Ezekieli 24:1-27

  • Yerusalemu kama chungu cha kupikia chenye kutu (1-14)

  • Kifo cha mke wa Ezekieli ni ishara (15-27)

24  Neno la Yehova likanijia tena katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi huo, likisema:  “Mwana wa binadamu, andika tarehe hii,* siku hiihii ya leo. Mfalme wa Babiloni ameanza kulishambulia Yerusalemu siku hiihii ya leo.+  Na useme methali* kuhusu nyumba ya uasi, sema hivi kuwahusu: “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Weka motoni chungu cha kupikia;* kiweke motoni na utie maji ndani yake.+   Weka vipande vya nyama ndani yake,+ kila kipande kizuri, Paja na bega; kijaze kwa mifupa bora zaidi.   Chukua kondoo bora zaidi katika kundi,+ na urundike kuni chini ya chungu kuzunguka pande zote. Chemsha vipande hivyo, na upike mifupa iliyo ndani yake.’”   “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ole wake jiji la umwagaji wa damu,+ chungu cha kupikia chenye kutu, ambacho kutu yake haijaondolewa! Toeni nyama ndani yake, kipande kwa kipande;+ msizipigie kura.   Kwa maana damu yake imo ndani yake;+ aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi. Hakuimwaga ardhini, ili kuifunika kwa mavumbi.+   Ili kuchochea ghadhabu ya kulipiza kisasi, Nimeiweka damu yake juu ya mwamba ulio wazi, unaong’aa Ili isifunikwe.’+  “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ole wake jiji linalomwaga damu!+ Nitarundika rundo kubwa la kuni. 10  Rundika kuni na uwashe moto, Chemsha nyama kabisa, umwage mchuzi mzito, na uiache mifupa iungue. 11  Kiweke chungu kisicho na kitu kwenye makaa ili kiwe moto Ili shaba yake iwe moto kabisa. Uchafu wake utayeyuka ndani yake,+ na kutu yake itateketezwa. 12  Ni jambo linalokatisha tamaa na kuchosha, Kwa maana kutu yake nyingi haitatoka.+ Kitupeni motoni pamoja na kutu yake!’ 13  “‘Uchafu wako ulisababishwa na mwenendo wako mchafu.+ Nilijaribu kukusafisha lakini hungeweza kuwa safi kutokana na uchafu wako. Hutakuwa safi mpaka ghadhabu yangu dhidi yako itakapotulia.+ 14  Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema. Itatendeka. Nitatenda bila kujizuia, bila huruma, bila kughairi.+ Watakuhukumu kulingana na njia zako na matendo yako,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” 15  Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 16  “Mwana wa binadamu, kwa pigo moja niko karibu kumwondoa mpenzi wako kutoka kwako.+ Hupaswi kuomboleza;* wala hupaswi kulia wala kutokwa na machozi. 17  Lia kimyakimya kwa maumivu, wala usifanye desturi za kuwaombolezea waliokufa.+ Jifunge kilemba chako,+ na uvae viatu vyako.+ Hupaswi kufunika masharubu yako,*+ na usile mkate ulioletewa na watu wengine.”*+ 18  Nami nikazungumza na watu asubuhi, na mke wangu akafa jioni. Basi asubuhi nikafanya kama nilivyoamriwa. 19  Watu walikuwa wakiniuliza: “Je, hutatuambia jinsi mambo haya unayofanya yanavyotuhusu?” 20  Nikawajibu: “Neno la Yehova limenijia likisema, 21  ‘Waambie watu wa nyumba ya Israeli, “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko karibu kupatia unajisi mahali pangu patakatifu,+ chanzo cha fahari yenu kubwa, kitu mnachokipenda sana na tamaa ya moyo wenu.* Wana na mabinti wenu mliowaacha watauawa kwa upanga.+ 22  Nanyi mtalazimika kufanya kama nilivyofanya. Hamtafunika masharubu yenu, nanyi hamtakula mkate mlioletewa na watu wengine.+ 23  Vilemba vyenu vitakuwa kwenye vichwa vyenu na viatu vyenu kwenye miguu yenu. Hamtaomboleza wala kulia. Badala yake mtaoza katika makosa yenu,+ na kila mmoja wenu atamlilia mwenzake kwa maumivu. 24  Ezekieli amekuwa ishara kwenu.+ Mtatenda kama alivyotenda. Jambo hilo litakapotukia, mtalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’”’” 25  “Nawe, mwana wa binadamu, siku nitakapoondoa ngome yao kutoka kwao—kitu maridadi kinachowaletea shangwe, kitu wanachokipenda sana, tamaa ya moyo wao*—pamoja na wana wao na mabinti wao,+ 26  utajulishwa jambo hilo na yule aliyeponyoka.+ 27  Siku hiyo utafungua kinywa chako na kuzungumza na yule aliyeponyoka, nawe hutakuwa tena bubu.+ Utakuwa ishara kwao, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “jina la siku.”
Au “istiari.”
Au “chungu cha kupikia chenye mdomo mpana.”
Au “kukipigapiga kifua chako.”
Au “mdomo wako wa juu.”
Tnn., “mkate wa wanadamu.”
Au “kitu ambacho nafsi yenu inakihurumia.”
Au “nafsi zao.”