Esta 2:1-23

  • Malkia mpya atafutwa (1-14)

  • Esta awa malkia (15-20)

  • Mordekai afunua njama (21-23)

2  Baada ya mambo hayo, hasira kali ya Mfalme Ahasuero+ ilipopungua, akakumbuka kosa la Vashti+ na uamuzi uliofanywa kumhusu.+  Ndipo wahudumu binafsi wa mfalme wakasema: “Mfalme atafutiwe wasichana warembo mabikira.  Na mfalme ateue wajumbe katika mikoa yote ya* milki yake+ ili wawakusanye pamoja na kuwaleta wasichana wote warembo walio mabikira kwenye nyumba ya wanawake* katika ngome ya* Shushani.* Watatunzwa na Hegai+ towashi wa mfalme aliye mlinzi wa wanawake, nao watarembeshwa.*  Msichana atakayependwa zaidi na mfalme atakuwa malkia badala ya Vashti.”+ Na pendekezo hilo likamfurahisha mfalme, naye akafanya hivyo.  Kulikuwa na mwanamume fulani Myahudi aliyeishi katika ngome ya* Shushani;*+ aliitwa Mordekai+ mwana wa Yairi mwana wa Shimei mwana wa Kishi, Mbenjamini,+  aliyekuwa miongoni mwa watu waliopelekwa uhamishoni kutoka Yerusalemu pamoja na Mfalme Yekonia*+ wa Yuda, ambaye Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alimpeleka uhamishoni.  Alikuwa mlezi* wa Hadasa,* yaani, Esta binti ya ndugu ya baba yake,+ kwa maana Esta hakuwa na baba wala mama. Msichana huyo alikuwa mrembo na mwenye umbo zuri, na baba na mama yake walipokufa, Mordekai alimchukua na kumlea kama binti yake.  Amri na sheria ya mfalme ilipotangazwa na wasichana wengi kukusanywa kwenye ngome ya* Shushani* chini ya utunzaji wa Hegai,+ Esta pia alipelekwa kwenye nyumba ya* mfalme chini ya utunzaji wa Hegai mlinzi wa wanawake.  Basi msichana huyo alimpendeza Hegai na kupata upendeleo wake,* basi Hegai akapanga mara moja arembeshwe*+ na kupewa chakula cha pekee, pia akampa wasichana saba waliochaguliwa kutoka kwa nyumba ya mfalme. Vilevile akamhamisha Esta na wale wasichana na kuwapeleka mahali bora zaidi katika nyumba hiyo ya wanawake.* 10  Esta hakusema lolote kuhusu watu wake+ wala watu wake wa ukoo, kwa maana Mordekai+ alikuwa amemwagiza asimwambie yeyote.+ 11  Siku baada ya siku Mordekai alikuwa akipita mbele ya ua wa nyumba ya wanawake* ili ajue hali ya Esta na mambo yaliyokuwa yakimpata. 12  Kila msichana alikuwa na zamu ya kwenda mbele ya Mfalme Ahasuero baada ya kurembeshwa kwa kipindi cha miezi 12 walichopangiwa wanawake, kwa maana huo ndio uliokuwa utaratibu wa kurembeshwa*—miezi sita kwa mafuta ya manemane+ na miezi sita kwa mafuta ya zeri+ na mafuta mbalimbali ya urembo.* 13  Kisha msichana angekuwa tayari kwenda mbele ya mfalme, naye alipewa chochote alichoomba alipoondoka katika nyumba ya wanawake* kwenda kwenye nyumba ya mfalme. 14  Msichana angeingia kwa mfalme jioni, na asubuhi angerudi kwenye nyumba ya pili ya wanawake* iliyosimamiwa na Shaashgazi, towashi wa mfalme,+ mlinzi wa masuria. Hangerudi kwa mfalme tena isipokuwa iwe mfalme alipendezwa naye kwa njia ya pekee na kumwita kwa jina.+ 15  Ilipofika zamu yake ya kuingia kwa mfalme, Esta binti ya Abihaili ndugu ya baba ya Mordekai, aliyemchukua na kumlea kama binti yake,+ hakuomba chochote ila vitu alivyopendekeza Hegai towashi wa mfalme, aliyekuwa mlinzi wa wanawake. (Wakati wote huo kila mtu aliyemwona Esta alipendezwa naye.) 16  Esta akapelekwa kwa Mfalme Ahasuero katika nyumba yake ya kifalme mwezi wa kumi, yaani, mwezi wa Tebethi* katika mwaka wa saba+ wa utawala wake. 17  Naye mfalme akampenda Esta kuliko wale wanawake wengine wote, akapata upendeleo na kibali* machoni pa mfalme kuliko wale mabikira wengine wote. Basi akamvika taji la* malkia na kumfanya kuwa malkia+ badala ya Vashti.+ 18  Naye mfalme akaandaa karamu kubwa kwa ajili ya wakuu wake wote na watumishi wake wote, karamu ya Esta. Kisha akatangaza msamaha kwa mikoa,* naye akatoa zawadi kulingana na mali ya mfalme. 19  Sasa mabikira*+ walipokusanywa mara ya pili, Mordekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme. 20  Esta hakusema lolote kuhusu watu wake wa ukoo na watu wa taifa lake,+ kama Mordekai alivyokuwa amemwagiza; Esta aliendelea kutii maneno ya Mordekai, kama alivyofanya alipokuwa akimlea.+ 21  Siku hizo Mordekai alipokuwa akiketi katika lango la mfalme, Bigthani na Tereshi, maofisa wawili wa makao ya mfalme, walinzi wa milango, walikasirika na kupanga njama ya kumuua Mfalme Ahasuero. 22  Lakini Mordekai akajua jambo hilo, na mara moja akamwambia Malkia Esta. Naye Esta akazungumza na mfalme kwa jina la* Mordekai. 23  Basi jambo hilo likachunguzwa na mwishowe likathibitishwa, na wale wanaume wawili wakatundikwa mtini; na mambo hayo yote yakaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati mbele ya mfalme.+

Maelezo ya Chini

Au “wilaya zote za utawala za.”
Au “nyumba ya harimu.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “watakandwa.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Anaitwa Yehoyakini kwenye 2Fal 24:8.
Au “mtunzaji.”
Maana yake “Mhadasi.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “jumba la.”
Au “katika nyumba ya harimu.”
Au “akandwe.”
Au “upendo wake mshikamanifu.”
Au “nyumba ya harimu.”
Au “kukandwa.”
Au “na kukandwa kwa wanawake.”
Au “nyumba ya harimu.”
Au “nyumba ya pili ya harimu.”
Au “upendo mshikamanifu.”
Au “kilemba cha.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “wasichana.”
Au “kwa niaba ya.”