Ezekieli 2:1-10

  • Ezekieli apewa kazi ya kuwa nabii (1-10)

    • ‘Iwe watasikiliza au hawatasikiliza’ (5)

    • Aonyeshwa kitabu cha kukunjwa chenye nyimbo za huzuni (9, 10)

2  Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu,* simama kwa miguu yako ili nizungumze nawe.”+  Alipozungumza nami, roho ikaingia ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu+ ili niweze kumsikia Yule anayezungumza nami.  Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, ninakutuma kwa watu wa Israeli,+ kwa mataifa yenye kuasi ambayo yameniasi.+ Wao na mababu zao wamenikosea mpaka leo hii.+  Ninakutuma kwa wana wakaidi* na wenye moyo mgumu,+ nawe lazima uwaambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyosema.’  Nao, iwe watasikiliza au watakataa kusikiliza—kwa maana wao ni nyumba ya uasi+—watajua kwa hakika kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.+  “Lakini wewe, mwana wa binadamu, usiwaogope,+ na usiogope maneno yao, ingawa umezungukwa na michongoma na miiba*+ na unakaa katikati ya nge. Usiogope maneno yao+ na usitishwe na nyuso zao,+ kwa maana wao ni nyumba ya uasi.  Ni lazima uwaambie maneno yangu, iwe watasikiliza au la, kwa maana wao ni waasi.+  “Lakini wewe, mwana wa binadamu, sikiliza ninalokuambia. Usiwe mwasi kama nyumba hii ya uasi. Fungua kinywa chako ule ninachokupa.”+  Nilipotazama, niliona mkono ulionyooshwa kunielekea,+ na katika mkono huo niliona kitabu cha kukunjwa kilichoandikwa.+ 10  Alipokikunjua mbele yangu, kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma.+ Nyimbo za huzuni na maombolezo na vilio vilikuwa vimeandikwa kwenye kitabu hicho.+

Maelezo ya Chini

“Mwana wa binadamu”; maneno haya yanapatikana mara 93 katika Ezekieli na hapa ndipo yanapopatikana kwa mara ya kwanza.
Au “wenye uso mgumu.”
Au labda, “ingawa watu ni wakaidi, nao ni kama vitu vinavyokudunga.”