Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitabu cha Ezekieli

Sura

Muhtasari wa Yaliyomo

  • 1

    • Ezekieli aona maono ya Mungu akiwa Babiloni (1-3)

    • Maono ya gari la kimbingu la Yehova (4-28)

      • Dhoruba, wingu, na moto (4)

      • Viumbe hai wanne (5-14)

      • Magurudumu manne (15-21)

      • Anga linalometameta kama barafu (22-24)

      • Kiti cha ufalme cha Yehova (25-28)

  • 2

    • Ezekieli apewa kazi ya kuwa nabii (1-10)

      • ‘Iwe watasikiliza au hawatasikiliza’ (5)

      • Aonyeshwa kitabu cha kukunjwa chenye nyimbo za huzuni (9, 10)

  • 3

    • Ezekieli aambiwa ale kitabu cha kukunjwa alichopewa na Mungu (1-15)

    • Ezekieli atakuwa mlinzi (16-27)

      • Kupuuza kunasababisha hatia ya damu (18-21)

  • 4

    • Aonyesha jinsi Yerusalemu litakavyozingirwa (1-17)

      • Abeba hatia kwa siku 390 na siku 40 (4-7)

  • 5

    • Aonyesha jinsi Yerusalemu litakavyoanguka (1-17)

      • Nywele za nabii zilizonyolewa zagawanywa katika mafungu matatu (1-4)

      • Yerusalemu lina uovu kuliko mataifa (7-9)

      • Waasi waadhibiwa kwa njia tatu (12)

  • 6

    • Dhidi ya milima ya Israeli (1-14)

      • Sanamu zinazochukiza zitafedheheshwa (4-6)

      • “Mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova” (7)

  • 7

    • Mwisho umefika (1-27)

      • Msiba wa pekee (5)

      • Pesa zatupwa barabarani (19)

      • Hekalu litatiwa unajisi (22)

  • 8

    • Ezekieli apelekwa Yerusalemu katika maono (1-4)

    • Vitu vinavyochukiza vyaonekana hekaluni (5-18)

      • Wanawake wakimlilia Tamuzi (14)

      • Wanaume wakiabudu jua (16)

  • 9

    • Wanaume sita wanaoangamiza na mwanamume mwenye kidau cha wino (1-11)

      • Hukumu itaanzia patakatifu (6)

  • 10

    • Moto wachukuliwa kutoka kati ya magurudumu (1-8)

    • Ufafanuzi kuhusu makerubi na magurudumu (9-17)

    • Utukufu wa Mungu waondoka hekaluni (18-22)

  • 11

    • Wakuu waovu washutumiwa (1-13)

      • Jiji lafananishwa na chungu cha kupikia (3-12)

    • Ahadi ya kurudishwa (14-21)

      • Wapewa “roho mpya” (19)

    • Utukufu wa Yehova waondoka Yerusalemu (22, 23)

    • Ezekieli arudi Ukaldayo katika maono (24, 25)

  • 12

    • Atabiri uhamisho kwa mifano (1-20)

      • Mizigo ya kwenda uhamishoni (1-7)

      • Mkuu ataondoka kukiwa na giza (8-16)

      • Mkate wa wasiwasi, maji ya hofu (17-20)

    • Msemo wa udanganyifu wathibitika kuwa uwongo (21-28)

      • “Hakuna neno langu lolote litakalokawia” (28)

  • 13

    • Dhidi ya manabii wa uwongo (1-16)

      • Kuta zilizopakwa chokaa zitaanguka (10-12)

    • Dhidi ya manabii wa kike wa uwongo (17-23)

  • 14

    • Wanaoabudu sanamu washutumiwa (1-11)

    • Hukumu dhidi ya Yerusalemu haiwezi kuepukika (12-23)

      • Noa, Danieli, na Ayubu waliokuwa waadilifu (14, 20)

  • 15

    • Yerusalemu, mzabibu usiofaa (1-8)

