Ayubu 8:1-22

  • Bildadi azungumza kwa mara ya kwanza (1-22)

    • Adai kwamba watoto wa Ayubu wametenda dhambi (4)

    • ‘Ikiwa ungekuwa safi, Mungu angekulinda’ (6)

    • Adai kwamba Ayubu amemkataa Mungu (13)

8  Kisha Bildadi+ Mshua+ akajibu:   “Utaendelea kuongea kwa njia hiyo mpaka lini?+ Maneno ya kinywa chako ni upepo wenye nguvu!   Je, Mungu atapotosha haki,Au, je, Mweza-Yote atapotosha uadilifu?   Ikiwa watoto wako walimtendea dhambi,Aliwaacha waadhibiwe kwa sababu ya uasi wao;*   Laiti ungemtumaini Mungu+Na kumsihi Mweza-Yote upate kibali chake,   Na ikiwa kwa kweli ungekuwa safi na mnyoofu,+Angekusikiliza*Na kukurudisha mahali unapostahili.   Na ingawa mwanzo wako ulikuwa mdogo,Wakati wako ujao utakuwa mkubwa.+   Tafadhali, uliza kizazi kilichotangulia,Na usikilize mambo ambayo baba zao walijifunza.+   Kwa maana tulizaliwa jana tu, nasi hatujui lolote,Kwa sababu siku zetu duniani ni kivuli. 10  Je, hawatakufundishaNa kukwambia wanayojua?* 11  Je, mafunjo yanaweza kusitawi katika eneo lisilo na umajimaji? Je, utete unaweza kusitawi bila maji? 12  Hata kabla haujachanua, kabla haujakatwa,Utakauka kabla ya mmea mwingine wowote. 13  Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa* wote wanaomsahau Mungu,Kwa maana tumaini la wanaomkataa Mungu* litapotea, 14  Ambao tegemeo lao ni ubatiliNa ambao tumaini lao ni hafifu kama utando wa* buibui. 15  Ataegemea nyumba yake, lakini haitaendelea kusimama;Atajaribu kuishikilia, lakini haitadumu. 16  Yeye ni mmea wenye unyevunyevu juani,Na matawi yake huenea shambani.+ 17  Mizizi yake husokotana katika rundo la mawe;Hutafuta nyumba katikati ya mawe.* 18  Lakini anapong’olewa* kutoka mahali pake,Mahali hapo patamkana na kusema, ‘Sijawahi kamwe kukuona.’+ 19  Naam, hivyo ndivyo atakavyotoweka;*+Kisha wengine watachipuka kutoka mavumbini. 20  Kwa hakika Mungu hatawakataa watu wanaoshika utimilifu;*Wala hatawaunga mkono* waovu, 21  Kwa maana bado atakijaza kinywa chako kichekoNa midomo yako kelele za shangwe. 22  Wale wanaokuchukia watavishwa aibu,Na hema la waovu halitakuwapo tena.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Aliwatia mikononi mwa uasi wao.”
Tnn., “Angeinuka kwa ajili yako.”
Tnn., “Na kusema maneno yaliyo mioyoni mwao?”
Tnn., “Hivyo ndivyo zilivyo njia za.”
Au “waasi imani.”
Tnn., “nyumba ya.”
Au “Hutazama nyumba ya mawe.”
Au “anapomezwa.”
Au “hivyo ndivyo njia yake itakavyoyeyuka.”
Au “wasio na lawama.”
Tnn., “hatawashika mkono.”