Ayubu 6:1-30

  • Jibu la Ayubu (1-30)

    • Adai kwamba ana sababu ya kulia (2-6)

    • Wafariji wake ni wenye hila (15-18)

    • “Maneno ya unyoofu hayaumizi!” (25)

6  Kisha Ayubu akajibu:  “Laiti maumivu yangu makali+ yangepimwa kikamiliNa kuwekwa kwenye mizani pamoja na msiba wangu!   Kwa maana sasa ni mazito kuliko mchanga wa bahari. Ndiyo sababu maneno yangu yamekuwa mazungumzo ya ovyoovyo.*+   Kwa maana mishale ya Mweza-Yote imenichoma,Na roho yangu inakunywa sumu yake;+Vitisho vya Mungu vinaniandama.   Je, punda mwitu+ atalia akiwa na majani,Au ng’ombe dume atalia akiwa na chakula?   Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi,Au maji ya mholi yana ladha?   Nimekataa kugusa vitu vya aina hiyo. Ni kama uchafu katika chakula changu.   Laiti ombi langu lingejibiwaNa laiti Mungu angenipa ninachotamani!   Kwamba Mungu angekuwa tayari kunipondaponda,Na kwamba angeunyoosha mkono wake na kuniangamiza!+ 10  Kwa maana hata hilo lingenifariji;Ningeruka kwa shangwe licha ya maumivu yangu yasiyokwisha,Kwa maana sijayakana maneno ya Aliye Mtakatifu.+ 11  Je, nina nguvu za kuendelea kungoja?+ Na ni mwisho gani unaonisubiri, hivi kwamba niendelee kuishi?* 12  Je, nguvu zangu ni kama za mwamba? Au mwili wangu umetengenezwa kwa shaba? 13  Je, kuna njia yoyote ninayoweza kujisaidia mwenyeweWakati nimenyang’anywa njia zangu zote za kujitegemeza? 14  Yeyote anayekataa kumtendea mwanadamu mwenzake kwa upendo mshikamanifu+Ataacha kumwogopa Mweza-Yote.+ 15  Ndugu zangu wenyewe wamekuwa na hila+ kama kijito cha majira ya baridi kali,Kama maji ya vijito vya majira ya baridi kali yanayokauka. 16  Vimekuwa vyeusi kwa sababu ya barafu,Na theluji inayoyeyuka imejificha ndani yake. 17  Lakini katika majira ya kiangazi vinakauka na kutoweka;Joto linapoongezeka, vinakauka. 18  Mikondo yake hugeuka;Navyo huelekea jangwani na kutoweka. 19  Misafara ya Tema+ huvitafuta;Wasafiri kutoka Sheba*+ huvingojea. 20  Wameaibika kwa sababu hawakupata walichotumaini;Wanafika hapo na kukata tamaa tu. 21  Hivyo ndivyo mlivyo kwangu mimi;+Mmeona mateso ya msiba wangu, nanyi mnaogopa.+ 22  Je, nimewaambia, ‘Nipeni kitu fulani,’Au kuwaomba zawadi yoyote kutoka katika mali zenu? 23  Je, nimeomba niokolewe kutoka mikononi mwa aduiAu niokolewe* kutoka kwa wakandamizaji? 24  Nifundisheni, nami nitanyamaza;+Nisaidieni kuelewa kosa langu. 25  Maneno ya unyoofu hayaumizi!+ Lakini karipio lenu lina faida gani?+ 26  Je, mnapanga njama ya kukosoa maneno yangu,Maneno ya mtu aliyekata tamaa,+ yanayopeperushwa mbali na upepo? 27  Ninyi hata mngeweza kupiga kura kwa ajili ya yatima+Na kumuuza rafiki yenu!*+ 28  Basi sasa geukeni mnitazame,Kwa maana siwezi kusema uwongo mbele yenu. 29  Fikirieni tena, tafadhali—msinielewe vibaya—Naam, fikirieni tena, kwa maana mimi bado ni mwadilifu. 30  Je, ulimi wangu unasema jambo lisilo la haki? Je, mdomo wangu hautambui* kwamba kuna jambo ambalo si sawa?

Maelezo ya Chini

Au “nimezungumza bila kufikiri; harakaharaka.”
Au “hivi kwamba nirefushe maisha yangu (nafsi yangu)?”
Au “Msafara wa Wasabea.”
Tnn., “nikombolewe.”
Au “kubadilishana rafiki yenu kwa mali.”
Tnn., “kaakaa langu halitambui.”