  • 16

    • Upendo wa Mungu kwa Yerusalemu (1-63)

      • Apatikana kama mtoto aliyeachwa (1-7)

      • Mungu ampamba na kufanya agano la ndoa pamoja naye (8-14)

      • Akosa kuwa mwaminifu (15-34)

      • Aadhibiwa kama mwanamke mzinzi (35-43)

      • Alinganishwa na Samaria na Sodoma (44-58)

      • Mungu akumbuka agano lake (59-63)

  • 17

    • Kitendawili cha tai wawili na mzabibu (1-21)

    • Chipukizi changa litakuwa mwerezi mkubwa (22-24)

  • 18

    • Kila mtu anawajibika kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe (1-32)

      • Nafsi inayotenda dhambi itakufa (4)

      • Mwana hatalipia dhambi ya baba yake (19, 20)

      • Sifurahishwi na kifo cha mtu mwovu (23)

      • Toba huhifadhi uhai (27, 28)

  • 19

    • Wimbo wa huzuni kwa ajili ya wakuu wa Israeli (1-14)

  • 20

    • Historia ya uasi wa Waisraeli (1-32)

    • Ahadi ya kurudishwa kwa Waisraeli (33-44)

    • Unabii dhidi ya kusini (45-49)

  • 21

    • Upanga wa hukumu wa Mungu wachomolewa (1-17)

    • Mfalme wa Babiloni kushambulia Yerusalemu (18-24)

    • Mkuu mwovu wa Israeli ataondolewa (25-27)

      • “Ulivue taji” (26)

      • “Mpaka yule aliye na haki ya kisheria atakapokuja” (27)

    • Upanga utawashambulia Waamoni (28-32)

  • 22

    • Yerusalemu, jiji lenye hatia ya damu (1-16)

    • Waisraeli ni kama takataka isiyo na thamani (17-22)

    • Viongozi na watu wa Israeli washutumiwa (23-31)

  • 23

    • Dada wawili ambao si waaminifu (1-49)

      • Ohola na Ashuru (5-10)

      • Oholiba na Babiloni na Misri (11-35)

      • Kuadhibiwa kwa dada wawili (36-49)

  • 24

    • Yerusalemu kama chungu cha kupikia chenye kutu (1-14)

    • Kifo cha mke wa Ezekieli ni ishara (15-27)

  • 25

    • Unabii dhidi ya Amoni (1-7)

    • Unabii dhidi ya Moabu (8-11)

    • Unabii dhidi ya Edomu (12-14)

    • Unabii dhidi ya Ufilisti (15-17)

  • 26

    • Unabii dhidi ya Tiro (1-21)

      • “Uwanja wa kukaushia nyavu za kukokotwa” (5, 14)

      • Mawe na udongo vyatupwa ndani ya maji (12)

  • 27

    • Wimbo wa huzuni kuhusu meli inayozama ya Tiro (1-36)

  • 28

    • Unabii dhidi ya mfalme wa Tiro (1-10)

      • “Mimi ni mungu” (2, 9)

    • Wimbo wa huzuni kuhusu mfalme wa Tiro (11-19)

      • “Ulikuwa katika Edeni” (13)

      • “Kerubi anayefunika aliyetiwa mafuta” (14)

      • ‘Uovu ulipatikana ndani yako’ (15)

    • Unabii dhidi ya Sidoni (20-24)

    • Israeli watarudishwa (25, 26)

  • 29

    • Unabii dhidi ya Farao (1-16)

    • Jiji la Babiloni litapewa Misri kama malipo (17-21)

  • 30

    • Unabii dhidi ya Misri (1-19)

      • Shambulizi la Nebukadneza latabiriwa (10)

    • Nguvu za Farao zavunjwa (20-26)

  • 31

    • Kuanguka kwa Misri, mwerezi mrefu (1-18)

  • 32

    • Wimbo wa huzuni kuhusu Farao na Misri (1-16)

    • Misri kuzikwa pamoja na wasiotahiriwa (17-32)

