Ezekieli 19:1-14

  • Wimbo wa huzuni kwa ajili ya wakuu wa Israeli (1-14)

19  “Nawe lazima uimbe wimbo wa huzuni* kuhusu wakuu wa Israeli,  useme, ‘Mama yako alikuwa nani? Simba jike kati ya simba. Alilala kati ya wanasimba wenye nguvu* naye akawalea watoto wake.   Alimlea mmoja wa watoto wake, akawa mwanasimba mwenye nguvu.+ Naye akajifunza jinsi ya kurarua mawindo, Akamnyafua hata mwanadamu.   Mataifa yalisikia kumhusu na wakamkamata katika shimo lao, Nao wakamleta kwa kulabu nchini Misri.+   Mama huyo alisubiri na hatimaye akaona hakuna tumaini kwamba atarudi. Basi akamchukua mwingine kati ya watoto wake na kumtuma akiwa mwanasimba mwenye nguvu.   Yeye pia alitembea huku na huku kati ya simba, naye akawa mwanasimba mwenye nguvu. Akajifunza jinsi ya kurarua mawindo, na hata akawanyafua wanadamu.+   Akazungukazunguka katika minara yao yenye ngome na kuyaharibu majiji yao, Hivi kwamba nchi iliyo ukiwa ikajaa sauti ya mngurumo wake.+   Mataifa ya wilaya jirani yalikuja dhidi yake ili kuutandaza wavu wao juu yake, Naye akanaswa katika shimo lao.   Wakamweka katika kizimba kwa kulabu na kumpeleka kwa mfalme wa Babiloni. Wakamfunga huko ili sauti yake isisikike tena kwenye milima ya Israeli. 10  Mama yako alikuwa kama mzabibu+ katika damu yako,* uliopandwa kando ya maji. Ukazaa matunda na kujaa matawi kwa sababu ya maji mengi. 11  Nao ukatokeza matawi yenye nguvu,* yanayofaa kuwa fimbo za ufalme za watawala. Ukakua, ukawa mrefu kuliko miti mingine, Nao ukaonekana kwa sababu ya urefu wake na wingi wa majani yake. 12  Lakini aling’olewa kwa ghadhabu+ na kutupwa chini ardhini, Na upepo wa mashariki ukayakausha matunda yake. Matawi yake yenye nguvu yalikatwa yakakauka,+ na moto ukayateketeza.+ 13  Sasa amepandwa nyikani, Katika nchi isiyo na maji na yenye kiu.+ 14  Moto ukaenea kutoka kwenye matawi yake* na kuteketeza machipukizi yake na matunda yake, Na hakuna tawi lenye nguvu lililobaki, hakuna fimbo ya mfalme ya kutawala.+ “‘Huo ni wimbo wa huzuni, nao utatumiwa kama wimbo wa huzuni.’”

Maelezo ya Chini

Au “wimbo wa maombolezo.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au labda, “kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu.”
Au “fimbo zenye nguvu.”
Au “fimbo zake.”