Ayubu 38:1-41

  • Yehova afundisha kuhusu udogo wa mwanadamu (1-41)

    • ‘Ulikuwa wapi nilipoiumba dunia?’ (4-6)

    • Wana wa Mungu walishangilia kwa sauti (7)

    • Maswali kuhusu matukio ya asili (8-32)

    • “Sheria zinazoongoza mbingu” (33)

38  Kisha Yehova akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba ya upepo:+   “Ni nani huyu anayepotosha mashauri yanguNa kuzungumza bila ujuzi?+   Tafadhali, jitayarishe* kama mwanamume;Nitakuuliza maswali, nawe unijibu.   Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?+ Niambie, ikiwa unafikiri unaelewa.   Ni nani aliyeweka vipimo vyake, ikiwa unajua,Au ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?   Nguzo zake zilizamishwa ndani ya nini,Au ni nani aliyeweka jiwe lake la pembeni,+   Nyota za asubuhi+ zilipopaza kelele pamoja kwa shangwe,Na wana wote wa Mungu*+ wakaanza kushangilia kwa sauti?   Na ni nani aliyeizuia bahari nyuma ya milango+Ilipotoka kwa nguvu katika tumbo la uzazi,   Nilipoivalisha mawinguNa kuifunika kwa* giza zito, 10  Nilipoiwekea mpaka wanguNa kuweka makomeo yake na milango yake mahali pake,+ 11  Nami nikaiambia, ‘Unaweza kufika hapa, lakini usipite hapa;Hapa ndipo mawimbi yako ya kifahari yatakapokomea’?+ 12  Je, umewahi kuiamuru* asubuhiAu kuyafanya mapambazuko yajue mahali pake,+ 13  Ili yaenee mpaka kwenye miisho ya duniaNa kuwakung’uta waovu kutoka humo?+ 14  Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi utiwapo muhuri,Na vitu vilivyomo hung’aa kama mapambo ya vazi. 15  Lakini waovu hunyimwa nuru yao,Na mkono wao ulioinuliwa huvunjwa. 16  Je, umeshuka chini kwenye chemchemi za bahariAu kuchunguza vilindi vya maji?+ 17  Je, umeonyeshwa malango ya kifo,+Au umeona malango ya giza zito?*+ 18  Je, umeelewa upana mkubwa sana wa dunia?+ Niambie, ikiwa unajua haya yote. 19  Nuru hukaa upande gani?+ Na makao ya giza yako wapi, 20  Ili ulipeleke katika eneo lakeNa kuelewa vijia vinavyoelekea nyumbani kwake? 21  Je, unajua hayo kwa sababu ulikuwa tayari umezaliwaNa idadi ya miaka yako ni mingi?* 22  Je, umeingia kwenye maghala ya theluji,+Au umeyaona maghala ya mvua ya mawe,+ 23  Ambayo nimeyahifadhi kwa ajili ya wakati wa taabu,Kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?+ 24  Nuru* hutawanywa kutoka upande gani,Na upepo wa mashariki huvuma duniani kutoka wapi?+ 25  Ni nani amechimba mtaro kwa ajili ya mafurikoNa kutengeneza kijia kwa ajili ya mawingu ya dhoruba yenye ngurumo,+ 26  Na kuifanya mvua inyeshe mahali ambapo watu hawaishi,Nyikani ambako hakuna wanadamu,+ 27  Ili kutosheleza maeneo yaliyoharibiwa yenye ukiwaNa kufanya majani yachipuke?+ 28  Je, mvua ina baba,+Au ni nani baba ya matone ya umande?+ 29  Barafu ilitoka kwenye tumbo la uzazi la nani,Na ni nani aliyeizaa theluji ya mbinguni+ 30  Maji yanapofunikwa kana kwamba na jiwe,Na sehemu ya juu ya vilindi vya maji inapoganda kabisa?+ 31  Je, unaweza kufunga kamba za kundi la nyota la Kima*Au kufungua kamba za kundi la nyota la Kesili?*+ 32  Je, unaweza kuliongoza nje kundi la nyota* katika majira yakeAu kulielekeza kundi la nyota la Ashi* pamoja na wanawe? 33  Je, unajua sheria zinazoongoza mbingu,+Au unaweza kutumia mamlaka ya sheria hizo* duniani? 34  Je, unaweza kuinua sauti yako mpaka mawinguniIli kusababisha mafuriko ya maji yakufunike?+ 35  Je, unaweza kuutuma umeme wa radi? Je, utakuja na kukwambia, ‘Niko hapa!’? 36  Ni nani aliyeweka hekima mawinguni*+Au kuyapa uelewaji matukio ya angani?*+ 37  Ni nani aliye na hekima ya kutosha kuhesabu mawingu,Au ni nani anayeweza kuinamisha mitungi ya maji ya mbinguni+ 38  Mavumbi yanapomiminika na kugandamanaNa mabonge ya udongo yanaposhikamana? 39  Je, unaweza kumwindia simba mawindoAu kutosheleza hamu ya chakula ya wanasimba+ 40  Wanapojikunyata katika maficho yaoAu wanaponyemelea mapangoni mwao? 41  Ni nani anayemtayarishia chakula kunguru+Makinda wake wanapomlilia Mungu wakiomba msaadaNa kutangatanga kwa sababu hawana chakula?

Maelezo ya Chini

Tnn., “jifunge.”
Msemo wa Kiebrania unaorejelea malaika, wana wa Mungu.
Au “kuifungafunga katika.”
Tnn., “Je, katika siku zako umeiamuru.”
Au “kivuli cha kifo.”
Tnn., “Na idadi ya siku zako ni nyingi?”
Au labda, “Radi.”
Labda ni nyota zinazoitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, au Ng’ombe.
Labda ni kundi la nyota la Orioni.
Tnn., “Mazarothi.” Kwenye 2Fa 23:5, neno linalohusiana na hilo ambalo liko katika wingi linarejelea makundi ya nyota za unajimu.
Labda ni kundi la nyota la Dubu Mkubwa (Kundi Kubwa la Ursa).
Au labda, “mamlaka Yake.”
Au labda, “ndani ya mwanadamu.”
Au labda, “kuweka uelewaji akilini.”