Ezekieli 10:1-22

  • Moto wachukuliwa kutoka kati ya magurudumu (1-8)

  • Ufafanuzi kuhusu makerubi na magurudumu (9-17)

  • Utukufu wa Mungu waondoka hekaluni (18-22)

10  Nilipokuwa nikitazama, niliona juu ya anga lililokuwa juu ya vichwa vya makerubi kitu kama jiwe la yakuti kikitokea juu yao, nacho kilifanana na kiti cha ufalme.+  Kisha akamwambia yule mwanamume aliyevaa kitani:+ “Ingia katikati ya magurudumu yanayozunguka,+ chini ya makerubi, na ujaze mikono yako miwili makaa yanayowaka+ kutoka katikati ya makerubi na kuyarusha juu ya jiji.”+ Basi akaingia huku nikitazama.  Makerubi walikuwa wamesimama upande wa kulia wa ile nyumba mwanamume huyo alipoingia, nalo wingu likajaa katika ua wa ndani.  Na utukufu wa Yehova+ ukainuka kutoka kwa makerubi mpaka kwenye kizingiti cha mlango wa nyumba hiyo, na hatua kwa hatua nyumba hiyo ikajaa wingu,+ na ua ulikuwa umejaa mwangaza wa utukufu wa Yehova.  Na sauti ya mabawa ya makerubi ilisikika katika ua wa nje, kama sauti ya Mungu Mweza-Yote anapozungumza.+  Kisha akamwamuru hivi yule mwanamume aliyevaa kitani: “Chukua moto kutoka katikati ya magurudumu yanayozunguka, kutoka katikati ya makerubi,” naye akaingia na kusimama kando ya gurudumu.  Kisha mmoja wa makerubi akaunyoosha mkono wake kuelekea moto uliokuwa katikati ya makerubi.+ Akachukua kiasi fulani na kukiweka kwenye mikono miwili ya yule aliyevaa kitani,+ naye akauchukua na kwenda nje.  Makerubi walikuwa na kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao.+  Nilipokuwa nikitazama, niliona magurudumu manne kando ya makerubi, gurudumu moja kando ya kila kerubi, na magurudumu hayo yalionekana yaking’aa kama jiwe la krisolito.+ 10  Kuhusu mwonekano wake, yote manne yalifanana, yalionekana kama gurudumu moja likiwa katikati ya gurudumu lingine. 11  Yaliposonga, yaliweza kwenda upande wowote kati ya zile pande nne bila kugeuka, kwa maana yalikuwa yakienda upande ambao kichwa kilitazama nayo yalienda bila kugeuka. 12  Miili yao yote, migongo yao, mikono yao, mabawa yao, na yale magurudumu, magurudumu ya wote wanne, yalijaa macho kila mahali.+ 13  Kuhusu yale magurudumu, nilisikia sauti ikiyaita, “Magurudumu yanayozunguka!” 14  Kila mmoja wao* alikuwa na nyuso nne. Uso wa kwanza ulikuwa uso wa kerubi, uso wa pili ulikuwa uso wa mwanadamu, wa tatu ulikuwa uso wa simba, na wa nne ulikuwa uso wa tai.+ 15  Na wale makerubi walikuwa wakiinuka—walikuwa viumbe hai walewale niliowaona* kwenye mto Kebari+ 16  na wale makerubi waliposonga, magurudumu yalikuwa yakisonga kando yao; na wale makerubi walipoinua juu mabawa yao ili yawe juu sana ya dunia, magurudumu hayo hayakuwa yakigeuka au kuondoka kando yao.+ 17  Waliposimama tuli, nayo yalisimama tuli; nao walipoinuka, yaliinuka pamoja nao, kwa maana roho iliyokuwa ikitenda katika wale viumbe hai* ilikuwa ndani ya magurudumu. 18  Kisha utukufu wa Yehova+ ukaondoka kwenye kizingiti cha mlango wa nyumba na kusimama tuli juu ya makerubi.+ 19  Sasa makerubi wakainua juu mabawa yao na kuinuka kutoka duniani huku nikitazama. Yale magurudumu pia yalikuwa kando yao walipoondoka. Wakasimama katika kizingiti cha lango la mashariki la nyumba ya Yehova, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.+ 20  Hao ndio viumbe hai niliokuwa* nimeona chini ya Mungu wa Israeli kwenye mto Kebari,+ basi nikajua kwamba walikuwa makerubi. 21  Wote wanne walikuwa na nyuso nne, mabawa manne, na kitu kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao.+ 22  Na nyuso zao zilikuwa kama nyuso nilizokuwa nimeona kando ya mto Kebari.+ Kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja.+

Maelezo ya Chini

Yaani, kila kerubi.
Tnn., “kilikuwa kile kiumbe hai nilichoona.”
Tnn., “roho ya yule kiumbe hai.”
Tnn., “Huyu ndiye kiumbe hai niliyekuwa.”