Ayubu 42:1-17

  • Ayubu amjibu Yehova (1-6)

  • Rafiki watatu wa Ayubu washutumiwa (7-9)

  • Yehova ambariki tena Ayubu (10-17)

    • Wana na mabinti wa Ayubu (13-15)

42  Kisha Ayubu akamjibu Yehova:   “Sasa ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yoteNa kwamba hakuna jambo lolote unalokusudia lisilowezekana kwako.+   Ulisema, ‘Ni nani huyu anayepotosha mashauri yangu bila ujuzi?’+ Kwa hiyo nikazungumza, lakini sikuwa na uelewajiKuhusu mambo yanayonistaajabisha sana, ambayo siyajui.+   Ulisema, ‘Tafadhali sikiliza, nami nitaongea. Nitakuuliza maswali, nawe unijibu.’+   Masikio yangu yamesikia habari zako,Lakini sasa ninakuona kwa macho yangu.   Ndiyo sababu ninabatilisha* niliyosema,+Nami ninatubu katika mavumbi na majivu.”+  Baada ya Yehova kumwambia Ayubu maneno hayo, Yehova akamwambia Elifazi Mtemani: “Hasira yangu inawaka dhidi yako na rafiki zako wawili,+ kwa sababu hamkusema ukweli kunihusu+ kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.  Sasa chukueni ng’ombe dume saba na kondoo dume saba kisha mwende kwa mtumishi wangu Ayubu, na mtoe dhabihu ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Na mtumishi wangu Ayubu atasali kwa ajili yenu.+ Kwa hakika nitakubali ombi lake* nami sitawatendea kulingana na upumbavu wenu, kwa sababu hamkusema ukweli kunihusu kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.”  Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshua, na Sofari Mnaamathi wakaenda na kufanya kama Yehova alivyowaambia. Kisha Yehova akakubali sala ya Ayubu. 10  Baada ya Ayubu kusali kwa ajili ya rafiki zake,+ Yehova akamwondolea Ayubu dhiki+ na kumrudishia ufanisi wake.* Yehova akampa maradufu ya vitu alivyokuwa navyo awali.+ 11  Ndugu na dada zake wote pamoja na rafiki zake wote wa zamani+ wakaja kwake na kula pamoja naye nyumbani mwake. Wakampa pole na kumfariji kwa sababu ya mateso yote ambayo Yehova alikuwa ameruhusu yampate. Kila mmoja wao akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu. 12  Kwa hiyo, Yehova alibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ya kwanza,+ na Ayubu akawa na kondoo 14,000, ngamia 6,000, ng’ombe 2,000,* na punda jike 1,000.+ 13  Akapata pia wana wengine saba na mabinti wengine watatu.+ 14  Akamwita binti yake wa kwanza Yemima, wa pili Kezia, na wa tatu Kereni-hapuku. 15  Katika nchi yote hapakuwa na wanawake warembo kama mabinti wa Ayubu, na baba yao aliwapa urithi pamoja na ndugu zao. 16  Baada ya hayo Ayubu aliishi miaka 140, akawaona watoto wake na wajukuu wake—vizazi vinne. 17  Mwishowe Ayubu akafa, baada ya kuishi maisha marefu na yenye kuridhisha.*

Maelezo ya Chini

Au “ninafuta.”
Tnn., “Kwa hakika nitauinua uso wake.”
Tnn., “Yehova akaondoa utekwa wa Ayubu.”
Yaani, jozi 1,000 za ng’ombe.
Tnn., “akiwa amezeeka na akiwa amejaa siku.”