Ayubu 7:1-21

  • Ayubu aendelea kujibu (1-21)

    • Maisha ni kama kazi ya kulazimishwa (1, 2)

    • “Kwa nini umenifanya niwe shabaha yako?” (20)

7  “Je, maisha ya mwanadamu anayeweza kufa si kama kazi ya kulazimishwa,Na siku zake kama siku za kibarua?+   Kama mtumwa, anatamani sana kivuli,Na kama kibarua, anasubiri mshahara wake.+   Kwa hiyo nimepangiwa miezi ya ubatiliNami nimehesabiwa usiku baada ya usiku wa kuteseka.+   Ninapolala mimi huuliza, ‘Nitaamka wakati gani?’+ Lakini kadiri usiku unavyojikokota, ndivyo ninavyogaagaa hadi alfajiri.*   Mwili wangu umefunikwa na mabuu na magamba ya uchafu;+Ngozi yangu imejaa vigaga na usaha.+   Siku zangu zinasonga upesi sana kuliko gurudumu la mfumaji,+Nazo zinafikia mwisho bila tumaini.+   Kumbukeni kwamba maisha yangu ni upepo,+Kwamba jicho langu halitaona tena kamwe furaha.*   Jicho linaloniona sasa halitaniona tena;Macho yenu yatanitafuta, lakini nitakuwa nimeenda zangu.+   Kama wingu linalofifia na kutoweka,Mtu anayeshuka chini Kaburini* harudi juu tena.+ 10  Hatarudi tena katika nyumba yake,Na mahali pake hapatamtambua tena.+ 11  Kwa hiyo, sitazuia kinywa changu. Nitaongea kwa uchungu wa roho yangu;Nitalalamika katika mateso yangu makali!*+ 12  Je, mimi ni bahari au mnyama mkubwa sana wa baharini,Hivi kwamba uniwekee mlinzi? 13  Ninaposema, ‘Kochi langu litanifariji;Kitanda changu kitasaidia kupunguza mateso yangu,’ 14  Kisha unanitisha kwa ndotoNa kuniogopesha kwa maono, 15  Hivi kwamba natamani kusongwa pumzi,Naam, natamani kifo badala ya mwili huu wangu.*+ 16  Ninachukia maisha yangu;+ sitaki kuendelea kuishi. Niache, kwa maana siku zangu ni kama pumzi.+ 17  Mwanadamu anayeweza kufa ni nini hivi kwamba umhangaikieNa kumkazia uangalifu?*+ 18  Kwa nini unamkagua kila asubuhiNa kumjaribu kila wakati?+ 19  Je, hutaacha kunitazamaNa kuniacha peke yangu nipate muda wa kumeza mate?+ 20  Ikiwa nimetenda dhambi, ninawezaje kukudhuru wewe, Mchunguzaji wa wanadamu?+ Kwa nini umenifanya niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako? 21  Kwa nini husamehi dhambi yanguNa kuachilia kosa langu? Kwa maana hivi punde nitalala mavumbini,+Nawe utanitafuta, lakini nitakuwa nimeenda zangu.”

Maelezo ya Chini

Au “mpaka mapambazuko.”
Tnn., “mema.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kwa uchungu wa nafsi yangu!”
Tnn., “badala ya mifupa yangu.”
Tnn., “kuuweka moyo wako juu yake?”