Ezekieli 30:1-26

  • Unabii dhidi ya Misri (1-19)

    • Shambulizi la Nebukadneza latabiriwa (10)

  • Nguvu za Farao zavunjwa (20-26)

30  Neno la Yehova likanijia tena likisema:  “Mwana wa binadamu, tabiri, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ombolezeni, ‘Ole, ile siku inakuja!’   Kwa maana siku hiyo iko karibu, naam, siku ya Yehova iko karibu.+ Itakuwa siku ya mawingu,+ wakati uliowekwa wa mataifa.+   Upanga utaishambulia Misri, na Ethiopia itakumbwa na hofu wakati waliouawa watakapoanguka huko Misri; Utajiri wake umechukuliwa na misingi yake imebomolewa kabisa.+   Ethiopia,+ Putu,+ Ludi na watu wote wa mataifa mbalimbali,* Na Kubu, pamoja na wana wa nchi ya agano,* Wote watauawa kwa upanga.”’   Yehova anasema hivi: ‘Wale wanaoiunga mkono Misri wataangamia pia, Na nguvu zake zenye kiburi zitashushwa.’+ “‘Kuanzia Migdoli+ mpaka Siene+ watauawa kwa upanga nchini,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.  ‘Watafanywa kuwa nchi yenye ukiwa zaidi, na majiji yake yatakuwa majiji yaliyoharibiwa kabisa.+  Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowasha moto huko Misri na wote walioungana naye watakapopondwa.  Siku hiyo nitawatuma wajumbe katika meli ili kuifanya Ethiopia inayojitumaini itetemeke; watashikwa na hofu katika siku hiyo inayokuja dhidi ya Misri, kwa maana hakika itakuja.’ 10  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitauangamiza umati wa Misri kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni.+ 11  Yeye na wanajeshi wake, taifa katili zaidi kati ya mataifa,+ wataletwa ili kuiangamiza nchi. Watachomoa panga zao na kuishambulia Misri na kuijaza nchi watu waliouawa.+ 12  Nitaigeuza mifereji ya Nile+ iwe nchi kavu na kuiuza nchi mikononi mwa watu waovu. Nitaifanya nchi na kila kitu kilichomo kiwe ukiwa kwa mkono wa wageni.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’ 13  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitaziangamiza pia sanamu zinazochukiza* na kuiharibu miungu ya ubatili ya Nofu.*+ Hakutakuwa tena na mkuu* anayetoka katika nchi ya Misri, nami nitaweka hofu katika nchi ya Misri.+ 14  Nitalifanya jiji la Pathrosi+ liwe ukiwa na kuwasha moto katika jiji la Soani na kutekeleza hukumu dhidi ya jiji la No.*+ 15  Nitalimwagia ghadhabu yangu jiji la Sini, ngome ya Misri, na kuwaangamiza wakaaji wa jiji la No. 16  Nitawasha moto nchini Misri; na jiji la Sini litashikwa na hofu na jiji la No litapenywa kwa nguvu na Nofu* litashambuliwa kweupe kabisa wakati wa mchana! 17  Wanaume vijana wa Oni* na Pibesethi watauawa kwa upanga, na majiji yatapelekwa utekwani. 18  Kule Tehafnehesi mchana utakuwa na giza nitakapovunja nira za Misri huko.+ Nguvu zake zenye kiburi zitakwisha,+ mawingu yatamfunika, na miji yake itapelekwa utekwani.+ 19  Nitatekeleza hukumu dhidi ya Misri, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’” 20  Na katika mwaka wa 11, mwezi wa kwanza, siku ya saba ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema: 21  “Mwana wa binadamu, nimeuvunja mkono wa mfalme Farao wa Misri; hautafungwa upone au kufungwa kwa kitambaa uwe na nguvu za kushika upanga.” 22  “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko dhidi ya mfalme Farao wa Misri,+ nami nitaivunja mikono yake, mkono wenye nguvu na ule uliovunjika,+ nami nitaufanya upanga uanguke kutoka mkononi mwake.+ 23  Kisha nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali.+ 24  Nitaitia nguvu mikono ya* mfalme wa Babiloni+ na kuutia upanga wangu mkononi mwake,+ nami nitaivunja mikono ya Farao, naye atalia kwa sauti na kwa maumivu makali kama mtu anayekufa mbele yake.* 25  Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babiloni, lakini mikono ya Farao italegea; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babiloni naye aunyooshe dhidi ya nchi ya Misri.+ 26  Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”

Maelezo ya Chini

Au “wote waliotoka katika mataifa mengine.”
Huenda inarejelea Waisraeli walioungana na Misri.
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “kiongozi.”
Au “Memfisi.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Yaani, Thebesi.
Au “Memfisi.”
Yaani, Heliopolisi.
Au “nitaongeza nguvu za.”
Yaani, mbele ya mfalme wa Babiloni.