Ezekieli 29:1-21

  • Jiji la Babiloni litapewa Misri kama malipo (17-21)

29  Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya 12 ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema:  “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwa Farao mfalme wa Misri, na utabiri dhidi yake na dhidi ya nchi yote ya Misri.+  Sema maneno haya: ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Niko dhidi yako, Farao mfalme wa Misri,+ Mnyama mkubwa sana wa baharini anayelala kati ya vijito vya mto wake Nile,*+ Ambaye amesema, ‘Mto wangu Nile ni wangu. Niliutengeneza kwa ajili yangu.’+   Lakini nitatia kulabu katika mataya yako na kufanya samaki wa mto wako Nile washikamane na magamba yako. Nitakutoa katika mto wako Nile pamoja na samaki wa mto wako Nile wanaoshikamana na magamba yako.   Nitakuacha jangwani, wewe na samaki wote wa mto wako Nile. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa wala kuokotwa.+ Nitakufanya uwe chakula cha wanyama wa mwituni wa dunia na ndege wa angani.+   Ndipo wakaaji wote wa Misri watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, Kwa sababu kwa watu wa nyumba ya Israeli walikuwa kama unyasi* tu, hawakuwategemeza.+   Walipokushika mkono, ulipondwa, Nawe ukafanya wavunjike bega. Walipojitegemeza kwako, ulivunjika, Nawe ukafanya miguu yao ipepesuke.”*+  “‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ninaleta upanga ukushambulie,+ nami nitamwangamiza mwanadamu na mnyama kutoka ndani yako.  Nchi ya Misri itakuwa ukiwa na mahali palipoharibiwa;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, kwa maana umesema,* ‘Mto Nile ni wangu; mimi ndiye niliyeutengeneza.’+ 10  Basi niko dhidi yako na dhidi ya mto wako Nile, nami nitaifanya nchi ya Misri iwe mahali palipoharibiwa na palipokauka, mahame na ukiwa,+ kutoka Migdoli+ hadi Siene+ hadi kwenye mpaka wa Ethiopia. 11  Hakuna mwanadamu wala mnyama wa kufugwa atakayepitia humo kwa miguu,+ nayo haitakaliwa kwa miaka 40. 12  Nitaifanya nchi ya Misri iwe nchi yenye ukiwa kuliko nchi zote, na majiji yake yatakuwa majiji yenye ukiwa kuliko majiji yote kwa miaka 40;+ nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali.”+ 13  “‘Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Baada ya miaka 40 nitawakusanya Wamisri kutoka katika mataifa ambako walitawanywa;+ 14  Wamisri waliotekwa nitawarudisha katika nchi ya Pathrosi,+ katika nchi waliyozaliwa, na huko watakuwa ufalme duni. 15  Misri itakuwa chini kuliko zile falme nyingine nayo haitayatawala tena yale mataifa mengine,+ nitawafanya wawe wadogo sana hivi kwamba hawataweza kuyatiisha mataifa mengine.+ 16  Nchi ya Misri haitakuwa tena tegemeo kwa watu wa nyumba ya Israeli,+ bali itawakumbusha tu kosa walilofanya kwa kutafuta msaada kutoka kwa Wamisri. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’” 17  Sasa katika mwaka wa 27, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema: 18  “Mwana wa binadamu, Mfalme Nebukadneza*+ wa Babiloni aliamuru jeshi lake lifanye kazi kubwa ya kushambulia Tiro.+ Kila kichwa kilitiwa upara, na kila bega lilisuguliwa na kuchubuka ngozi. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kwa ajili ya kazi kubwa aliyofanya ya kuishambulia Tiro. 19  “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninampa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni nchi ya Misri,+ naye atabeba utajiri wake na kuchukua nyara kwa wingi na kuipora; na vitu hivyo vitakuwa malipo ya jeshi lake.’ 20  “‘Kama malipo ya kazi kubwa aliyofanya ya kushambulia Tiro, nitampa nchi ya Misri kwa sababu walitenda kwa ajili yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 21  “Siku hiyo nitaichipusha pembe kwa ajili ya watu wa nyumba ya Israeli,*+ nami nitakupa* nafasi ya kuzungumza kati yao; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”

Maelezo ya Chini

Kuanzia mstari huu, neno “Nile” linarejelea mto huo na mifereji yake ya kumwagilia mimea maji.
Tnn., “utete.”
Tnn., “viuno vyao vipepesuke.”
Tnn., “amesema.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “nitawapa nguvu watu wa nyumba ya Israeli.”
Yaani, Ezekieli.