Ezekieli 15:1-8

  • Yerusalemu, mzabibu usiofaa (1-8)

15  Neno la Yehova likanijia tena likisema:  “Mwana wa binadamu, mbao za mzabibu hutofautianaje na za mti mwingine wowote au tawi la miti ya msituni?  Je, ufito wake unaweza kutumiwa kufanyia kazi? Au je, watu huutumia kutengeneza kijiti cha kuning’inizia vyombo?  Tazama! Hutupwa motoni uwe kuni, na moto huchoma miisho yote miwili na kuunguza katikati. Je, sasa unafaa kwa kazi yoyote?  Hata ulipokuwa mzima, haungetumiwa kwa chochote. Je, utakuwa na thamani yoyote baada ya kuchomwa na kuunguzwa na moto?”  “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kama mbao za mzabibu kati ya miti ya msituni, ambazo nimezitoa ziwe kuni kwa ajili ya moto, ndivyo nitakavyoshughulika na wakaaji wa Yerusalemu.+  Nimewakataa.* Wameponyoka kutoka motoni, lakini moto utawateketeza. Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowakataa.’”*+  “‘Nami nitaifanya nchi iwe ukiwa+ kwa sababu wametenda kwa ukosefu wa uaminifu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nimeukaza uso wangu dhidi yao.”
Tnn., “nitakapoukaza uso wangu dhidi yao.”