Ayubu 9:1-35

  • Jibu la Ayubu (1-35)

    • Mwanadamu anayeweza kufa hawezi kushindana na Mungu (2-4)

    • ‘Mungu hufanya mambo yasiyochunguzika’ (10)

    • Mtu hawezi kubishana na Mungu (32)

9  Ayubu akajibu:  “Kwa kweli ninajua hivyo ndivyo ilivyo. Lakini mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa mwadilifu katika kesi na Mungu?+   Mtu akitaka kubishana Naye,*+Mtu huyo hawezi kujibu hata swali moja kati ya maswali Yake elfu moja.   Yeye ni mwenye hekima moyoni na ana nguvu nyingi sana.+ Ni nani anayeweza kumpinga na asipate madhara?+   Yeye huihamisha* milima bila yeyote kujua;Huipindua kwa hasira yake.   Huitikisa dunia kutoka mahali pake,Hivi kwamba nguzo zake zinatetemeka.+   Huliamuru jua lisiangazeNaye huziba kabisa nuru ya nyota;+   Huzitandaza mbingu akiwa peke yake,+Naye hukanyaga mawimbi makubwa ya bahari.+   Aliumba kundi la nyota la Ashi,* Kesili,* na Kima,*+Na makundi ya nyota yaliyo katika anga la kusini;* 10  Hufanya mambo makuu yasiyochunguzika,+Mambo yenye kustaajabisha yasiyoweza kuhesabiwa.+ 11  Yeye hupita karibu nami, lakini siwezi kumwona;Hupita mbele yangu, lakini siwezi kumtambua. 12  Anapochukua kitu kwa ghafla, ni nani anayeweza kumzuia? Ni nani anayeweza kumuuliza, ‘Unafanya nini?’+ 13  Mungu hataizuia hasira yake;+Hata wanaomsaidia Rahabu*+ watamwinamia. 14  Sembuse ninapomjibuNi lazima nichague maneno yangu kwa uangalifu ili kujadiliana naye! 15  Hata kama singekuwa na kosa, singemjibu.+ Ningemsihi tu mwamuzi* wangu anionyeshe rehema. 16  Nikimwita, je, atanijibu? Siamini kwamba atasikiliza sauti yangu, 17  Kwa maana yeye huniponda kwa dhorubaNaye huzidisha majeraha yangu bila sababu.+ 18  Haniruhusu nipumue;Huendelea kunijaza mambo machungu. 19  Kama ni nguvu, yeye ndiye mwenye nguvu.+ Kama ni haki, anauliza: ‘Ni nani anayeweza kunishtaki?’* 20  Kama singekuwa na kosa, kinywa changu mwenyewe kingenishutumu;Hata nikishika utimilifu wangu,* atanitangaza kuwa mwenye hatia.* 21  Hata nikishika utimilifu wangu,* sijiamini;* Ninakataa* maisha haya yangu. 22  Yote ni sawa. Ndiyo sababu ninasema,‘Yeye huwaangamiza wasio na hatia* na waovu pia.’ 23  Mafuriko ya ghafla yakisababisha kifo ghafla,Ataidhihaki hali ya kukata tamaa ya watu wasio na hatia. 24  Dunia imetiwa mikononi mwa mwovu;+Huwafumba macho* waamuzi wake. Kama si yeye, ni nani basi? 25  Sasa siku zangu zinakimbia kasi kuliko mkimbiaji;+Zinakimbia na kutoweka bila kuona mema. 26  Zinanyiririka kama mashua za matete,Kama tai wanaoshuka kwa ghafla kukamata mawindo yao. 27  Nikisema, ‘Nitasahau malalamiko yangu,Nitabadili hali ya uso wangu na kuwa mchangamfu,’ 28  Bado nitaogopa kwa sababu ya maumivu yangu yote,+Nami najua hutanipata bila hatia. 29  Nitapatikana na hatia.* Basi kwa nini nitaabike bure?+ 30  Nikioga kwa maji ya theluji inayoyeyuka,Na kunawa mikono yangu kwa sabuni,*+ 31  Wewe utanitumbukiza shimoni,Hivi kwamba hata mavazi yangu mwenyewe yatanichukia. 32  Kwa maana yeye si mwanadamu kama mimi ili nimjibu,Hivi kwamba twende mahakamani pamoja.+ 33  Hakuna mtu wa kuamua kesi baina yetu wawili,*Anayeweza kuwa mwamuzi wetu.* 34  Ikiwa angeacha kunipiga*Na kuacha kuniogopesha kwa vitisho vyake,+ 35  Ndipo ningeongea naye bila woga,Kwa sababu sijazoea kuongea kwa woga.

Maelezo ya Chini

Au “kumpeleka mahakamani.”
Au “huiondoa.”
Labda ni kundi la nyota la Dubu Mkubwa (Kundi Kubwa la Ursa).
Tnn., “katika vyumba vya ndani vya kusini.”
Labda ni nyota zinazoitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, au Ng’ombe.
Labda ni kundi la nyota la Orioni.
Labda ni mnyama mkubwa sana wa baharini.
Au labda, “mshtaki.”
Tnn., “kunipeleka mahakamani?”
Au “Hata nikiwa bila hatia.”
Tnn., “atanitangaza kuwa mpotovu.”
Au “nikiwa bila hatia.”
Au “Siijui nafsi yangu.”
Au “Ninadharau.”
Au “watimilifu.”
Tnn., “nyuso.”
Tnn., “kuwa mwovu.”
Au “magadi.”
Au “kutupatanisha.”
Tnn., “kuweka mkono wake juu yetu wawili.”
Tnn., “angeondoa fimbo yake juu yangu.”