Danieli 4:1-37

  • Mfalme Nebukadneza atambua utawala wa Mungu (1-3)

  • Ndoto ya mfalme kuhusu mti (4-18)

    • Nyakati saba kupita baada ya mti kuangushwa (16)

    • Mungu ni Mtawala wa wanadamu (17)

  • Danieli aeleza maana ya ndoto (19-27)

  • Utimizo wa kwanza wamhusu mfalme (28-36)

    • Mfalme ashikwa na wazimu kwa nyakati saba (32, 33)

  • Mfalme amtukuza Mungu wa mbinguni (37)

4  “Mimi Mfalme Nebukadneza, nawaandikia watu wa makabila yote, mataifa, na lugha zote duniani: Amani yenu na iongezeke!  Ninafurahi kuwatangazia ishara na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Zaidi amenifanyia.  Jinsi ishara zake zilivyo kuu, na jinsi maajabu yake yalivyo yenye nguvu! Ufalme wake ni ufalme wa milele, na utawala wake unadumu kizazi hata kizazi.+  “Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nikistarehe nyumbani mwangu na kufurahia ufanisi katika jumba langu la kifalme.  Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono ya kichwa changu yalinitisha.+  Basi nikaagiza wanaume wote wenye hekima wa Babiloni waletwe mbele yangu ili wanieleze maana ya ndoto hiyo.+  “Wakati huo makuhani wachawi, watu wanaofanya mazingaombwe, Wakaldayo,* na wanajimu+ wakaja mbele yangu. Nilipowasimulia ndoto hiyo, walishindwa kunieleza maana yake.+  Mwishowe Danieli akaja mbele yangu, anayeitwa pia Belteshaza,+ jina la mungu wangu,+ na ambaye ana roho ya miungu mitakatifu,+ nami nikamwambia ndoto hiyo:  “‘Ee Belteshaza mkuu wa makuhani wachawi,+ ninajua vema kwamba roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako,+ na hakuna siri yoyote iliyo ngumu sana kwako.+ Basi nieleze maono niliyoona katika ndoto yangu na maana yake. 10  “‘Katika maono ya kichwa changu nilipokuwa kitandani mwangu, niliona mti+ katikati ya dunia, nao ulikuwa mrefu kwelikweli.+ 11  Mti huo ulikua na kuimarika, na kilele chake kikafika mbinguni, nao ulionekana hadi kwenye miisho ya dunia nzima. 12  Majani yake yalipendeza, na matunda yake yalikuwa mengi, nao ulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Wanyama wa mwituni walitafuta kivuli chini yake, na ndege wa angani walikaa kwenye matawi yake, na viumbe wote* walipata chakula kutoka katika mti huo. 13  “‘Nilipokuwa nikitazama maono ya kichwa changu nikiwa kitandani mwangu, nilimwona mlinzi, mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.+ 14  Akasema hivi kwa sauti kubwa: “Ukateni na kuuangusha mti huu,+ yakateni matawi yake, yapukutisheni majani yake, na kutawanya matunda yake! Wanyama na wakimbie kutoka chini yake, na ndege kutoka kwenye matawi yake. 15  Lakini kiacheni kisiki na mizizi yake ardhini kati ya majani ya shambani, kikiwa na pingu ya chuma na ya shaba. Acheni umande wa mbinguni ukiloweshe, na acheni fungu lake liwe pamoja na wanyama, kati ya majani ya dunia.+ 16  Moyo wake na ubadilishwe usiwe wa mwanadamu, nacho kipewe moyo wa mnyama, na acheni nyakati saba+ zipite.+ 17  Hilo ni kwa agizo la walinzi,+ na ombi hilo ni kwa neno la watakatifu, ili watu walio hai wajue kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu+ na kwamba yeye humpa ufalme huo yeyote anayetaka kumpa, naye humweka juu ya ufalme huo hata mwanadamu wa hali ya chini zaidi.” 18  “‘Hiyo ndiyo ndoto ambayo mimi, Mfalme Nebukadneza, niliota; sasa, Ee Belteshaza, nieleze maana ya ndoto hiyo, kwa maana wanaume wengine wote wenye hekima katika ufalme wangu wameshindwa kunieleza maana yake.+ Lakini wewe unaweza kufanya hivyo, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.’ 19  “Wakati huo Danieli, anayeitwa Belteshaza, akaduwaa kwa muda, na mawazo yake yakaanza kumtisha. “Mfalme akasema, ‘Ee Belteshaza,+ usiruhusu ndoto hii na maana yake ikutishe.’ “Belteshaza akamwambia, ‘Ee bwana wangu, ndoto hii na iwahusu wale wanaokuchukia, na maana ya ndoto hiyo itimie kwa maadui wako. 20  “‘Mti ulioona ambao ulikua mpaka ukawa mkubwa na kuimarika, ambao kilele chake kilifika mbinguni na ambao ulionekana duniani pote,+ 21  uliokuwa na majani yanayopendeza, matunda mengi, na chakula kwa ajili ya wote, na ambao chini yake wanyama wa mwituni waliishi na ndege wa angani kukaa kwenye matawi yake,+ 22  ni wewe, Ee mfalme, kwa sababu umekuwa mkuu na umeimarika, na utukufu wako umeongezeka na kufika mbinguni,+ na utawala wako kwenye miisho ya dunia.+ 23  “‘Wewe mfalme ulimwona mlinzi, mtakatifu,+ akishuka kutoka mbinguni, aliyekuwa akisema: “Ukateni na kuuangusha chini mti huu na kuuharibu, lakini kiacheni kisiki na mizizi yake ardhini kikiwa na pingu ya chuma na ya shaba, katikati ya majani ya shambani. Na acheni umande wa mbinguni ukiloweshe, na acheni fungu lake liwe pamoja na wanyama wa mwituni mpaka nyakati saba zipite.”+ 24  Ee mfalme, hii ndiyo maana yake; ni agizo la Aliye Juu Zaidi ambalo lazima litimie kwako bwana wangu mfalme. 25  Utafukuzwa mbali kutoka miongoni mwa wanadamu, utaishi na wanyama wa mwituni, nawe utapewa majani ule kama ng’ombe dume; na utalowa kwa umande wa mbinguni,+ na nyakati saba+ zitapita,+ mpaka utakapojua kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu na kwamba yeye humpa ufalme huo yeyote anayetaka kumpa.+ 26  “‘Lakini kwa sababu walisema kisiki cha mti huo kiachwe pamoja na mizizi yake,+ utarudishiwa tena ufalme wako baada ya kujua kwamba mbingu zinatawala. 27  Kwa hiyo, Ee mfalme, shauri langu na likubalike kwako. Geuka uziache dhambi zako kwa kutenda yaliyo sawa, na uache uovu wako kwa kuwaonyesha maskini rehema. Huenda muda wa ufanisi wako ukarefushwa.’”+ 28  Hayo yote yalimpata Mfalme Nebukadneza. 29  Miezi kumi na miwili baadaye alikuwa akitembea kwenye paa la jumba lake la kifalme la Babiloni. 30  Mfalme alikuwa akisema: “Je, hii si Babiloni Kubwa ambayo nimeijenga mimi mwenyewe kuwa makao ya kifalme kwa nguvu zangu mwenyewe na uwezo wangu na kwa ajili ya utukufu wa ukuu wangu?” 31  Mfalme alipokuwa akiendelea kusema maneno hayo, sauti ikasema hivi kutoka mbinguni: “Unaambiwa hivi, Ee Mfalme Nebukadneza, ‘Ufalme umekuponyoka,+ 32  nawe unafukuzwa mbali kutoka kati ya wanadamu. Utaishi na wanyama wa mwituni, nawe utapewa majani ule kama ng’ombe dume, na nyakati saba zitapita, mpaka utakapojua kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu na yeye humpa ufalme huo yeyote anayetaka kumpa.’”+ 33  Papo hapo, maneno hayo yakatimia kwa Nebukadneza. Akafukuzwa mbali kutoka kati ya wanadamu, akaanza kula majani kama ng’ombe dume, na mwili wake ukalowa kwa umande wa mbinguni, mpaka nywele zake zikawa ndefu kama manyoya ya tai na kucha zake zikawa kama kucha za ndege.+ 34  “Mwishoni mwa kipindi hicho,+ mimi, Nebukadneza, nilitazama juu mbinguni, na ufahamu wangu ukanirudia; nami nikamsifu Aliye Juu Zaidi, nikamsifu na kumtukuza Yeye anayeishi milele, kwa sababu utawala wake ni utawala wa milele na ufalme wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+ 35  Wakaaji wote wa dunia wanaonwa kuwa si kitu, naye hufanya kulingana na mapenzi yake mwenyewe miongoni mwa jeshi la mbinguni na wakaaji wa dunia. Na hakuna yeyote anayeweza kumzuia*+ au kumuuliza, ‘Umefanya nini?’+ 36  “Wakati huo ufahamu wangu ukanirudia, nami nikarudiwa na utukufu wa ufalme wangu, ukuu wangu, na fahari yangu.+ Maofisa wangu wakuu na watu mashuhuri walinitafuta kwa bidii, nami nikarudishwa kwenye ufalme wangu, na hata nikaongezewa ukuu mwingi zaidi. 37  “Sasa mimi, Nebukadneza, ninamsifu na kumkweza na kumtukuza Mfalme wa mbinguni,+ kwa sababu kazi zake zote ni kweli na njia zake ni haki,+ na kwa sababu anaweza kuwaaibisha wale wanaotembea katika kiburi.”+

Maelezo ya Chini

Yaani, wabashiri na wanajimu hodari.
Tnn., “wote wenye mwili.”
Au “kuuzuia mkono wake.”