hutoka kaskazini;Utukufu wa Mungu+ unaogopesha. 23  Hatuwezi kumwelewa Mweza-Yote;+Ana nguvu nyingi,+Na hapotoshi kamwe haki+ na uadilifu wake mwingi.+ 24  Kwa hiyo watu wanapaswa kumwogopa.+ Kwa sababu yeye hampendi yeyote anayefikiri ana hekima.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “huweka muhuri juu ya mkono wa kila mwanadamu.”
Au “ardhi inayozaa.”
Tnn., “fimbo.”
Au “anavyoyaamuru.”
Au “kuzikunjua.”
Yaani, ya jua.