  • 33

    • Majukumu ya mlinzi (1-20)

    • Habari kuhusu kuanguka kwa Yerusalemu (21, 22)

    • Ujumbe kwa wakaaji wa magofu ya Yerusalemu (23-29)

    • Watu wapuuza ujumbe (30-33)

      • Ezekieli “kama wimbo wa mapenzi” (32)

      • “Nabii alikuwa miongoni mwao” (33)

  • 34

    • Unabii dhidi ya wachungaji wa Israeli (1-10)

    • Jinsi Yehova anavyowatunza kondoo wake (11-31)

      • “Mtumishi wangu Daudi” atawachunga (23)

      • “Agano la amani” (25)

  • 35

    • Unabii dhidi ya milima ya Seiri (1-15)

  • 36

    • Unabii kuhusu milima ya Israeli (1-15)

    • Kurudishwa kwa Waisraeli (16-38)

      • “Nitalitakasa jina langu kuu” (23)

      • “Kama bustani ya Edeni” (35)

  • 37

    • Maono ya bonde la mifupa mikavu (1-14)

    • Vijiti viwili vitaunganishwa pamoja (15-28)

      • Taifa moja chini ya mfalme mmoja (22)

      • Agano la kudumu la amani (26)

  • 38

    • Gogu kushambulia Israeli (1-16)

    • Hasira ya Yehova dhidi ya Gogu (17-23)

      • ‘Mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova’ (23)

  • 39

    • Kuangamizwa kwa Gogu na vikosi vyake (1-10)

    • Mazishi katika Bonde la Hamoni-Gogu (11-20)

    • Kurudishwa kwa Waisraeli (21-29)

      • Roho ya Mungu yamiminwa juu ya Waisraeli (29)

  • 40

    • Ezekieli aletwa Israeli katika maono (1, 2)

    • Ezekieli aona hekalu kwenye maono (3, 4)

    • Nyua na malango (5-47)

      • Lango la nje la mashariki (6-16)

      • Ua wa nje; malango mengine (17-26)

      • Ua wa ndani na malango (27-37)

      • Vyumba vya utumishi wa hekaluni (38-46)

      • Madhabahu (47)

    • Ukumbi wa hekalu (48, 49)

  • 41

    • Patakatifu pa hekalu (1-4)

    • Ukuta na vyumba vya kando (5-11)

    • Jengo la magharibi (12)

    • Majengo yapimwa (13-15a)

    • Sehemu ya ndani ya patakatifu (15b-26)

  • 42

    • Majengo ya vyumba vya kulia chakula (1-14)

    • Pande nne za hekalu zapimwa (15-20)

  • 43

    • Utukufu wa Yehova wajaa hekaluni (1-12)

    • Madhabahu (13-27)

  • 44

    • Lango la mashariki kubaki likiwa limefungwa (1-3)

    • Maagizo kuhusu wageni (4-9)

    • Maagizo kwa ajili ya Walawi na makuhani (10-31)

  • 45

    • Mchango mtakatifu na jiji (1-6)

    • Sehemu ya kiongozi (7, 8)

    • Viongozi watatenda kwa unyoofu (9-12)

    • Michango ya watu na ya kiongozi (13-25)

  • 46

    • Matoleo ya pindi mbalimbali (1-15)

    • Kurithi mali ya kiongozi (16-18)

    • Sehemu za kuchemshia dhabihu (19-24)

  • 47

    • Kijito kinachotiririka kutoka hekaluni (1-12)

      • Kina cha maji chaongezeka hatua kwa hatua (2-5)

      • Maji ya Bahari ya Chumvi yaponywa (8-10)

      • Sehemu zenye majimaji haziponywi (11)

      • Miti kwa ajili ya chakula na kuponya (12)

    • Mipaka ya nchi (13-23)

  • 48

    • Kuigawa nchi (1-29)

    • Malango 12 ya jiji (30-35)

      • Jiji linaloitwa “Yehova Yupo Hapo” (35)